TAMWA ZNZ, YAWATAKA WANDISHI WA HABARI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITAL KUHIFADHI KAZI ZAO.

 


NA MARYAM NASSOR

Chama cha wandishi  wa  habari wanawake  Tanzania Zanzibar, ( TAMWA ZNZ)  kimewataka  wandishi wa habari  nchini , kubadilika na kutumia mifumo wa kidigitali  kuhifadhi kazi zao ili ziishi kwa muda mrefu na zikiwa na ubora.

Akiutambulisha  mfumo wa Air table,katika kikao cha  wandishi wa habari na wadau   huko,katika Ofisi za Tamwa Tunguu Unguja, Afisa wa tathmini na ufuatiliaji  wa chama hicho, Mohamed Hatibu Mohamed , amesema kuwa ipo haja kwa wandishi wa habari kuhifadhi kazi zao katika mifumo hiyo.

 

Amesema kuwa, mfumo huo ni mzuri kwa wandishi  wa habari,kuutumia kwa ajili ya kuhifadhi taarifa zao, kwani ni rahisi kuutumia na salama kwa kuhifazia taarifa zao.

‘’ Mfumo huu wa Air table, ni mzuri na rahisi kwa matumizi yenu  ya kuhifadhi taarifa zenu ikiwemo story na Makala kwani zitadumu kwa muda mrefu zikiwa na ubora ule ule ‘’ amesema Mohamed.


Nae, Afisa habari wa mradi huo, kutoka Tamwa ZNZ, Nafda Hindi amesema miradi yote ya Tamwa , kuanzia sasa watatumia mfumo huo, hivyo aliwataka wandishi wa habari wanaofanya kazi nao, kuutumia mfumo huo.

‘’ Tamwa tumejipanga kuutumia mfumo wa Air table katika miradi yetu yote, kwani ni rahisi kuutumia lakini pia ni salama kuhifadhia taarifa zenu ‘’ amesema.

 Nao, baadhii ya wadau walioshiriki katika kikao hicho, Khamis Haroun kutoka tume ya ukimwi Zanzibar ( ZAC) amewapongeza  Tamwa kwa kutumia mfumo wa kidigitali  kwa kuhifadhia taarifa zao.

 ‘’ Huu mfumo ni mzuri na salama kuhifadhia taarifa  zetu hivyo, ni vyema kwa taasisi nyengine  ambazo hazijaanza kutumia mifumo  kama hiyo, kuanza kuutumia ili taarifa zao zibaki salama’’ amesema.

 Amesema kuwa,  ipo haja kwa Taasisi nyingine kutumia mifumo ya kidigitali katika kuhifadhia taarifa zao, kwani dunia sasa imekuwa kijiji kutokana na maendeleo makubwa ya kimtandao.

Nao, baadhi ya wandishi wa habari waliohudhuria kikao hicho, Berema Suleiman na Huwaida Nassor walisema wako tayari kuutumia mfumo huo, kwani kazi zao nyingi huwa zinapotea kutokana na kuhifadhi katika komputa na mara ikiharibika basi, wanapoteza kumbukumbu zao.

 

 

No comments

Powered by Blogger.