MICHEZO NI FURSA KWA VIJANA KUJIAJIRI

 

NA MARYAM NASSOR

MICHEZO  hujenga Afya, huimarisha urafiki  ni pesa ni fursa za kiuchumi lakini ndio sekta inayoongoza ulimwenguni kutoa ajira kwa vijana.

Michezo ndio sekta inayoongoza Duniani kutoa mishahara mikubwa Zaidi kuliko sekta yoyote.

Kwa mujibu wa gazeti la kibiashara la nchini marekani forbes, limeorodhesha wanariadhaa kumi wanaolipwa pesa nyingi Zaidi duniani nafasi ya kwanza  akiishikilia Christiano Ronald.

Mchezaji mwenye asili ya kireno, akilipwa pound milioni175,000 kwa mwaka sawa na bilioni 493,000 za  kitanzania, sawa na  mshahara wa  milioni 41,000 kwa mwezi.

  Huku  mcheza gofu Jon Rahm akipanda hadi nafasi ya pili akilipwa dola milioni 218,000, wachezaji waliyodumu katika orodha hiyo ni Serena Wilium, Roger Fererer, Tom Brady ambao wamekusha  staafu.

 Huko ni barani Ulaya , turudi nyumbani Afrika bara lililosheheni kila aina ya vipaji’ waswahili wanasema mcheza kwao hutunzwa’tuwaangalie wachezaji walitajirika kupitia michezo, tumuangalie Sadio mane na Mohamed sallah wa nchini Misri, mchezaji kutoka Senegal Sadio Mane akilipwa bilioni  nane. kwa mwezi na Mo Sallah analipwa milioni 18.2 na wengine wengi .

 Kwa mujibu wa tarifa kutoka kwa  mrajisi wa vyama vya michezo  hapa Zanzibar kuna vyama  42 vya michezo vilivyosajiliwa.

 Akizungumza na mwandishi wa Makala haya, mrajisi Abubakar Mohamed Lunda amesema kwa sasa sekta ya michezo Zanzibar imekuwa na vijana wengi wanazitumia vizuri  fursa  za michezo kujiajiri.

Amesema kuwa, michezo ni sekta inayowainua vijana kiuchumi, kwani kuna michezo unatumia roundi  nne sawa na dakika 12 unalipwa milioni tatu au Zaidi, kama mchezo wa ngumi za kulipwa(Boxing) na hapa Zanzibar tayar zimekwisha ruhusiwa.

“ Vijana tumieni fursa za michezo kujiajiri kwani michezo ni mingi na yote yanasaidia kutoa ajira kwa vijana’’ alishauri.

Nae, kocha wa michezo kwa maendeleo Maryam Charles amesema  michezo ni fursa hasa kwa watoto wakike kwani, wachezaji wengi wanaocheza Zanzibar wengi wanatoka Tanzania bara kutokana na hapo awali watu walikuwa wanachukulia michezo kama uhuni.

Amesema kuwa, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewekeza kwenye michezo ili wananchi wanufaike na fursa zinazotokana na michezo, hivyo ni vyema wazazi wakawaacha watoto kujiendeleza katika michezo ili wajiajiri kwani michezo ni ajira kama ajira nyengine.

“Wazazi wasiuchukulie  mpira kama ni uhuni na kukatisha ndoto za watoto wao, kwani hapa Zanzibar tunao wachezaji kama Fei toto anacheza mpira na analipwa vizuri na kuendesha maisha yake’’ alisema.

 Aidha alisema kuwa, vipaji vipo katika kila michezo ni wakati sasa wazazi kuwasaidia watoto wao kuendeleza vipaji vyao na humo , kwenye michezo zinapatikana ajira kuliko zile za sekta ya umma au mashirika binafsi kwani mshahara wa wachezaji  ni mkubwa kuliko muajiriwa Serikalini.

‘’ Michezo ni fursa mimi mwenye  nimesafiri sehemu nyingi kwa ajili ya michezo, hapa juzi tu timu ya watoto chini ya umri wa miaka 15 ya wanawake imeenda Ufaransa,kwa kupitia mpira hizo ndio fursa za michezo ,” alisema.

Nae, mchezaji kutoka timu ya wanawake ya New Generation Hafidha Juma Ali amesema ni kweli michezo ni ajira na fursa ya kiuchumi lakini, Serikali  izidi kuwekeza katika michezo, kwani kwa ligi za wanawake bado kuna changamoto ya ufadhili.

Amesema kuwa, mpira wa wanawake umekuwa akimchukulia mfano  mchezaji kutoka bara Clara  Ruvanga analipwa hadi milioni 25 kwa mwezi ni mfano mzuri kuona soka linalipa.

Aidha aliiomba Serikali kama mdau nambari moja kuzidi kufanya uwekezaji ili na mpira wa Zanzibar ufike mbali na wachezaji wanufaike kupitia michezo.

“ Michezo ni fursa za ajira kwani wachezaji wanajiajiri kupitia soka lakini , Serikali izidi kufanya uwekezaji ili tufike mbali na sisi wachezaji kutoka Zanzibar ‘’ alishauri.

Nae, Makame Ameir  Mgeni kocha wa michezo kwa maendeleo, amesema  michezo ni pesa hasa katika michezo ya mtu mmoja mmoja kama ngumi za kulipwa,mpira wa wavu na riadhaa.

Amesema kuwa kwa hapa Zanzibar wapo wachezaji wanaojiajiri na kufanikiwa kupitia michezo hayo kama  mchezaji Dawa Haji, Asma Omar  na wengineo ambao wanaendesha maisha yao kupitia michezo.

 Katika mradi wa michezo kwa maendeleo unaotekelezwa na shirika la Ujerumani nchini Tanzania (GIZ)  umesema  mradi huo unalengo la kujenga viwanja saba vya mpira Unguja na Pemba,  vikiwemo viwanja vya tenis lengo likiwa ni kutekeleza usawa wa kijinsia katika michezo na kuinua sekta hiyo ili vijana wajiajiri kupitia michezo.

                            MWISHO

No comments

Powered by Blogger.