WAANDISHI WA HABARI VIJANA WAPATIWA MAFUNZO YA KUTAMBUA TAARIFA SAHIHI KUELEKEA KIPINDI CHA UCHAGUZI.


NA MARYAM NASSOR

WAANDISHI wa Habari  Vijana wametakiwa kuisoma elimu ya Artificial Intellegence ‘AKILI UNDE’  na kuielewa kwani wao ndio kinga moja wapo ya kuhakikisha jamii haiyathiriki na Habari za Uongo( Mis information).

Akifungua Mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa Habari Vijana kutoka klabu za waandishi wa Habari wa Unguja na Pemba,  Mkurugenzi  kutoka Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania  (UTPC) Keneth Simbaya katika Ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Kijangwani Mjini Unguja.

Amesema, lengo la mafunzo hayo  ni kuwaandaa waandishi wa Habari vijana kutekeleza majukumu ya kihabari kwa weledi  na umahiri katika  kipindi hichi cha uchaguzi  ambacho kumekuwa kukishamiri Habari za uongo na Upotoshaji  mitandaoni.

 “ Kama munavyofahamu katika dunia ya sasa  ambayo imetawaliwa na matumizi mabaya na mazuri ya ‘AKILI UNDE’  hivyo lengo la mafunzo haya kwenu  ni kuona kwa namna gani munatambua   taarifa sahihi na zisizosahihi kupitia njia mbali mbali” amesema .

Mkurugenzi huyo, amewataka waandishi wa Habari kujifunza zaidi matumizi  sahihi ya ‘AKILI UNDE’  ili kuhakikisha  taarifa zinazosambazwa mitandaoni  kuweza kuelewa usahihi wake.

Akiwasilisha mada juu ya namna ya kuzitambua  Habari za Uongo na Ukweli Mkufunzi  wa maswala ya kimtandao Ephraim  Muchemi, amewataka  waandishi wa Habari kutumia program mbali mbali  kama vile  Tine eye na Google  ili kuweza kutambua taarifa hizo.

Amesema , lazima waandishi wa Habari wasome njia tofauti tofauti za kuthibitisha Habari za uongo na ukweli  kabla ya kuzisambaza ili kuepusha taarifa za upoteshaji zisisambae.

“ Kuna njia nyingi  zinaweza kusaidia katika kuzitambua Habari za Uongo na Upotoshaji  ikiwa ni picha, video au hata maelezo  unaweza kuingiza kwenye program ya  Google Lens,  Tin eye na nyenginezo kupata kujua usahihi wa  taarifa hizo” amesema Mkufunzi huyo.


Kwa upande wake, Afisa Programu kutoka UTPC  Andrew Marawiti,  amewataka  waandishi wa Habari hao kuendelea kuyafanyia kazi mafuzo hayo kwa vitendo  ili yaweze  kuwasaidia katika shughuli zao za kiuandishi.

“ Kuwa kwenu hapa leo haikuwa Bahati mbaya tambueni kuwa mulikuwa wengi sana kwenye  maombi ila nyinyi ndio tumeona munafaa zaidi  kutokana na maelezo yenu mulivyojielezea , hivyo basi tunaomba sana mukaendelee  kuyatumia mafunzo  haya kwa vitendo ili yaweze kuwasaidia zaidi “  amesisitiza .

Nao, Baadhi ya waandishi wa Habari waliyopatiwa mafunzo  hayo  Suleiman Tambuligeni kutoka Zanzibar Press Club (ZPC) na Muyaba Kombo kutoka Pemba Press Club (PPC)  wamesema  mafunzo hayo yamekuja muda muafaka na yatawasaidia katika kipindi hicho cha Uchaguzi Mkuu .

Akifunga Mafuzo hayo ya siku moja,  Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar ( ZPC) Abdalla Mfaume amesema  katika zama  hizi  za Maendeleo ya  Sayansi na Teknolojia  kumekuwa na Habari nyingi za  Uongo na Upotoshaji. Hivyo amewaomba waandishi hao kuyafanyia kazi  mafunzo hayo hasa kipindi hichi cha uchaguzi.

Mafunzo hayo ya siku moja, yamewashirikisha Waandishi wa Habari Vijana kutoka  katika klabu za waandishi wa Habari  wa Unguja na Pemba, ambayo yameandaliwa na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania ( UTPC) kwa ufadhili wa Nether land (NL).



                                   Mwisho

 

No comments

Powered by Blogger.