WATOTO WA KIKE ITUMIENI MICHEZO KAMA NJIA YA KUJILINDA- TAMWA ZNZ.


NA  MARYAM NASSOR

WATOTO wa kike na wasichana wametakiwa kuitumia michezo kama njia moja wapo ya kujikinga na kujilinda na vitendo vya Ukatili na Udhalilishaji wa kijinsia.

 Wito huo, umetolewa na Afisa wa mradi wa michezo kwa maendeleo kutoka chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar, ( TAMWA ZNZ) Hairat Haji huko katika ukumbi wa Bima mipirani Unguja, katika madhimisho ya siku 16 za kupinga  udhalilishaji.

Akisoma ripoti ya majumuisho ya  vitendo vya ukatili wa kijinsia kutoka January  hadi oktoba mwaka huu 2024, alisema zinaonesha hali ya kutisha,  kwa kuongeza kwa vitendo hivyo  kati ya kesi 1,582 za ukatili wa kijinsia ziliripotiwa  na waathirika watoto walikuwa 1,337 kati ya hao, wasichana walikuwa ni 1,095 na wavulana 242.

Aidha Afisa huyo, alisema kuwa  kesi 693 zilihusisha watoto wa  umri kati ya miaka 15 hadi 16 huku akitanabahisha kuwa, vitendo hivyo hufanyika  kati ya saa 9:00 jioni  na saa tatu usiku. Wakati muda huo watoto wengi wapo mazingira ya nyumbani ambapo kuna usalama.

Aidha alisema kuwa, kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘’kuelekea 2030: Tuungane kutafakari na kuchukua hatua kumaliza Udhalilishaji dhidi ya wanawake Zanzibar’’ ikiwa ni miaka 6 kutoka sasa, hivyo ipo haja ya kuunganisha nguvu ili kumaliza vitendo hiv


Nae, Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo, Mwatima Issa Rashid amesema  kuwa, katika siku hizo 16 za kupinga udhalilishaji,wad  kwa kushirikiana na Serikali kuendelea kuzitumia  katika kupinga vitendo hivyo, kwani vinaonekana bado vinaongezeka.



Amesema kuwa,siku hizo, zitumike katika kujenga jamii iliyo bora, ambayo haijihusishi na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto.

Aidha,amesema kuwa, ripoti iliyotolewa na Afisa  Hairat kutoka Tamwa, inaonesha ipo haja ya kushirikiana kwa pamoja wadau na Serikali katika kupinga vitendo hivyo vya udhalilishaji kwani hali bado inatisha.

Nae,  naibu kamisheni ya uhamiaji na Kocha wa mpira wa miguu, Nasra Juma Mohamed amesema, michezo inasaidia  watoto kujiepusha na vitendo vya udhalilishaji duniani, kote takwimu zinaonesha hivyo.

Amesema kuwa,kila kwenye watoto watatu basi mmoja kakumbwa na vitendo vya udhalilishaji, hivyo ipo haja kuitumia michezo kama njia ya kujikinga na vitendo hivyo.

Jesse Mikofu, ni mwandishi wa habari mkongwe katika tasnia ya habari, alishauri kuwa wazazi kuvuja ukimnya kwa watoto wao,  kwani watoto wanahitaji sehemu salama ya kueleza madhila wanayopitia , kwani kimnya  kinazidi kuwawatesa na kuendelea kuwafanya wathirika wa vitendo hivyo.

Madhimisho hayo, ya siku 16 za kupinga vitendo vya  udhalilishaji  yameandaliwa na TAMWA ZNZ, na kuwashirikisha wandishi wa habari na wadau mbali mbali ili kutafakari na kutafuta ufumbuzi, yakiwa na kauli mbiu ‘’ KUELEKEA 2030: TUUNGANE KUTAFAKARI NA KUCHUKUA HATUA KUMALIZA UDHALILISHAJI DHIDI YA WANAWAKE ZANZIBAR.

                                      Mwisho


No comments

Powered by Blogger.