WANAWAKE WANAHITAJI NAFASI ZA UONGOZI ILI KULETA MABADILIKO NCHINI,


Na Maryam Nassor

Katika jamii ambayo mara nyingi nafasi za uongozi huonekana kama  ni ngome ya  wanaume, si jambo jepesi kwa mwanamke kunyanyuka na kudai nafasi yake.

Ni safari ngumu inayohitaji uvumilivu, ujasiri na kujitolea bila kuchoka, Njia hiyo ndefu imewafanya wengi kukata tamaa, wakihisi mzigo huo una changamoto kubwa kuliko ndoto zao.

 Hata hivyo, wapo wachache waliothubutu kusonga mbele bila kuyumbishwa na vikwazo. Kwa uthubutu huo wameweza kubadilisha mitazamo y a muda mrefu kwamba uongozi ni eneo la wanaume pekee, na kuonesha kuwa nafasi hiyo ni ya wote wenye maono na uwezo wa kuongoza.

Katika taswira hiyo, Machavu Bakar Juma ameibuka kama sauti mpya inayothibitisha kuwa uongozi si suala la jinsia, bali ni uwezo, maono na dhamira ya kweli ya kuwatumikia wananchi.

Kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Machavu   ameonesha matumaini mapya kwa jamii yake na wananchi wa Zanzibar  kwa ujumla.

Machavu ambaye  alizaliwa miaka ya 1965 huko  Mjimbini wilaya ya mkoani Kisiwani Pemba,  katika familia ya  Mzee Bakar Juma  akiwa ni  mtoto wa nne wa Familia hiyo.

 Elimu yake ya msingi na sekondari aliipata katika skuli ya Muembe Makumbi, kabla ya kuendelea  na masomo ya sekondari katika skuli ya Darajani, Mjini Unguja.

“Nilipokuwa skuli, ndoto yangu kubwa ilikuwa kuona wanawake wakishiriki katika siasa si kama wapiga kura pekee, bali kama watunga sera na watekelezaji wa mabadiliko,” amesema Machavu.

 Elimu hiyo ilimfungulia   milango ya ajira  katika chama cha CUF ambapo alihudumu katika nafasi ya  Mwenyekiti wa Wilaya ya Mjini na Mjumbe wa Kamati kuu ya chama Taifa.

Mwaka 1992, alijiunga rasmi na siasa kupitia Chama cha Wananchi CUF, kilichojulikana kwa msimamo wake wa haki, uwazi na uwajibikaji. Safari yake ya kisiasa ilianza kuchukua mwelekeo mpya .


Machavu hakupata mafanikio mara moja. Mwaka 2010 aligombea uwakilishi wa nafasi maalum za wanawake, lakini hakufanikiwa.

 Mwaka 2015 alijitosa tena kwenye nafasi ya uwakilishi lakini kura hazikutosha. Hata hivyo, juhudi zake hazikuishia hapo na mwaka 2020 aligombea uwakilishi wa nafasi za viti maalum na uchaguzi ulighairishwa.

Lakini,  Kupitia mafunzo aliyopata kuhusu wanawake na uongozi kutoka Chama cha Waandishi wa  Habari Wanawake  TAMWA ZNZ  yalimjenga na kumfanya  kuwa na ndoto kubwa ya kugombea katika  jimbo .

“ Baada ya kupata mafunzo mara kwa mara ya wanawake na uongozi kutoka taasisi mbali ikiwemo TAMWA ZNZ, nimeshawishika kugombea kwenye jimbo na ndoto yangu hiyo imetimia” amesema Bi Mashavu.

 Mashavu ambaye ni mgombea Ubunge jimbo la Chumbuni kupitia chama cha ACT Wazalendo,  chama ambacho amejiunga mwaka 2020 baada ya kuhudumu kwa miaka 19 katika chama cha CUF.

 Amesema, wanawake wana uwezo mkubwa kuliko wanaume  katika kuongoza  kwani wanayajua madhila yanaowafika wananchi na wana hamuya  kuitumikia   jamii.

   Maashavu ambaye kwa sasa anakaimu nafasi ya Katibu Mwenezi Mahusiano ya Umma Ngome ya Wanawake  ACT Wazalendo Tanzania nzima , amesema ana uzoefu mzuri wa kuongoza na kuwatumikia wananachi.

 “ Kupitia nafasi nyingi nilizohudumu  nimepata uzoefu mkubwa wa kuwatumikia wananchi wezangu wa Zanzibar hivyo  najiamini kugombea nafasi hii “ amesema .

   
Kama kiongozi mwanamke, Machavu amekutana na changamoto nyingi zikiwemo ukosefu wa mtaji wa kisiasa na mitandao ya muda mrefu ambayo mara nyingi hutumiwa na wanasiasa wakongwe.

 Katika mazingira ya siasa za Zanzibar, ambako mara nyingi zinatawaliwa na  mifumo dume ,  mwanamke  kugombea nafasi ya uongozi si jambo rahisi .

“Wapo waliokuwa wakiniambia siwezi kufanikisha ndoto zangu kwa sababu mimi ni mwanamke na sina uzoefu mkubwa wa siasa. Lakini niliona ni lazima kubadili mtazamo huo kwa vitendo, si maneno,” amesema Machavu.

Kwa Machavu, siasa si jukwaa la kujitafutia heshima binafsi, bali ni njia ya kubadilisha maisha ya wananchi.


“Siasa ni dhamana. Kila kura ya mwananchi ni ahadi kwamba nitafanya kazi kwa niaba yao, si kwa faida yangu binafsi,” amesema.

Kwa mujibu wa  Katibu Mwenezi wa chama cha ACT Wazalendo  Salim Diman , anamzungumzia Mashavu kama    kiongozi muelewa , mchapakazi na mpenda maendeleo  ambaye  amepata mafunzo ya uongozi sehemu mbali mbali ikiwemo TAMWA ZNZ.

“Machavu   ni kiongozi ambaye ni mpigania demokrasia na mpenda Maendeleo anawakilisha kizazi kipya cha wanasiasa wanaoamini kwenye hoja na uwajibikaji zaidi kuliko siasa za majukwaa na kelele “ anasema  Salim.

Fatma Kassim, mkaazi wa Chumbuni, anamwona Machavu kama ushahidi kwamba wanawake wanaweza kushika nafasi kubwa za uongozi iwapo watapewa nafasi na kuaminiwa.


 “Ni mfano wa kiongozi anayechanganya elimu, maadili na maono ya kisiasa, katika wakati ambapo jamii nyingi bado zinahofia kuwapa wanawake uongozi,” amesema Fatma .

MWISHO

No comments

Powered by Blogger.