Mashindano ya ladies first kwa mara ya kwanza yamefanyika Zanzibar.

 

 


NA MARYAM NASSOR

KAMISHNA wa baraza la michezo Zanzibar,Mohamed Makame amesema mashindano ya 6 ya ladies First yamefana  kwa Zanzibar na  kuwashukuru shirika la maendeleo la Japan(JICA) kwa kuwakubalia ombi lao la kuja kuyafanya hapa Zanzibar.

Ameyasema hayo, huko katika Uwanja wa Amaan complex, alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari, mara baada ya kumaliza mashindano hayo.

Amesema, mashindano hayo  ya ladies first  lengo lake ni kuhamasisha wanawake kushiriki katika michezo, hususani katika michezo ya riadhaa.

“Mashindano haya ya ladies first ni mara ya sita kufanya kwa Tanzania bara, lakini kwa hapa kwetu Zanzibar ni mara ya kwanza, lakini tumefurahi yamefana sana’’ amesema.

Amesema kuwa,  wachezaji kutoka Zanzibar walikuwa wakishiriki Tanzania bara, na kupata ushindi ndipo walipowaomba JICA, kuja kuyafanya Zanzibar kutokana na kuboreshwa kwa mindombinu ya michezo na viwanja vya kisasa.

‘’Tukiangalia michezo mingi wanashiriki wanaume kuliko, wanawake hivyo, kuja kwa mashindano haya ya ladies first ni fursa kwa wanawake kushiriki katika matamasha kama haya’’ amesema.

Nae, balozi wa Japan nchini Tanzania Yasushi Misawa, amesema mashindano hayo ni fursa kwa wanawake kushiriki, na amewashukuru wadau wote walishiriki kwa pamoja kufanikisha jambo hilo.



Amesema kuwa, anaamini  nchi ya Tanzania inakuwa kwa kasi, kutokana na kuwa inatunza rasilimali watu, na amewataka vijana kutumia uwezo wao, katika kufanya kazi vizuri katika Sanaa na michezo, kwani ni lazima mwanamke ashirikishwe ili kuleta maendeleo.

 Nae, mshindi wa kurusha mkuki kutoka mkoa wa magharibi ,Tuma  Makame Ali amesema amefurahi kushiriki mashindano hayo na kushinda, na amewataka watoto wa kike kutumia fursa kama hizo zinapotokea kujitangaza na kukuza vipaji vyao.

Mashindano hayo, maalum kwa wanawake, yamefanyika kwa lengo la kuwahamasish watoto wa kike kushiriki  michezo,hasa katika riadhaa na yameshirikisha washiriki kutoka mikoa mitano ya Zanzibar, na mshindi katika shindano hilo ni kutoka mkoa wa Mjini magharibi Unguja.

 


No comments

Powered by Blogger.