“NCCR–Mageuzi Yazindua Kampeni, Yaahidi Kurejesha Mitaji ya Wajasiriamali Walioathiriwa na Mikopo Kaushadamu”
NA MARYAM NASSOR,
MGOMBEA Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha NCCR
Mageuzi – Leila Rajab Khamis, amesema
kama akipata ridhaa ya kuiongoza Zanzibar atarudisha mitaji kwa wajasiamali
waliochukuwa mikopo ya kaucha damu na kuuwa mitaji yao.
Ameyasema hayo, huko katika viwanja vya Kibanda Maiti
mkoa wa Mji Unguja katika ufunguzi wa
kampeni za chama hicho.
Amesema , katika mazingira ya Zanzibar eneo moja la kukuza uchumi ni kuweka mazingira wezeshi kwa wajasiriamali na kukuza
mitaji yao bila ya kujihusisha na mikopo
umiza.
Amesema kuwa, masoko yamekuwa yakijengwa lakini wafanyabiashara wadogo wamekuwa wakisahauliwa na badala yake wanachukuwa mikopo ya kausha damu na kuuwa mitaji yao.
“ Sote tumekuwa
tukishuhudia wafanyabiashara wa kibanda
Maiti wametolewa Mjini na kuletwa hapa
ambapo mvua zikinyesha soko linageuka bwawa la kuogelea lakini mukinipa ridhaa
nitalijenga soko hili ndani ya siku 100 za utawala wangu “ amesema mgombea huyo.
Ameeleza
kuwa, ameona jitihada za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ya kujenga Mahospital
lakini bado changamoto ya Afya iko pale pale Madaktari hakuna.
Amesema
kuwa, Moja ya kipaumbele chake katika chama chao ni kuboresha huduma za afya na
atahakikisha anawapeleka wanafunzi wa kada ya afya kusoma nje ya nchi na kila
mmoja ataajiriwa karibu na sehemu anayotoka .
“ Nitachohitaji kutoka kwenu nyinyi wazanzibar wenzangu ni kunipa ridhaa ya kuwatumikia ili kuhakikisha naimarisha kila sekta muhimu kwa jamii yetu “ amesema.
Nae, Mgombea
Mwenza wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Everiny Munis akimnadi mgombea huyo amesema , wanataka
uongozi kwa sababu wamejipanga kuleta mageuzi ya kila sekta ikiwemo kwenye siasa, afya na kiuchumi nchini.
Amesema
kuwa, Zanzibar ni tajiti na imejaaliwa utajiri wa kutosha unaotokana na Bahari na
Uchumi wa buluu lakini hakuna anaonufaika nao.
“Tunataka kuleta mageuzi kwa kuwa na Uvuvi wa kisasa na Uchumi jumuishi kila mmoja afaidike kutokana na utaalamu alionao , suala la ajira halitokuwa tatizo endapo mutaichagua NCCR Mageuzi “ amesema
Nae, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho kwa upande wa Tanzania bara, Martin Bernad
amesema kwa mujibu wa Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania vyama vyote 19
ni halali kugombea na kushinda.
Amesema
kuwa, akimnukuu Rais wa kwanza wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mwalim Julius Kambarage Nyerere amewahi kusema kuwa, nchi
inahitaji mambo manne ili iendelee.
Akiyataja mambo hayo, la kwanza amesema ni watu, la pili ni ardhi, la tatu ni siasa safi na la nne ni uongozi bora , baadhi ya mambo hayo yapo lakini siasa safi na uongozi bora utapatikana endapo wananchi watakichagua chama hicho.
Aidha akiwanadi wagombea Ubunge, Uwakilishi na Udiwani wa Chama hicho amesema watanzania kama wanataka kuchagua wanataka muungano wa namna gani basi wakichaguwe chama hicho.
“ Sote
tunajua suala la Muungano wetu haliwezi kuwa ni maamuzi ya chama Fulani ni muhimu wananchi wenyewe tuamuwe
muungano wa namna gani tunautaka hivyo hayo yatafikiwa endapo mutakichaguwa
chama chetu “ amesema Naibu Katibu Mkuu huyo.
Mwisho




Post a Comment