HARAKATI ZA WANAWAKE KATIKA UONGOZI,NA VIKWAZO WANAVYOKUMBANA NAVYO
NA MARYAM NASSOR,
SITI Ali Makame 47,
diwani wa wadi ya Banda kuu Nungwi, wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja,
simulinzi yake na harakati za kutafuta uongozi,
inaonesha historia ya kipekee katika safari za wanawake wengi waliokuwa na
ndoto za kugombania nafasi mbali mbali za uongozi visiwani Zanzibar.
Siti, ambae alianza harakati za siasa mwaka 2020 akiwa mwanachama hai wa chama cha
Mapinduzi-CCM ambaye aligombea nafasi ya udiwani mara mbili mwaka 2020 na mwaka
2015 ndipo aliposhinda na kuwa diwani.” Sikukata tamaa, niligombea mara mbili nafasi ya
udiwani, na mwaka ule (2015)
bahati ilikuwa upande wangu nilifanikiwa
kuupata udiwani” amesema Siti.
Akiendelea
kusimulia , amesema baada ya kupitishwa
na chama chake, cha CCM kugombea hakuamini” Baada ya tu kutangazwa basi wanawake wenzangu walinifuatwa na kuniambia
nisigombee, maana hiyo nafasi ni ya
mwanamme” amesema maneno hayo yaliniumiza
na kunikatisha tamaa hasa kwa vile
yametoka kwa wanawake wenzangu ambao wao walipaswa kuniunga mkono.
Sheria ya
vyama vya siasa nchini Tanzania , sheria
no.5 ya mwaka 1992, sura ya 258 inatoa sharti kwa vyama vya siasa nchini kuhakikisha usawa wa
kijinsia katika kuandaa na kutekeleza sera zake.
Pamoja na
masharti hayo, utafiti uliyofanywa mwaka 2013 ,uliyofanywa na wadau kutoka vyama 16 vya Siasa nchini Tanzania, Pamoja
na wanasheria umebaini kuwa bado kuna changamoto ya utekelezaji wa sheria
hiyo,kutokana na baadhi ya vyama vya siasa, kutokuweka mazingira wezeshi kwa
wagombea wanawake.
Baraza la
Manispa wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja kuna wana wapiga kura 157,369 kati ya hao wanawake
ni 80,205 na wanaume ni 77,164. Licha ya kuonekana kuwa na idadi kubwa ya
wanawake katika baraza hilo, lakini wanaongoza kwa wingi wa kupigiwa kura ni wanaume wakiwa ni 12 na
wanawake ni saba tu.
“ Licha ya
kuwa wanawake ni wengi katika kupiga kura, lakini wanaoongoza kupigiwa kura
nyingi katika majimbo na wadi ni wanaume, hii ni kwasababu bado dhana ya
wanajamii kuwa wanawake hawawezi ipo vichwani mwao” amesema Siti akimalizia.
Makala hii,
ilimtafuta diwani wa wadi ya Mahonda wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja, Pili
Mohamed Said ambaye amekuwa kwenye nafasi hiyo ya udiwani tokea mwaka 2020 ,amesema nchi
nyingi zinazoendelea duniani, zinaonesha
ushiriki wa wanawake katika siasa na hiyo ni kwa sababu ya nguvu ya
wanawake katika uongozi, husaidia
kuimarisha kwa huduma za kijamii.
“Tupewe
fursa sawa katika nyanja za maamuzi ili tuweze kuzisaidia jamii
na kuleta mabadiliko ni dhana ya wazi, kwamba mwanamke ni kiongozi anaweza kulea na
kusaidia upatikanaji wa maendeleo” amesema
Pili ambae alipata nafasi ya kuwa diwani mwaka 2020.
Akionekana
na nguvu ya kuleta mabadiliko Siti ,
anapitia changamoto ya kuwepo mfumo dume unaendelea kumtafuna katika wadi yake, kwa kuona kuwa kuna baadhi
ya madiwani wanaume kuja kwenye wadi
yake na kumuingilia katika majukumu yake ya kiutendaji’’ kuna madiwani wanaume wanatoka sehemu zao, wanakuja kufanya
kazi katika wadi yangu bila ya taarifa, na nikipeleka malalamiko kwa wakubwa hayapewi uzito, labda
kwa sababu naonekana ni mwanamke na naumia kuhusu hili” amesema Siti.
