WAZIRI PEMBE ATAKA USAWA WA KIJINSIA MICHEZONI
NA MARYAM NASSOR,
WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Riziki Pembe Juma, amesema Usawa wa kijinsia ni lazima uzingatiwe Kila sehemu, ili kujenga Jamii yenye Usawa.
Ameyasema hayo, huko katika uwanja wa Mau,katika hafla ya uzinduzi wa Mpango Mkakati Jumuishi wa Jinsia katika Michezo Zanzibar, wa mwaka 2024/25-2028/29.
Waziri Pembe, amesema kuwa Mpango huo mkakati, umekuja kusaidia Utekelezaji wa sera ya Michezo, ya mwaka 2018 na kuuondoa vizuizi vya kiutamaduni na kidini, vilivyopo.
"Kwenye huu Mpango Mkakati umezingatia, Usawa wa kijinsia, na kuondoa, vizuizi vya kiutamaduni na dini, ambavyo vipo"amesema Waziri Pembe .
Aidha, amesema kuwa Mpango huo, umezingatia kukuza Usawa wa kijinsia na ujumuishi kupitia michezo Kwa wote, hususani Kwa Makundi maalumu ya watu wenye ulemavu.
Amesema kuwa, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inataka Usawa wa kijinsia, Kila sehemu hata kwenye Michezo, kutokana na hapo awali ulikuwa haupo.
Mwakilishi kutoka Chama cha Wanasheria Wanawake Zanzibar, (ZAFELA) ambao walioshiriki katika kuandaa Muongozo huo, Jamila Mahmoud, amesema ni vyema,ukapelekwa Kila sehemu ili walengwa wapate kusoma na kuuelewa ili kupata kujilinda.
Amesema kuwa, Muongozo huo wa kumlinda Mtoto wa kike, na watu wenye ulemavu, utasaidia kuweka mazingira salama michezoni na Kila mtu kushiriki michezo.
Nae, Afisa Mdhamini Wizara ya Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Pemba, Mfamau Lali Mfamau ,Kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara Hiyo, amesema Mpango Mkakati huo, utatoa ulinzi Kwa watu wote, hususani watu wenye Ulemavu, na kuifanya Michezo kuwa,sehemu salama Kwa Kila mtu kushiriki.
Aidha, ametoa wito Kwa Jamii na Wana michezo Kwa ujumla, kuusoma muongozo huo na kuuelewa.
Hija Mohamed Ramadhan, ni mshauri Jinsia kutoka Taasisi ya Ujerumani (GIZ) amesema kupitia mradi wa michezo Kwa maendeleo, watahakikisha , michezo hiyo inakuwa sehemu salama,na kuhamasisha Usawa wa kijinsia.
Amesema kuwa, kupitia Mpango Mkakati Jumuishi wa Jinsia katika Michezo, utasaidia kutekeleza sera ya Michezo ya Zanzibar ya mwaka 2018 ya Michezo Kwa wote.
Nao, baadhi ya wanamichezo wa Timu ya Kabadi ya Km km, Hajra Shauri na Faidha Ramadhan, walisema Mpango Mkakati huo, ni Mzuri na kutoa wito Kwa wanamichezo wengine kuripoti vitendo vya Udhalilishaji vinavyotokea michezoni, ili wafanyaji wachukuliwe hatua.
Walisema kuwa, Mpango Mkakati huo, ni vyema ukawafikia walengwa, kwani wao ndio wathirika wakubwa wa vitendo vya Udhalilishaji Michezoni, na hawana elimu ya kuviripoti.
Mpango Mkakati Jumuishi wa Jinsia katika Michezo, Zanzibar wa mwaka 2024/25- 2028/29.umeandaliwa Kwa kushirikiana na wadau mbali mbali, wakiwemo Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Asasi za kiraia, Mashirikisho ya Michezo na Jamii Kwa ujumla.


Post a Comment