ZACCA YAPANDA MIKOKO 386,000 UNGUJA NA PEMBA KUPUNGUZA ATHARI ZA MABADILIKOYA TABIANCHI
NA MARYAM
NASSOR
MKURUGENZI
wa Taasisi ya kukabiliana na Mabadiliko
ya Tabianchi Zanzibar (ZACCA) amesema tayari wamepanda miti milioni tatu,laki nane
na elfu sita ( 386,000) za mikoko Unguja
na Pemba kwa lengo la kupunguza athari
za mabadiliko ya tabianchi visiwani Zanzibar.
Akizungumza
katika mafunzo ya kukabiliana na
mabadiliko ya tabianchi kwa wandishi wa Habari, huko katika ofisi ya taasisi
hiyo Tunguu Unguja Mkurugenzi
Mahafoudh Haji amesema ni vyema jamii ikashirikiana na taasisi hiyo
kupanda mikoko ili kupunguza athari zinazotokana
na mabadiliko ya tabianchi.
Amesema kuwa, wamekuwa wakipanda miti ya
mikoko sehemu zilizoathirika zaidi na
mabadiliko ya Tabianchi tokea mwaka 2014
walipopata usajili rasmi wa taasisi yao, ili kupunguza athari zaidi na kuweza
kukabiliana na madhara makubwa yatokanayo na
mabadiliko ya tabianchi.
“ Taasisi
yetu tunafanya utafifi wa kujua vipi mabadiliko ya tabianchi yanaathiri visiwa
vyetu hivi, na kuchukua hatua yakukabiliana nayo kwa kupanda mikoko sehemu zilizoathirika
zaidi Unguja na Pemba” amesema Mahfoudh.
Aidha amesema kuwa, lengo kuu la kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni kujenga
uhimilivu wa mabadiliko ya tabianchi na kutoa uelewa kwa jamii kuhusu mabadilko hayo na njia za kukabiliana nayo.
Nae,Afisa
Mazingira kutoka ZACCA Maryam Abrahman Juma amesema ni vigumu kuzuia mabadiliko
ya tabianchi yasitokee lakini wanaweza kupunguza madhara yake kwa kupanda
mikoko na kutumia njia mbali mbali ikiwemo kutoa elimu kwa jamii ili kusaidia
kupunguza athari hizo.
Amesema
kuwa, ni vyema kushirikiana kwa Pamoja ili kupunguza na kukabiliana na athari
za mabadiliko hayo kwani yako kila
pahali na dunia bado haijapata suluhu ya mabadiliko hayo.
“ Jamii tuwe mstari wa mbele kukabiliana
na mabadiliko ya hali ya hewa kwani kila
kukicha tunashuhudia joto kali linaongezeka” amesema Maryam.
Hishamu Mohamed ni Afisa uhamasishaji jamii kutoka ZACCA amesema kuwa, miti ya mikoko husaidia kuwepo kwa bayoanuai na kuwa ni makaazi muhimu ya kuzalisha Samaki.
Aidha
amesema kuwa mikoko inauwezo wakukabiliana na mafuriko , tsunami , mwawimbi
makubwa ya Bahari na kuzuia mmomonyoko wa udongo.
“ Miti ya
mikoko ni muhimu sana kwani, mchanga
wake humeza gesi ya ukaa na hewa ukaa, na ina uwezo wa kukabiliana na kiwango
kikubwa cha kaboni “ amesema Hishami.
Nao baadhi ya wandishi waliopatiwa mafunzo hayo ya siku moja Malik Shahran na Huwaida Nassor walisema, mafunzo hayo yamewasaidia kupata uwelewa wa mambo mengi kuhusu madhara ya mabadiliko ya tabianchi na njia za kukabiliana nayo.
Mafunzo hayo ya siku moja yamewashirikisha wandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali, yameandaliwa na ZACCA kwa kushirikiana na TAMWA ZNZ kwa lengo la kuwajengea uwezo wandishi kuhusu mabadiliko ya tabianchi.

Post a Comment