Mstahiki
Meya Baraza la Manispaa ya Wilaya ya Kaskazini
‘A’ Unguja, Machano Fadhil Machano, amesema katika baraza lake la Madiwani hakuna utaratibu wa kuingilliana katika majukumu, kwani huo si
utaratibu wao, ‘’Sikumbuki kupokea barua
rasmi ya malalamiko, kutoka kwa diwani kuwa
kaingiliwa katika majukumu yake , lakini nimeshawahi kuyasikia
malalamiko kama hayo, chini chini” ameongeza kwa kusema
kuwa ikiwa mtu anaona anaingiliwa katika majukumu yake
basi huyo, hafanyi majukumu yake’’ amemaliza kwa kusema hivyo
Machano.
Zanzibar
imesaini mikataba kadhaa ya kikandaa na kimataifa kama mkataba wa Beijing, lengo la mkataba huo ni kuhakikisha uwiano sawa katika nafasi za uongozi, lakini
utekelezaji wa mikataba hiyo bado inasuasua.
Halima
Ibrahimu Mohamed kutoka chama cha Act
Wazalendo na Waziri wa Baraza kivuli,
akiwa kama Waziri kivuli upande wa Wizara ya Maendeleo ya Wanawake ,Watoto na Makundi maalum , amesema ushiriki wa
wanawake katika chama chake, ni mzuri,
wanayo mabaraza kivuli ambayo washiriki wake
Zaidi ya asilimia 52 , ni wanawake.’’ Tunahitaji mengi kufanyika ili tuendane na kasi ya Mabadiliko ya
Ulimwengu na kuwainua wanawake katika
nafasi za uongozi ili tuone mabadiliko
na kuisaidia jamii” amesema Halima.
Ripoti ya
sensa ya watu na makaazi ya Tanzania ya mwaka 2022, inaonesha kuwa Zanzibar ina wakaazi milioni 1.8 kati ya
hao wanaume ni 915,492 na wanawake ni
974,281.hii ina maana kwamba wanawake ni
asilimia 51.6 ya wakaazi wote wa Zanzibar, lakini wingi huo hauonekani katika
nafasi za uongozi.
Lucy John
Mtembo ni Mwenyekiti wa Umoja wa
Wanawake Tanzania , kupitia chama cha Mapinduzi -UWT, chama ambacho hujinasibu
kuwepo kwa usawa wa kijinsia wa viongozi wake
kwenye uwakilishi.” Sisi wanawake tuko wengi kuliko wanaume,lakini huu wingi wetu hauakisi bado katika uongozi na vyombo
vya maamuzi” amesema Lucy huku akiona
hali ya uoga na kujiamini ni miongoni mwa sababu zinazowarudisha nyuma.
“ Kwa miaka
mingi wanawake tumekuwa nyuma kimaendeleo, kwa sababu tulikuwa tunaogopa
kushika nafasi za uongozi na wanawake wengi walikuwa hawana elimu ya uongozi,
lakini sasa tumejidhatiti kugombea na tunataka 50 kwa 50” Amemaliza Lucy huku
akionesha msisitizo.
Dk Mzuri Issa
ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha
Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar -TAMWA -ZNZ ambao kwa
kushirikiana na Taasisi ya Kidemokrasia -NDI, walifanya utafiti juu ya kujua hali ya wanawake
viongozi kwenye vyama vya siasa,” Ushiriki hai wa wanawake katika siasa mara nyingi husababisha kuimarika
kwa hali ya kijamii na kiuchumi, kwani wanawake wana uwezo wa kukabiliana na kupunguza umasikini
ukilinganisha na wenzao wanaume”Amemaliza
Dk Mzuri akiwa Ofisini kwake Tunguu
Zanzibar.
Thabiti Idarus
Faina ni Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi
Zanzibar -ZEC amesema Tume ya Uchaguzi ina sera jumuishi ya jinsia,
ambayo lengo lake kubwa ni kuhamasisha ushiriki
wa jinsia zote, kushiriki katika kugombea nafasi za uongozi, “Sisi
tunasimamia suala hili la jinsia , ambapo tunavishauri vyama vyote vya siasa nchini, vifuate usawa wa kijinsia
katika kuteuwa viongozi wake” Akizungumzia suala la kuwarudisha nyuma au kutokuwapa nafasi Idarus amesema “ Ni vyema sana
viongozi wa siasa kujua umuhimu wa sera
na kutoa nafasi kwa wanawake na
iwapo wanawake wataona hawatendewi haki basi watoe taarifa na sisi tutatoa msaada”
amesema Faina.

Post a Comment