USHIRIKISHWAJI KWENYE MICHEZO KWA WATU WENYE UALBINO BADO KITENDAWILI
NA MARYAM NASSOR
JUMUIYA ya watu wenye ualibino
Zanzibar imesema kutokushirikishwa ipasavyo kwenye michezo kunawanyima haki yao ya msingi ya kikatiba na fursa za ajira kupitia
michezo.
Walisema
kuwa, katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 12 (1) kimefafanua kuwa
watu wote ni sawa mbele ya sheria lakini licha ya katiba kutamka hivyo,bado
hawajapewa nafasi katika michezo.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi, Ofisini kwao mjini Unguja katibu wa Jumuiya hiyo Abdillah Salum Shaame, alisema
wamekuwa hawashirikishwi kwenye michezo kama watu wengine waliyokuwa
hawana ulemavu na kupelekea kukosa fursa za ajira kupitia michezo.
Alisema, licha ya katiba ya Zanzibar kusema kuwa, watu wote ni sawa, lakini ukiangalia suala la michezo kwa watu wenye ulemavu bado hawajapewa nafasi ipasavyo kutokana na mitazamo ya watu kuona hawana uwezo huo.
Alisema kuwa, sera ya michezo ya mwaka 2018 imetamka nia njema ya serikali katika fursa za michezo lakini bado hizo fursa wao hazijawafikia kutokana na kuwa bado hawana mindombinu rafiki inayowafanya washiriki michezo.
Alieleza kuwa ni wakati wa jamii
kubadilika na kuondokana na itikadi
potofu na badala yake kuwashirikisha , watu wenye ulemavu kwenye michezo ili kujipatia
kipato kupitia michezo.
Aidha alisema kuwa, watu wenye ulemavu
wanahaki ya kushiriki michezo kama watu
wengine, hivyo ni wajibu wataasisi na
wizara ya michezo kuwashirikisha ili
kukuza vipaji vyao.
“ Sisi watu
wenye ulemavu hatushirikishi ipasavyo kwenye michezo kutokana na ulemavu wetu,
lakini ni haki yetu na sisi kushirikishwa kwenye michezo “ alisema.
Nae mchezaji
katika timu ya watu wenye ulemavu wa
mguu mmoja na mkono mmoja Kassim Mohamed amesema kuwa, kutokana na ulemavu waliyokuwa
nao hawana kiwanja maalum cha kufanyia mazoezi na kupelekea kufanya mazoezi
mara tatu tu kwa wiki.
‘’ hatuna
kiwanja maalum cha kufanyia mazoezi na
kupelekea kufanya mazoezi mara chache sana kwa wiki” alisema.
Afisa
mdhamini Wizara ya habari, vijana na michezo
Pemba, Mfamau lali Mfamau hivi karibuni
alisema wizara hiyo, imo kwenye mkakati wa kuboresha mindombinu
ya michezo ikiwemo kujenga viwanja ili kuona watu wenye ulemavu
wanaingia kwenye michezo.
MWISHO
Post a Comment