WAANDISHI VITUMIENI VYOMBO VYA HABARI KUTATUA MATATIZO YANAYOIKUMBA JAMII-TAMWA ZNZ
NA MARYAM NASSOR
CHAMA cha Waandishi
wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar- TAMWA ZNZ kimesema wakati
umefika kwa wandishi wa Habari nchini kujikita
katika kuandika Habari za mabadiliko
ya tabianchi kwani janga hilo linaikumba
dunia kwa sasa.
Akizungumza
katika madhimisho ya siku ya Redio Duniani huko katika ofisi kuu za TAMWA ZNZ, Tunguu Unguja Mkurugenzi wa Chama hicho, Dkt Mzuri
Issa , amesema ni vyema wandishi wakaandika zaidi Habari za mabadiliko ya
tabianchi yanayoikumba dunia,ili jamii ipate uelewa wa kukabiliana nayo.
Amesema
kuwa, Dunia imekumbwa na majanga ya mabadiliko ya tabianchi na Zanzibar ni
sehemu ya dunia nayo imekumbwa na
madhara ya mabadiliko hayo .
Aidha amesema kuwa, wakati dunia ikiadhimisha siku ya redio duniani ni vyema chombo hicho kikatumika zaidi katika kuhamasisha na kuelimisha jamii juu ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi na kuhamasisha wanawake kugombea nafasi za uongozi kwani mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi.
Nae,
mwandishi mkongwe visiwani Zanzibar na mjumbe wa bodi ya TAMWA ZNZ, Bi Hawra
Shamte amesema siku ya redio duniani kwa umuhimu wake
ilitangazwa na UNESCO na ikathibitishwa na Umoja wa Mataifa hivyo ni muhimu
wandishi kuendelea kuitumia siku hiyo kwa kuelimisha jamii juu ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi.
Amesema
kuwa, bado waandishi wa Habari hawajaitumia redio na vyombo vyengine vya
Habari ipasavyo katika kuhamasisha wanawake kugombea nafasi za uongozi na kufanya uchechemuzi wa sheria rafiki ya Habari
ili ipatikane karibuni.
Aidha
amesema kuwa, ipo haja kwa wandishi wa
Habari nchini kuendelea kuandika na kufanya uchechemuzi wa sheria za Habari ,
kwani sheria inayotumika kwa sasa ni ya
muda mrefu na imepitwa na wakati.
“Tuendelee kufanya uchechemuzi kwa kuandika Habari na Makala za kuhamasisha sheria rafiki za Habari na madhara ya mabadiiko ya tabianchi kwani jamii bado haina uwelewa wa kutosha wa mambo hayo “ amesema bi Hawra.
Nae,
mwandishi wa Habari mkongwe kutoka gazeti la
Mwanahalisi Zanzibar Jabir Idrissa amesema ,katika tasnia ya Habari kunahitajika
mapinduzi makubwa kufanyika ili jamii iendelee kuviamini vyombo hivyo, kwani
vingi vyao vimejikita katika kutangaza muziki na mpira na kuacha kutatua
matatizo yanayoikumba jamii na kuyapatia ufumbuzi.
“Vyombo vingi
vya Habari vimejikita kutangaza mipira na muziki , wandishi wameacha
kuandika matatizo yanayoikumba jamii na kuyatafutia ufumbuzi, hivyo
jamii imeacha kuvisikiliza vyombo hivyo” amesema Jabiri.
Amesema
kuwa, dunia ikiadhimisha siku ya Redio
ni muhimu wandishi kujitathimini jee chombo hicho na vyombo vyengine vya habari vinatumika ipasavyo kuisaidia jamii
kutatua matatizo yake na kuhamasisha wanawake kugombea nafasi za uongozi.
Mwandishi wa Habari kutoka Redio ya Zenji FM Berema Suleiman amewasihi wandishi wa habari kuwa makini zaidi katika kazi zao, kwani kipindi kinachoelekea ni uchaguzi , usalama wao ni muhimu mno wakati wakitimiza majukumu yao kwani tafiti zinaonesha misuko suko mingi huwakuta wandishi wakati huo.
Siku ya
Kimataifa ya redio huadhimishwa Febuary
13 kila mwaka tangu
ilipotangazwa rasmi na UNESCO
mwaka 2011 na kupitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2013, kwa lengo la kutambua mchango wa
redio katika kufikisha taarifa kwa jamii na kauli mbiu ya mwaka huu ni “ Redio
na Mabadiliko ya Tabianchi”.



Post a Comment