WADAU WA MICHEZO WATAKA CHANGAMOTO ZA WATOTO WA KIKE ZITATULIWE ILI KUWAPA UHURU KUSHIRIKI MICHEZO .
NA MARYAM NASSOR
MICHEZO ni
sehemu muhimu ya Maisha ya kisasa, ikitoa fursa za afya, kutoa ajira, Maendeleo ya kijamii na umaarufu.
Hata
hivyo,wanawake wanakabiliwa na changamoto lukuki wanaposhiriki katika shughuli
za michezo mbali mbali nchini na baadhi
ya changamoto hizo ni ubaguzi wa kijinsia.
Akizungumza na mwandishi wa Makala hii, Saida
Saidi mchezaji wa mpira wa miguu katika timu ya worries anasema moja ya
changamoto inayowakabili wachezaji wa kike ni ubaguzi wa kijinsia, kwani mara
nyingi wanawake hawapati fursa sawa kama
wenzao wanaume katika mashindano mbali mbali .
“ Ukiangalia
sisi wachezaji wakike ligi zetu hazina udhamini, hii inatufanya iwe ngumu
kujitokeza kwa wingi kuonesha vipaji vyetu kama ilivyo kwa wanaume” anasema
mchezaji huyo .
Amesema
kuwa, ingawa kuna jitihada mbali mbali za kuboresha nafasi ya mwanamke katika
michezo , lakini bado kuna hitajika juhudi za ziada ili kuinua soka la wanawake.
Aidha
amesema kuwa, wanawake mara nyingi wanakabiliwa na changamoto za kifedha katika
michezo, ukosefu wa wadhamini na rasilimai fedha unawafanya wengi washindwe
kudhamini mafunzo na vifaa vyao vya
kimichezo.
Nae,
mchezaji wa mpira wa miguu kutoka timu ya New Generation Hafidha Juma amesema
matarajio ya wanajamii yanaathari kubwa katika maendeleo ya wanawake kwenye
michezo.
“Katika
jamii nyingi za kiafrika ,kuna mitazamo
kwamba wanawake hawawezi kuwa na mafanikio
sawa na wanaume katika michezo, hii inawafanya baadhi ya wanawake
kujihisi kushindwa hata kabla ya kujaribu”
anasema Hafidha.
Amesema
kuwa, mitazamo kama hiyo inaweza kuathiri ndoto za Watoto wakike wakiingia
katika michezo, wakifikiria ni sehemu
ambayo inaweza kuwajiajiri na kuendesha Maisha yao.
Nae,
mchezaji wa mpira wa miguu katika timu ya watu wenye ulemavu , Amina Simba, amesema changamoto
kubwa inayowakumba timu yao ni ukosefu wa vifaa na maandalizi kwani wana ukosefu mkubwa wa vifaa na mazingira ya kufanyia
mazoezi.
Aidha
amesema kuwa, hali hiyo inawafanya kuwa kidogo katika mashindani na kuwakatisha tamaa ya kushiriki mashindano
mengi ya kimataifa,”Kiukweli hatuna viwanja maalumu vya kufanyia mazoezi na
hali hii inatuathiri na kutukatisha tamaa” amesema Amina.
Nae, Kocha wa mpira wa miguu Bi Nasra Juma amesema ni kweli mpira wa wanawake una changamoto ukilinganisha na wanaume.
Amesema kuwa, ni vyema Serikali na mashirika mengine yakajitokeza katika kudhamini mpira wa wanawake ili kusaidia kukuza vipaji vya wachezaji wakike.
"Ni vyema mashirika binafsi yakajitokeza kudhamini ligi za wanawake ili kuinua soka lao, nao kujiajiri kupitia sekta hiyo" amesema Bi Nasra.
Mkurugenzi
wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania -TAMWA ZNZ , Dk Mzuri Issa
ni mdau mkubwa wa sekta ya michezo kwa maendeleo, wakati wa maadhimisho ya siku
ya mtoto wa Afrika, mwaka 2024 alisema ni vyema Watoto wakike kushiriki katika
michezo mbali mbali licha ya changamoto
zinazowakabili.
Amesema kuwa, changamoto za wanawake katika michezo ni nyingi na zinahitaji juhudi za Pamoja kutoka katika jamii, Serikali na mashirika ya michezo ili kutatuliwa.
“ Ni vyema kila mmoja achukuwe jitihada za kukabiliana na changamoto hizi ili kukuza usawa wa kijinsia katika michezo” ameshauri Dr Mzuri.
HijaMohamed ni mshauri elekezi katika mambo ya kijinsia katika mradi wa michezo kwa Maendeleo unaofadhiliwa na Serikali ya Ujerumani nchini Tanzania ( GIZ) amesema wana malengo ya kujenga viwanja saba vya mpira Unguja na Pemba, ili kuondoa changamoto ya Watoto wa kike kushiriki michezo.
Amesema
kuwa, viwanja hivyo vinne
vitajengwa Unguja na vitatu vitajengwa
Pemba ili kuimarisha sekta ya michezo
kwa maendeleo na vijana wengi
kuitumia fursa zinazotokana na michezo kujiajiri.
Nae, Katibu
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar
( ZFF) Hussein Ahmada Vuai amesema sekta
ya mpira wa miguu imekuwa na kuimarika kwa kujengwa viwanja vya kisasa ili
wachezaji wawe huru kufanya mazoezi na kushiriki michezo.
Amesema
kuwa, ni vyema Watoto wakike kuzitumia fursa za michezo kushiriki katika
michezo mbali mbali ya ndani na nje ya nchi kwani licha ya changamoto
zinazowakabili lakini pia wana fursa nyingi ambazo zinawanufaisha kupitia
michezo.

Post a Comment