DR. Mzuri awataka wandishi kuripoti habari za mabadiliko ya tabianchi na kuonesha nafasi ya mwanamke katika mabadiliko hayo.
NA MARYAM NASSOR,
CHAMA Cha wandishi wa habari wanawake Tanzania, Zanzibar(TAMWA ZNZ) kimesema wakati umefika Kwa wandishi wa habari kuripoti, habari za mabadiliko ya tabianchi, na kuonesha nafasi ya mwanamke katika kukabiliana na mabadiliko hayo.
Ameyasema hayo, mkurugenzi wa chama hicho, Dk Mzuri Issa, alipokuwa akifungua mafunzo Kwa wandishi wa habari kuhusu mabadiliko ya tabianchi.
Dk Mzuri, amesema kuwa wanawake ndio viongozi katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, lakini kazi zao hazitangazwi, hivyo watu wengine hawajui wanafanya nini katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
"Kuna wanawake wanafanya mambo makubwa, katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, lakini hawatangazwi kupitia vyombo vya habari" amesema.
Nae, mkufunzi katika mafunzo hayo, Ali Nassor Sultan amewataka wandishi wa Habari, kufanya utafiti zaidi ili kubaini ukubwa wa tatizo.
"Wandishi wa habari ni lazima muende mbali zaidi ili kubaini ukubwa wa tatizo " amesema.
Afisa habari katika mradi huo, Sophia Ngalapi amesema kuwa lengo la mafunzo hayo, ni kuhamasisha wanawake kuwa viongozi katika kukabiliana na tabianchi.
Amesema kuwa, wandishi wanatakiwa kuonesha nafasi ya mwanamke katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi na wanavyo kabiliana nayo.
" Wandishi munatakiwa kuonesha nafasi ya mwanamke katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi "amesema.
Nao, wandishi wa habari walioshiriki katika mafunzo hayo, Berema Nassor na Zurima Maulid ,walisema ipo haja Kwa wandishi wa habari kufanya kazi ya kuelimisha jamii kuhusiana na mabadiliko ya tabianchi kwani bado jamii haina uelewa kuhusu madhara ya mabadiliko ya tabianchi.
Jumla ya wandishi wa habari 30, kutoka Unguja na Pemba wamepatiwa mafunzo, ya siku mbili yanayolenga kuonesha nafasi ya mwanamke katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, kilimo Cha miti mseto ( Agroforestry) na kuhifadhi mazingira Kwa kutumia mikoko, mafunzo hayo yametolewa na chama Cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar, wakishirikiana na Taasisi ya kutunza mazingira ya Pemba,(CFP).


Post a Comment