VIJANA TUMIENI SEKTA YA MICHEZO KUJIAJIRI
Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar imefanya mageuzi makubwa katika sekta ya michezo kwa kujenga viwanja vya kisasa vya
michezo mbali mbali visiwani Zanzibar.
Michezo ni
fursa kwa vijana kujiajiri, kwani ndio sekta inayoongoza kwa kutoa mishahara
mikubwa kwa wachezaji wake.
Akizungumza
na mwandishi wa Makala haya, Mrajisi wa Vyama vya michezo Abubakar Mohamed Lunda amesema kwa
sasa sekta ya michezo Zanzibar imekuwa
na vijana wengi wanazitumia fursa hizo
kujiajiri.
Amesema
kuwa, michezo ni
Sekta ambayo inawainua vijana wengi
kiuchumi na hapa Zanzibar wachezaji wengi tayari wamejiajiri kupitia
michezo mbali mbali.
“ Ni vizuri
vijana wetu kuitumia fursa za michezo kujiajiri kuliko kutegemea ajira kutoka
Serikali ambazo haziwezi kuajiri watu
wote’’ ameshauri Lunda.
Aidha amewataka
vijana kuchangamkia michezo, ambapo Raisi wa Zanzibar amekuwa mstari wa mbele
kuimarisha Sekta hiyo kwa kujenga
Viwanja vya kisasa .
Bi Nasra Juma
ni kocha wa mpira wa miguu katika
kikosi cha Uhamiaji Zanzibar amesema michezo ni fursa nzuri kwa vijana
kujiajiri na kuondokana na ukosefu wa
ajira.
Amesema
kuwa, michezo kwa sasa ni ajira ni pesa tofauti na zamani kwani wachezaji wa
mpira wa miguu na michezo mingine wanalipwa vizuri na wanaendesha Maisha yao
kwa kujiajiri katika sekta hiyo.
Aidha amesema kuwa, ni vyema vijana wanaomaliza vyuo au skuli wasipoteze
muda wao kushinda katika vijiwe viovu na badala yake kuitumia michezo kujenga
afya zao lakini pia kujiajiri.
“
Tumeshuhudia katika awamu hii ya Raisi
Mwinyi amekuwa akiwekeza katika sekta ya michezo ni vyema vijana wetu kuitumia
michezo kujiajiri” ameshauri Nassra.
Amesema kuwa, familia ni vyema kuwasaidia
Watoto wao kutimiza ndoto zao za kimichezo , ile dhana ya michezo ni uhuni
haipo tena , kwani ipo mifano mingi ya wachezaji
wanawake na wanaume wanaolipwa mishahara mizuri na kuishi kifahari kutokana na
michezo.
Nae,
mchezaji wa mpira wa miguu kutoka timu ya
Mahonda FC Ali Swaleh amesema kutokana na kukuwa kwa sekta ya michezo, sio
muda tena kwa vijana kulilia ajira kutoka Serikalini.
Amesema
kuwa, vijana wachangamkie sekta ya michezo kwa maendeleo ili kujiajiri, na kuondokana na utegemezi wa
ajira kutoka utumishi wa umma ambako hakuna ajira zinazoweza kuajiri vijana
wote wa Zanzibar.
“ Uzuri wa
michezo ni fursa kwa maendeleo sio lazima uwe umesoma sana ndio uajiriwe, ni
uwezo wako tu wa kusakata kabumbu “ amesema
Ali.
Amesema kuwa, mpira wa miguu ndio unaongoza kwa kuajiri wachezaji
wengi ukilinganisha na michezo mingine na hapa Zanzibar kuna
vipaji vingi .
Amesema kuwa, Katika uongozi wa Raisi Mwinyi
tumeshuhudia vijana wengi na wengine wadongo chini ya umri wa miaka 15
wanaiwakilisha nchi kupitia mpira wa miguu na kushinda na wengine kushiriki katika kombe la
Mapinduzi,” Zanzibar inaendelea kushika
kombe hilo , hii inaonesha Dhahiri kama tuna vipaji lakini vijana
hawajashirikishwa ipasavyo kwenye michezo ili tujiajiri” anasema mchezaji huyo.
Nae, Zubeda
Kassim kutoka timu ya mpira wa miguu ya
Wanawake ya Worries amesema kuwa, ni vyema Serikali kuwandaa mabonanza
maalum ikiwa ni kampeni kwa Watoto wa kike kushiriki na kuielimisha jamii juu ya dhana potofu
iliyoaminishwa hapo zamani ya michezo ni uhuni.
Amesema
kuwa, michezo ni fursa kwa wanawake kujiajiri lakini wengi wa Watoto wakike wa
kizanzibar wanaogopa kuzitumia fursa za michezo kwa kigezo cha dini.
“ Asilimia
99 ya wakaazi wa Zanzibar ni waisilamu watoto wa kike wanapenda kushiriki
michezo, lakini tunahofu na wazazi na jamii zitatuchukuliaje” anasema Zubeda.
Aidha
amewashauri wazazi , kuwasaidia Watoto wao kutimiza ndoto zao za kimichezo kwani Watoto wote hawana ndoto za
kuwa wahasibu wala madaktari, wana hamu kusakata kambumbu wasaidiwe wafike
mbali.
Khairat Haji ni Afisa Programu ya michezo kwa
Maendeleo kutoka Chama cha Wandishi wa
Habari Wanawake Tanzania kwa upande wa Zanzibar- TAMWA ZNZ amesema ni vyema
Watoto wa kike na wanawake kutumia fursa za michezo kujiajiri na kuachana na
zile kasumba za michezo ni uhuni.
Amesema
kuwa, mradi wa michezo kwa Maendeleo unahamasisha Watoto wa kike kushiriki
michezo na kujiajiri kupitia sekta hiyo kwani Serikali imekuwa ikijenga viwanja
vya kisasa kukuza sekta hiyo.
Post a Comment