WAANDISHI WA HABARI WA ZANZIBAR WAPATIWA MAFUNZO YA ULINZI NA USALAMA


 NA MARYAM NASSOR

WAANDISHI wa Habari wa Zanzibar wamepatiwa mafunzo ya ulinzi na usalama  kuelekea uchaguzi  mkuu  wa  Oktoba mwaka, kipindi ambacho mara nyingi huwa hatarishi kwa wandishi wa Habari.

 Mafunzo hayo , ya ulinzi na usalama  yametolewa   August 6 na 7 , 2025  huko katika Afisi za TAMWA ZNZ Tunguu , na mkufunzi  Maryam  Nassor ambaye ni mwandishi wa Habari  baada ya kujengewa uwezo na  Umoja wa klabu  za Waandishi wa habari  Tanzania ( UTPC)  akimuwakilisha ToT Najjat Omar kutoka klabu ya wandishi wa Habari Zanzibar ( ZPC).

Amesema ,  waandishi wa Habari wanapaswa  kuwa makini  na kuchukuwa tahadhari  kwa kujilinda wakati wote  kwani ulinzi na usalama wa mwandishi huanza na mwandishi mwenyewe.  

 Amesema  kuwa, ulinzi na usalama wa mwandishi wa Habari  unaanza na  yeye mwenyewe hivyo ni lazima  kutambua mazingira anayofanyia kazi na watu anaofanya nao kazi , ili kujihakikishia ulinzi  na usalama  wake wakati akiwa kazini.

“ Waandishi  wa Habari lazima muwe makini katika kipindi hichi tunachoelekea kwani musipokuwa makini munaweza kuingia  kwenye matatizo  na kuhatarisha  maisha yenu “ amesema mkufunzi huyo.


Aidha amewataka wandishi wa  Habari kujilinda pia katika mitandao ya kijamii na kujiepusha kufungua viunganishi ( links) ambavyo sio  salama na hawajui vinapotoka.

 Amesema kuwa,   ni vyema wandishi wa Habari kulinda taarifa zao binafsi  zisifike kwa watu wasiohusika ili kuzuwia  udukuzi  na wizi wa taarifa.

 Nao baadhi ya wandishi waliyobahatika kupata mafunzo  hayo, Jesse Mikofu kutoka gazeti la mwananchi Zanzibar ameshauri ni vyema elimu kama hiyo kupewa na wamiliki wa vyombo vya Habari ili kusaidia kuwapatia vitendea kazi ambavyo vitasaidia kuwalinda.

Amesema kuwa, vyombo vingi vya Habari hawahamasishi waandishi wao, kuwa na vifaa vya kujilinda kama Press Jacket   na vyenginevyo wakati wa majanga.

Nae,  mwandishi   Samira Abdalla  kutoka  Zanzibar University online Tv , ameshukuru kupatiwa mafunzo hayo  ya ulinzi na usalama  hasa kuelekea kipindi hichi cha uchaguzi, na kuahidi kuyafanyia kazi.

Mafunzo hayo ya  siku mbili, ya  ulinzi na usalama wa kimwili , kidigital na Afya ya akili   kwa waandishi wa  Habari yanalenga  kuimarisha  ulinzi na usalama kwa wandishi wa Habari kuelekea kipindi cha uchaguzi.

                             mwisho    

No comments

Powered by Blogger.