UWT , YAIPONGEZA TUME YA UCHAGUZI ZNZ KWA PUNGUZO LA ASILIMIA 50 KWA WAGOMBEA WANAWAKE.
NA MARYAM NASSOR
UMOJA wa Wanawake Tanzania( UWT) wa chama cha Mapinduzi (CCM) wameipongeza tume ya Uchaguzi Zanzibar ( ZEC) kwa kutoa punguzo la asilimia
50 kwa
wanawake wanaotaka kugombea nafasi mbali mbali za uongozi katika
uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Akizungumza na mwandishi wa Habari hizi katika
ofisi za chama hicho Kisiwandui mkoa wa
mjini Unguja, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa wanawake Tanzania( UWT) upande
wa Zanzibar Tunu Juma Kondo, amesema tume imewajali na wao kama umoja wa
wanawake wameanza harakati mbali mbali za kuwahamasisha wanawake wagombee katika
majimbo.
Amesema,
wanajua wanawake wanazo nafasi za viti maalumu lakini uchaguzi wa mwaka huu wanataka wanawake wajitokeze kugombea
katika majimbo katika nafasi mbali mbali
za uongozi ili 50/ 50 ifikiwe.
“ Uchaguzi
wa mwaka huu tunataka 50/50 ifikiwe hivyo tunawasihi wanawake wajitokeze kwa
wingi kugombea nafasi mbali mbali za
uongozi ili kuongeza ushiriki wetu”
Amesema kuwa,
mwamko ni mkubwa kwa wanawake wanaotia
nia ya kugombea ukilinganisha na miaka
ya nyuma kutokana na kupata hamasa ya
kuona kiongozi wa juu wa nchi ni
mwanamke tena anaongoza Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
“ Kiukweli
mwaka huu wanawake vijijini na mjini wote wameonesha hamasa ya kugombea kila mmoja anatangaza nia ya kugombea nafasi
za uongozi kutokana na kupata mfano mzuri wa kuiga” anasema Tunu.
Aidha
amesema kuwa, wanawake wengi wamehamasika
kumuona mama Samia ni Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania hilo limeatia moyo na ujasiri kuamini kuwa wanaweza.
Ametoa wito
kwa wanawake, kila mwenye nia ya kugombea
nafasi za uongozi ajitokeze na ana wahamasisha wanawake
wawachaguwe wanawake wenzao kwanza kwa lengo la kufikia 50/50.
Hivi karibu,
tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ( ZEC) kupitia
Mwenyekiti wake Jaji George
Joseph Kazi imetangaza punguzo la asilimia 50 kwa wanawake wanaotaka kugombea nafasi
mbali mbali za uongozi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Jaji Kazi,
ameeleza hayo katika mkutano na wadau wa
uchaguzi wa utoaji tathimini ya uwandikishaji wapiga kura wapya awamu ya pili
kilichofanyika katika ukumbi wa Shekh Idrissa
Abdul Wakil Kikwajuni mjini Unguja.
Mwisho

Post a Comment