UWELEWA MDOGO WA WANANCHI KUHUSU SHERIA YA MITANDAO YA KIJAMII
NA MARYAM
NASSOR
KATIKA karne
ya 21 mitandao ya kijamii imekuwa sehemu muhimu ya mawasiliano, inakuza biashara , siasa na hata sekta ya elimu.
Kutokana na
ukuaji wa teknolojia, mataifa mengi yameanzisha sheria za kusimamia matumizi ya
mitandao.
Hata hivyo,
licha ya nia njema ya Serikali ya kuwalinda wananchi na kuhakikisha usalama wa
taarifa, sheria hizi zimekuwa na mapungufu mbali mbali yanayo weza kuathiri
uhuru wa kujieleza, faragha na maendeleo ya teknolojia.
Sheria ya
makosa ya kimtandao namba 14 ya
mwaka 2015, kifungu cha 22 kinaeleza kuwa mtu ambaye kwa
makusudi na kinyume cha sheria ataharibu
, atafuta ,ataondoa ataficha ,
atabadilisha au ataifanya data
komputa kukosa maana kwa lengo la kuharibu Ushahidi
au kuchelewesha upelelezi atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini ya kiwango kisichopungua milioni
tatu au kutumikia kifungo kwa muda usiopungua mwaka mmoja au vyote.
Kipengele
hichi ni bora kiainishe katika mazingira
yapi kufuta data ni kosa, kwani kuna matumizi
mengi ya data yakiwemo ya mtu
binafsi, ya taasisi kulingana na kazi husika.
Pamoja na
kukuwa kwa matumizi ya teknolojia lakini
bado watanzania wengi hawaifahamu sheria
hii na inawahusu kwa namna gani kwani
watu wengi wanatumia mitandao ya kijamii .
Kwa mujibu wa
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) kuna watanzania milioni 33 hadi Machi 2023 walikuwa
wanatumia huduma za intaneti huku mitandao ya facebook ikiongoza kwa
matumizi makubwa ya bando.
Ripoti hiyo,
inaonyesha mwenendo wa sekta ya mawasiliano nchini kwa kipindi cha miezi ya
January hadi machi 2023, watanzania milioni 33 walikuwa wanatumia huduma za
inteneti ambayo ni sawa na asilimia 53.4
ya watanzania wote.
Idadi hiyo,
ya watumiajiwa intaneti imeongezeka kwa asilimia 48 hadi machi 203
ikilinganishwa na idadi ya mwaka 2018 iliyokuwa watu milioni 22.3
Sheria hizi hazijaweka mipaka ya wazi kuhusu nini
kinachohesabika kama matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kwa mfano maneno
kama uchochezi, au kuharibu maadili ya jamii au tishio kwa usalama wa taifa
hutumika bila ya ufafanuzi wa kitaalamu
hivyo kutoa mwanya kwa mamlaka kutumia sheria hizo vibaya .
Akizungumza na mwandishi wa Makala hii, mwanasheria Ali Amour anasema bado wananchi hawana
uwelewa na sheria hizi kwani elimu haitolewi .
Anasema
kuwa, watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii ni vijana ambao hawajielewi ,wanakesha mitandaoni bila
ya kazi muhimu, hivyo kubwa wanalolifanya ni kujiposti na kuzima data.
“ Watumiaji wengi wa mitandao hawana uwelewa
na sheria ya mitandao ya kijamii namba 14 ya
mwaka 2015 hivyo ni vyema elimu
ikatolewa ‘’anasema mwanasheria huyo.
Nae, Mkurugenzi wa Shirika la Msaada wa
kisheria na Haki za Binadamu ( ZALHO) Harusi Miraji Mpatani anasema wananchi wengi
hawazijui sheria kutokana na kuwa , sheria
hizo hazisomeshi kwa wananchi.
Anasema
kuwa, ni vijana wachache utakao wakuta wanajua kama kuna sheria ya mitandao ya
kijamii na hao labda wameisoma sehemu.
“ Tujitahidi
kutoa elimu kwa wananchi ili wapate uwelewa wa sheria mbali mbali ili iwe
rahisi kwao kujitetea na kuzitumia sheria hizo” anasema Harusi.
Nao, baadhi
ya wananchi wa Fuoni meli tano Farina Ali na Saumu Juma wanasema wao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii
lakini hawajui kama kuna hata hiyo sheria ya mitandao ya kijamii.
Wanasema kuwa, hawana uwelewa na sheria hiyo,
na kuiomba mamlaka husika kutoa elimu ili jamii ipate uwelewa.
Nae, Mkuu wa
Chuo cha Uandishi wa Habari na
Mawasiliano ya Umma Zanzibar Imane Os Duwe, anasema dunia ikisherehekea ukuaji wa Teknolojia
kwenye eneo la Habari , lazima wandishi wa Habari wawe huru katika kazi zao.
Anasema
kuwa, sheria kandamizi lazima zifanyiwe kazi ili kutoa uhuru kwa wandishi wa
Habari kufanya kazi zao kwa amani na utulivu.
“ Kutokana
na kukuwa kwa Teknolojia dunia imekuwa
kama Kijiji na wandishi wa Habari wanataka uhuru wa kufanya wajibu wao” anasema
Duwe.
Daktari
Mzuri Issa ni Mkurugenzi wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania
(TAMWA ZNZ) anasema dunia ya sasa
inahitaji kufanya mambo kwa kasi inayoendana na wakati uliyopo sasa.
Anasema
kuwa, huu sio wakati tena wa kuwekewa vikwazo kila kona kwa wandishi wa Habari
kutokufanya kazi zao kwa ufasaha.
“ Tunataka
sheria kandamizi zifanyiwe marekebisho ili kuwapa uhuru wandishi wa Habari
kuwajibika kwa wananchi” anasema Dk Mzuri.
mwisho

Post a Comment