FURSA ZA KUJIAJIRI KUPITIA MICHEZO KWA WATU WENYE ULEMAVU BADO HAZIJAWAFIKIA
NA MARYAM NASSOR
KATIBA ya Zanzibar ya mwaka 1984
kifungu cha 12 (1) kimefafanua kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria na wanayo haki sawa bila ya ubaguzi wowote,
kulindwa na kupatiwa haki sawa.
Lakini licha
ya katiba kutamka wazi, lakini
ukiangalia suala la usawa kwenye michezo kwa watu wenye ulemavu bado hawajapewa nafasi kutokana na mitazamo
ya watu kuona hawana uwezo huo.
Mikataba
yakimataifa na kikanda ibara ya (30) imeridhia
kushirikishwa kwenye michezo kwa watu wenye ulemavu, kwani imeonekana
kuwa watu wenye ulemavu wanaachwa nyuma kushiriki katika michezo.
Akizungumza
na mwandishi wa Makala haya,afisini kwako mjini Unguja, mchezaji wa
timu ya watu wenye ualbino Abdillah Salum Shaame, amesema fursa za kujiajiri kupitia michezo bado hazijawafikia ipasavyo katika jumuiya zao.
Alisema
kuwa, licha ya katiba kuwapa uhuru wa kushiriki katika michezo lakini
hawashirikishi ipasavyo kama watu wengine waliyokuwa hawana ulemavu.
Aidha
alisema kuwa, bado kuna watu hawataki kuamini kuwa ukimshirikisha mtu mwenye
ulemavu basi, atashiriki na atashinda na
mifano ipo mingi.
‘’ Ni wakati wa jamii kuachana na itikadi potofu ambazo zimepitwa na wakati,na
badala yake watushirikishwe kwenye michezo kwani sasa michezo ni pesa na fursa
za ajira ‘’ alisema.
Hapa
aliiomba Serikali kama mdau nambari moja kuwajengea mazingira rafiki watu wenye
ulemavu nao watumie fursa za michezo kujiajiri kwani ajira ni ngumu kupatikana.
Nae, Hamad Ali mlemavu wa uziwi kutoka timu ya
special Olympic Zanzibar (SOZ) akizungumza kwa lugha ya alama na ishara kwa usaidizi wa mkalimani alisema kuwa
anapenda sana kushiriki michezo.
Amesema
kuwa, alishiriki mbio za olympiki nchini Ugiriki mwaka 2023 na kutokea mshindi
wa kwanza na kurudi na medali nchini hivyo angependa kujiajiri kupitia michezo.
“ Licha ya kupenda michezo,lakini hatushirikishi sana kwenye michezo kama watu wengine waliyokuwa hawana
ulemavu, watu huona sisi hatuna uwezo ‘’ alisema kwa masikitiko.
Aidha,
aliwataka wazazi kuwaruhusu watoto wenye ulemavu kujiunga katika jumuiya hizo
na wasiwafiche mayumbani, ili wafaidike na fursa za michezo.
Nae, Saada Hamad mwenyekiti wa timu ya special olympik ya Zanzibar, amesema timu za watu wenye ulemavu zinatengwa sana na wafadili ikilinganisha na timu za watu waliyokuwa hawana ulemavu.
Alisema
kuwa, timu zao hazina vifaa vya kufanyia mazoezi wala kiwanja maalum vya
mazoezi hivyo hupata wakati mgumu wakati wakijiandaa na mashindano ya
kimataifa.
“ Timu zetu
hazina bajeti kutoka Serikali wala hatuna viwanja vya kufanyia mazoezi wala
vifaa vya mazoezi, hivyo tunapata wakati
mgumu wakati wa kujiandaa na mashindano ya kimataifa’’, alisema.
Aidhaa
aiiomba Serikali na wadau wengine kuwasaidia katika ufadhili wa timu za watu
wenye ulemavu kwani, mara nyingi timu zao hukosa ufadhili.
Ahmed Khamis Iddi kapteni katika timu ya watu wenye
ulemavu wa mguu mmoja na mkono mmoja,
amesema kuwa wanapata msongo wa mawazo
kwa kukaa ndani bila ya kushiriki katika kitu chochote ikiwemo michezo.
Amesema
kuwa,hawana viwanja vya mazoezi kutokana na hali zao, wanafanya mazoezi katika
viwanja vilivyokuwa na miti na mchanga mwingi hivyo hupelekea kuumia misuli.
‘’ Tunakosa
Amani kwa kukaa ndani kujifungia lakini tukikutana katika michezo tunapata
matumaini na faraja na kujiona binadamu kama binadamu wengine na sisi tunatakakujiajiri kupita sekta ya michezo ‘’alisema.
Nae,Hassan
Haji Silima katibu katika timu ya watu
wenye ulemavu wa mguu mmoja na mkono mmoja, amesema kuwa wana changamoto
ya kiwanja cha kufanyia mazoezi na vifaa vya mazoezi hawana.
Hivyo, aliiomba Serikali kuwapa japo kile
kiwanja cha nje cha uwanja wa Amani kwa ajili ya kufanyia mazoezi ili nao wawe
na uhuru wa kukitumia.
Aidha anakiri kuwa, michezo ni muhimu hasa kwa
kuimarisha urafiki baina yao, na kutekeleza mkataba wa haki za watu wenye
ulemavu.
Kanuni na
sera ya michezo ya Zanzibar ya mwaka
2018, imetamka wazi nia njemaa ya Serikali
katika kuhakikisha uwepo wa
usawa wa jinsia katika michezo lakini bado hawajafikiwa ipasavyo kundi la
watu wenye ulemavu.
Sheria na.8
ya mwaka 2022 ya watu wenye ulemavu
kifungu cha 28 (1) kinasema watu wenye
ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za binaadamu sawa na watu wengine .
Lakini
katika kifungu cha 28 (f) kinaeleza kuwa
watu wenye ulemavu wanahaki ya kushiriki katika michezo na burudani kama watu
wengine waliyokuwa hawana ulemavu.
Hija Mohamed
Ramadhan mshauri katika maswala ya jinsia katika michezo katika mradi wa
michezo kwa maendeleo unaofadhiliwa na shirika la Ujerumani nchini Tanzania
(GIZ) umesema una lengo la kujenga viwanja saba vya michezo, vitatu Pemba na
vinne Unguja hivyo katika viwanja hivyo iwaangalie na watu wenye ulemavu.
MWISHO
Post a Comment