ZAMECO YAITAKA TUME YA UCHAGUZI ZNZ, KUZIFANYIA KAZI CHANGAMOTO ZA WANDISHI.

NA MARYAM NASSOR

KAMATI  ya waatalamu wa maswala ya Habari Zanzibar  ( ZAMECO)  imeitaka  tume ya uchaguzi   kuzifanyia kazi changamoto za wandishi wa Habari  kuelekea uchaguzi mkuu   2025.

 Tume ya uchaguzi  nchini  ( ZEC) ina jukumu la kuzifanyia kazi changamoto mbali mbali za uchaguzi zinazojitokeza  mara kwa mara hasa katika kipindi cha uchaguzi  ili kutoa  uhuru kwa vyombo vya Habari kufanya kazi zao kwa uhuru na  utulivu.

Sheria ya kufuta sheria ya uchaguzi namba. 11 ya mwaka 1984 na kutungwa sheria ya uchaguzi ya mwaka 2017 na maswala mengine yanayohusiana nayo.

Katika sheria hii, kuna kifungu cha 122   ambacho kinakizana na uhuru wa vyombo vya Habari nchini, ambacho kifungu hicho kinasema ‘’

‘’ Mtu yeyote  ambaye, atachapisha, atatoa chapisho  au atasababisha  kuchapishwa au kutolewa chapisho, au  atabandika au atasababisha kubandikwa au atasambaza au  atasababisha kusambazwa mabango au posta yanayohusiana na uchaguzi au kampeni za uchaguzi bila ya kuwa na

(a) ruhusa ya tume  au msimamizi wa uchaguzi kwa kadri itakavyofaa.

(b)                        Anuani ya mchapishaji

 

Atakuwa amefanya kosa na akipatikana na hatia atalipaa faini isiyozidi shilingi milioni tano na isiyopungua shilingi laki tano au atatumikia kifungo kwa kipindi kisichopungua miezi sita na kisichozidi mwaka mmoja au adhabu zote faini na kifungo

Akizungumza katika  madhimisho ya siku   ya uhuru wa vyombo vya Habari duniani 2025 , huko katika ukumbi wa Rahaleo Mjini Unguja  Katibu wa Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar  ( ZPC)  Mwinyi mvua Nzukwi kwa niaba ya  Mwenyekiti wa Club hiyo Abdalla Mfaume,  amesema tume ya uchaguzi lazima  izingalie changamoto za wandishi wa Habari kwani wao wapo kwa ajili ya kuwahabarisha  wananchi.

Amesema kuwa, jukumu la kukusanya na kutoa taarifa kwa wandishi wa Habari ni haki ya msingi na kisheria, hivyo serikali ina wajibu ya kuwalinda wanahabari ili kuweza kuihabarisha jamii bila ya kukumbana na changamoto zozote.

“ Jukumu la kukusanya  na kutoa taarifa kwa wandishi wa Habari  ni haki yao ya  msingi na ipo kisheria hivyo Serikali ina wajibu wa kutulinda ili kutimiza wajibu wetu wa kuihabarisha jamii” anasema   Nzukwi.

Aidha amewataka   wandishi wa Habari  kufuata madili ya  kazi zao, katika kipindi cha uchaguzi   ili kuepuka  kusababisha  kupotea  kwa amani  katika kipindi cha uchaguzi.

Salim Said , ni mwandishi mkongwe  wa Habari visiwani Zanzibar  anasema  uhuru wa Habari na haki ya kujieleza ni jambo muhimu litakalo pelekea mabadiliko Chanya kwa taifa.

Anasema , ili haki hiyo iweze kupatikana kikamilifu ni vyema mamlaka za nchi zikaifanyiakazi sheria zinazokizana na uhuru wa Habari na kuzirekebisha  ili kuondoa changamoto  zinazoikabili tasnia hiyo.

Anasema kuwa,  kuna sheria mbali mbali ambazo haziko sawa kwa wandishi kuziripoti kutokana na kufungwa kwa sheria hizo  kama sheria ya uchaguzi.

 “ Ni  vyema mamlaka zikaiangalia upya sheria hizi ili kutoa uhuru wa vyombo vya Habari nchini” anasema Salim.

  Nae,  Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Taifa  cha Zanzibar  ( SUZA)  ambae pia ni mjumbe wa chama cha Wandishi wa Habari Wanawake  Tanzania Zanzibar ( TAMWA ZNZ)  Imane Os. Duwe amesisitiza kuwa tume ya uchaguzi inapaswa kutoa mafunzo kwa wandishi wa Habari yatakayo Saidia kuzifahamu sheria za uchaguzi na namna ya kuripoti tukio hilo bila ya Kwenda kinyume na sheria hizo.

 Anasema kuwa,  wandishi wengi hawana uwelewa wa kuripoti Habari za uchaguzi hususani kuhusu matokeo hivyo ni  vyema tume ya uchaguzi kutoa elimu hiyo.

 

“Tume ya uchaguzi ni vyema ikatowa mafunzo kwa wandishi wa Habari ili kutoa uwelewa  wa kuziripoti Habari za uchaguzi” anasema Imane.

  Nae, mwanasheria Ali Amour kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, anasema sheria ya uchaguzi  si rafiki kwa wandishi wa Habari kutokana vifungu vinavyokizana na uhuru wa vyombo vya Habari.

 

Anasema kuwa, ni vyema tume ya uchaguzi ikavifanyia kazi  vifungu vinavyowabana wandishi wa Habari  ili wakapata uhuru wa kuripoti Habari za uchaguzi wa mwaka huu.

“ Ni lazima sheria hiyo ibadilishwe ili iwape nafasi wandishi wa Habari kuripoti kwa uwazi Habari za uchaguzi” anasema Ali.

Nae, Afisa Programu wa Maswala ya utetezi na Uchechemuzi kutoka Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar ( TAMWA ZNZ)  Zaina Abdalla Mzee anasema  wamekuwa wakichukuwa jitihada mbali mbali za kuzisemea sheria zote zinazohusu  habari ambazo haziko huru.

“ Tumekuwa tukipaza sauti zetu kwa muda mrefu sasa kupatikana sheria nzuri ambazo ni rafiki kwa wandishi na vyombo vya Habari” anasema Zaina.

Hata hivyo, ameeleza mikakati waliyojiwekea katika kupaza sauti zao juu ya mapungufu yaliyomo katika sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya uchaguzi na sheria ya  Habari Zanzibar ambayo mpaka sasa haijulikani ipo katika hatua ipi.

 

                                     MWISHO

No comments

Powered by Blogger.