Uhalisia wa Usawa wa Kijinsia Zanzibar Katika Uchaguzi na Hadithi za Wagombea Walioshindwa Kurejesha Fomu
Na Maryam Nassor
Zanzibar imekuwa ikijitahidi kutekeleza mikataba ya kimataifa kuhusu usawa wa
kijinsia, ikiwemo CEDAW na Beijing Platform for Action,
kwa kuhakikisha wanawake wanashiriki katika uongozi wa kisiasa.
Hata hivyo, pamoja na uwepo wa sera na nafasi za viti
maalumu, bado safari ya mwanamke kufika kileleni mwa uongozi hasa katika ngazi
ya juu kama urais imejaa changamoto kubwa. Uchaguzi wa hivi karibuni umeweka
wazi pengo hili.
Baadhi ya wagombea wanawake walishindwa hata kurejesha fomu
kwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), jambo lililoibua mjadala mkubwa juu ya
mazingira ya siasa na nafasi ya wanawake.
Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya 2022,
Zanzibar ina jumla ya watu 1,889,773, kati ya hao wanawake
wakiwa 974,281 (51.6%) na wanaume 915,492 (48.4%).
Wanawake ni wengi ukilinganisha na wanaume kwa idadi ya watu,
lakini hali hiyo bado haijaakisiwa ipasavyo katika nafasi za uongozi wa
kisiasa.
Naima Salum Hamad mwanamke wa miaka
48 kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja amejipanga
kugombea nafasi ya urais kupitia chama
chake cha upinzani cha United
Democratic Party (U DP) .
Ana elimu ya juu na
uzoefu wa kufanya kazi katika harakati
za kisiasa Visiwani Zanzibar kwa muda mrefu .
Lakini hatua ya kuchukua fomu ya kugombea,amegundua
gharama kubwa zinazohitajika kwa dhamana
ya kugombea fedha za kuchapisha nyaraka, safari
za kampeni, na ada ya uchaguzi.
“Nilikuwa
na ndoto kubwa ya kuonyesha kuwa mwanamke anaweza, lakini ukweli ni kuwa siasa
inahitaji fedha nyingi. Nilishindwa kukusanya hata nusu ya kiasi
kilichohitajika ndani ya muda mfupi,” ameeleza kwa masikitiko Naima .
Naima, hakuweza kurejesha fomu yake ZEC, na hivyo jina lake
halikuwahi kuingia kwenye mchujo wa wagombea kwa kukosa udhamini . Hii
inaonyesha wazi jinsi vikwazo vya kiuchumi vinavyoweza kumzuia mwanamke kufikia
ngazi za juu za uongozi.
Naima siyo pekee yake aliyeshindwa kurudisha fomu ZEC kuna na wengine na mmoja wao ni Isha Salim Hamad .
Isha Salum
Hamad ni kiongozi mwandamizi ndani ya Chama Cha Kijamii (CCK) Zanzibar, amepata
uungwaji mkono wa ndani awali kuwania urais.
Lakini changamoto zilianza
baada ya kuchukua fomu. Ndani ya chama, kulianza mivutano ya makundi, na baadhi
ya viongozi hawakumwona kama mgombea atakayeweza.
“Nilishangaa
kuona jina langu linaondolewa katika orodha ya waliopendekezwa dakika za
mwisho, eti kwa sababu sikuwakilisha maslahi ya chama kwa nguvu sawa na
wanaume,” amesema Isha.
Kwa hali hiyo, amekosa msaada wa chama chake katika
mchakato wa kurejesha fomu ZEC, na hatimaye amebaki nje ya kinyang’anyiro.
Hadithi hizi mbili zinagusia changamoto kuu zinazowakumba
wanawake wakati wakijitosa kugombea nafasi mbali mbali za uongozi wa kisiasa.
Awali, Mashirika yanayojihusisha na masuala ya
wanawake na uongozi Zanzibar yamewapongeza wanawake 13 nchini waliogombea
nafasi za uraisi na Makamu wa Rais katika
Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Mashirika hayo
ni Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar ( TAMWA ZNZ,
Chama cha Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) Jumuiya ya Wanawake wenye
Ulemavu ( JUWAUZA) na PEGAO, yamesema
idadi hiyo ni sawa na asilimia 36 kati ya wagombea waliochukua fomu kutokaTume
ya Uchaguzi ya Taifa (INEC) ambao jumla yao ni 36 katika ngazi ya Uraisi
naUmakamo.
Taarifa hiyo imesema kuwa, upande
wa nafasi ya Uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inagombewa na wanawake
watatu ambao ni pamoja na Raisi aliyepo madarakani Dk. Samia Suluhu Hassan
anaegombea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) huku Bi Mwajuma Mirambo akigombea
kupitia Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD) na Bi Swaumu Rashid
kutoka Chama cha United Democratic Party (UDP).[U1]
Idadi hii imeweka
rikodi katika historia ya nchi tokea kuanza kwa siasa za vyama vingi mwaka
1995. Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, kati ya wagombea 30 wa nafasi ya Uraisi na
Makamu wa Raisi, wanawake walikuwa 7 pekee sawa na asilimia 23.3, Kati ya hawa
watano (5) ndio waliotoka Zanzibar.
Almas Mohamed ni
mchambuzi wa maswala ya wanawake na uongozi Zanzibar amesema, vikwazo vya
kifedha gharama kubwa za uchaguzi zinawakatisha tamaa wanawake wengi.
Amesema kuwa, Uhusiano wa ndani ya
vyama mara nyingi vyama havitoi nafasi sawa, na wanawake hupuuzwa au
huachwa nyuma kwa misingi ya mitazamo ya kijinsia.
Aidha amesema kuwa, Mitazamo ya
kijamii baadhi ya jamii bado inaamini uongozi wa nafasi ya urais ni wa wanaume pekee na wanawake hawatakiwi wafike hapo.
“Licha ya Zanzibar kuwa na wanawake wengi katika idadi ya
watu na jitihada zinazochukuliwa za kuongeza ushiriki wao katika siasa, hadithi za wagombea walioshindwa
kurejesha fomu ZEC zinaonyesha kuwa bado kuna pengo kubwa”, amesema Sera na mikataba ya kimataifa ipo, lakini
utekelezaji wake unakwamishwa na changamoto za kifedha, mfumo wa vyama na
mitazamo ya kijamii.
Kwa maneno mengine, idadi ya majina ya wagombea
wanawake yanayorudi si kielelezo tosha cha dhamira ya kimataifa—bali ni kioo
cha changamoto halisi ambazo wanawake wanapitia katika safari ya siasa
Zanzibar.
Mwisho

Post a Comment