JAMII IMETAKIWA KUHAMASISHA USAWA WA KIJINSIA KATIKA ELIMU NA MICHEZO


NA MARYAM NASSOR

JAMII imetakiwa kutilia mkazo watoto katika kushiriki michezo mbali mbali ili  kukuza ujuzi wa stadi za maisha  katika kukabiliana na vikwazo  mbali mbali kama  ukatili na udhalilishaji wa kijinsia.

Hayo yameelezwana wadau katika kongamano la riadhaa la siku ya motto wa Afrika, kwa wanafunzi wa skuli mbali mbali  za Unguja yaliyoandaliwa na  chama cha wandiishi wa habari wanawake Zanzibar(TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana  na chama cha wanasheria wanawake Zanzibar (ZAFELA)  shirika la Ujerumani nchini Tanzania (GIZ)  na kituo cha majadilianao ya vijana (CYD) kwa lengo la kuhamasisha usawa wa jinsia katika michezo.

Akizungumza kuhusu juhudi za kuimarisha usawa wa kijinsia na kuhamasisha  michezo, Dk Mzuri Issa Ali Mkurugenzi wa TAMWA ZNZ, alisisitiza umuhimu wa kuwa mfano mzuri kwa  jamii ili iwe hamasa kwa watu wengine kuingia katika michezo.


 ‘’ Tuwe mifano mizuri ya kuigwa kwa kuwa na heshima katika jamii, kwasababu sisi tuna nafasi ya kupata mawaidha sehemu mbali mbali ya stadi za maisha , hivyo tuna kila sababu ya kuhamasisha michezo kwa wote’’ alisema.

Kwa upande wake Wanu Ali Makame , meneja  idara ya mitaala na vifaa kutoka wizara ya Elimu na mafunzo ya amali Zanzibar , alisema kuwa katika kutilia mkazo  umuhimu wa michezo kwa maendeleo , wizara imeweka somo maalum linaloelezea masuala ya michezo.

‘’ Tuna somo maalumu linaloelezea masuala ya michezo , tunaweza tukacheza na tukasoma kwa salama na Amani bila ya kuathiri mila  na tamaduni zenu’’ alisema.

Hija Ramadhan kutoka shirika la GIZ aliongeza kuwa jitihada za kutengeneza usawa wa kijinsia ni pamaoja na kuhakikisha wadau wanashirikiana kuwalinda watoto na wanawake dhidi ya ukatili.

Katika hafla hiyo, wanafunzi walipata fursa ya kushiriki mbio fupi na washindi kuzawadiwa zawadi mbali mbali ikiwemo medali ,madaftari na bahasha.

  Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Tamwa ZNZ, yamewaleta pamoja wadau mbali mbali ikiwemo wanafunzi kutoka skuli mbali mbali za Unguja, wanamichezo  walimu  na wadau wa maswala ya jinsia yakiambatana na kauli mbiu’’ WAKATI NI SASA ‘’ wekeza katika elimu na michezo kwa watoto wote ikiwa ni chombo muhimu ambapo michezo itatumika kama chombo cha kuleta maendeleo na usawa katika michezo.

                     MWISHO

No comments

Powered by Blogger.