WANDISHI WA HABARI NCHINI, WASHAURIWA KUJALI USALAMA WAO KWANZA
NA MARYAM
NASSOR,
WAANDISHI
wa habari nchini, wametakiwa kuangalia usalama wao kwanza, kuliko kitu chengine
wakati wakitimiza majukumu yao ya kila siku.
Wito, huo
umetolewa na ndugu Suleiman Omar Seif wakati akichangia mada katika
kikao cha kukusanya maoni ya Wandishi wa Habari wa Zanzibar, juu ya mradi wa
Uwajibikaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) huko katika ukumbi wa Kidongo
chekundu Unguja.
Amesema
kuwa, hakuna kitu kizuri na chenye thamani kwa mwandishi kama kujali usalama wake, kwanza kwani kuna
wandishi ambao wameshawahi kufikwa na masahibu mbali mbali wakiwa kazini, hivyo
ni vizuri kuchukuwa tahadhari hiyo.
“ Hakuna kitu kizuri kwa mwandishi kama kujali usalama wake,kwanza na ukitokezewa na chochote basi , waarifu wenzako ili wajuwe jinsi ya kukulinda “ alishauri.
Nae,
Mtaalamu elekezi wa mradi wa Uwajibikaji
kutoka MCT, Kajubi Kajanga , amewataka wandishi wa Zanzibar kutoa maoni yao
kuhusiana na mradi huo, kwani unategemea kuanza mapema mwakani hapa Zanzibar kuliko sehemu,nyengine za
Tanzania bara.
Aidha,
amesema kuwa, ni vyema Zanzibar ikawa na sheria ya haki ya kupata Habari , ili uwe rahisi kwa wandishi
kupata Habari kwa urahisi bila ya pingamizi zozote kutoka kwa mamlaka husika.
Aidha ameshauri kuwa, nini kifanyike katika kuondoa umasikini katika vyombo vya Habari nchini hususani vya Zanzibar ambavyo, vinategemea matangazo ili vijiendeshe .
Nae,
mwandishi mkongwe na mjumbe wa ZAMECO,
Salim saidi amesema kuwa, ni miongo
miwili sasa tokea waanze kudai sheria rafiki ya Habari, bila ya mafanikio.
Amesema
kuwa,mbona sheria nyengine zinachukuwa
miezi sita au mwaka kurekebishwa kama sheria ya uchaguzi na sheria ya huduma za
posho kwa wawakilishi,ugumu wa sheria za
Habari kurekebishwa uko wapi.
“ Ni miongo
miwili sasa, tunadai sheria rafiki ya Habari bila ya mafanikio, lakini
tunashuhudia sheria nyengine zinachukuwa miezi sita au mwaka, kurekebishwa
ugumu uko wapi kwenye sheria hii” amehoji Mr Salim.
Nae,
mwandishi wa Habari wa DW Zanzibar, Salma Said akichangia mada katika kikao
hicho,alisema usalama wa waandishi bado ni mdogo, wandishi wana hofu kutokana
na kuwa hakujapatikana sheria rafiki ya
Habari ambayo itawalinda hasa kipindi cha uchaguzi mkuu mwakani 2025.
Kikao hicho,
cha siku moja cha kujadili na kutoa maoni ya mradi wa Uwajibikaji , ambao ni wa miaka sita na unatarajiwa kuanza mapema mwakani, umewashirikisha wandishi wa Habari kutoka vyombo mbali mbali nchini na
wadau wa habari.
Post a Comment