SHERIA NZURI YA HABARI NI HAKI YETU TUENDELEE KUFANYA UCHECHEMUZI -TAMWA ZNZ

NA MARYAM NASSOR

CHAMA Cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA ZNZ) kimewataka wandishi wa Habari  kuendelea kufanya uchechemuzi wa sheria rafiki za Habari ili zipatikane kwa haraka.

Akizungumza katika kikao  cha  wadau wa Maswala ya Habari  na wandishi wa Habari huko katika Afisi za chama hicho Tunguu , Afisa  Programu   wa  sheria za Habari   kutoka chama hicho Zaina Mzee

 Amesema , ingawa mradi huo wa uchechemuzi wa maswala ya  sheria za Habari unamaliza muda wake lakini wandishi waendelee kuandika  Habari na Makala ili wenye mamlaka waendelee kusikia kilio cha wandishi.

“Mradi huu ulikuwa ni wa miaka miwili tu  na unamalizika, ikiwa sheria hiyo haijapatikana  lakini hatua kubwa tumepigwa kwa wandishi wa Habari wamepata  uwelewa na wenye mamlaka wamesikia kilio chetu” 

 Amesema kuwa,   ingawa sheria hiyo haijapatikana  lakini hatua kubwa imepigwa  kwani wandishi wa Habari  wamepata uwelewa kuhusu  kutetea zao na  haki za wananchi.

“ Mradi huu unamalizika lakini umeonesha mafanikio makubwa kwani kule Pemba wandishi wamepata uwelewa mzuri  hadi kuzuia mchele mbovu wasiuziwe wananchi “ amesema Zaina.

Amesema kuwa,  Lakini kitu kizuri  zaidi  Waziri pia kasikia kilio cha wandishi wa Habari cha kutaka mabadiliko ya sheria za Habari, kutokana na kuwa ni ya muda mrefu na ina vipengele ambavyo vinapinga uhuru wa Habari na kujieleza.

“ Mara nyingi Waziri katika vikao vyake amekuwa akilizungumzia  suala hili la sheria za Habari tunaamini amesikia kilio chetu cha muda mrefu na atalifanyia kazi “ amesema.

Nae,  Mjume wa Bodi ya  TAMWA  ZNZ  Bishifaa Said , akimuwakilisha  Mkurugenzi  wa Chama hicho Dk Mzuri Issa, amewashukuru wandishi wa Habari  kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kufanya uchechemuzi wa sheria za Habari.

Amesema kuwa,  hatua kubwa imepigwa kutokana na mradi huo waandishi wamepata uwelewa mzuri wa maswala ya sheria zinazominya uhuru wa  Habari.

“ Mradi unamalizika lakini waandishi wanaendelea kuwepo na kufanya kazi zao, hivyo ni vizuri wazidi kufanya uchechemuzi ili sheria nzuri ya Habari ipatikane” amesema  Bishifaa.

 Mohamed Hatib Mohamed ni Afisa Tathimini na Ufuatiliaji kutoka TAMWA ZNZ, amesema  , jumla ya  Habari na Makala  253 zimeandikwa katika mradi huo, 104 zikiandikwa kwa upande wa redio,  17 makala za gazeti na 132  habari za mitandao ya kijamii na  blog.

Aidha amesema kuwa, mafanikio makubwa  yamepatikana lakini pia isiishie hapo wandishi waendelee kufanya kazi ili mwisho wa siku sheria hiyo ipatikane.

 Nao, baadhi ya wandishi walioshiriki katika kikao  hicho  Huwaida Nassor  amesema kupitia mradi huo, pia imewasaidia wandishi wa Habari kurudi vyuoni kusoma ili itakapo patikana sheria hiyo  isijeikawabane kufanya kazi  zao kwa kutotimiza  masharti ya elimu.

                                  MWISHO

No comments

Powered by Blogger.