UKOSEFU WA UFADHILI LIGI YA WANAWAKE BADO CHANGAMOTO
NA MARYAM
NASSOR
UKOSEFU wa ufadhili katika ligi za mipira ya wanawake imetajwa kuwa ndio chanzo cha timu nyingi kufa.
Akizungumza na mwandishi wa Habari hizi, huko katika uwanja wa mazoezi Saateni, Unguja
kocha wa timu ya warrious Haji Hamdu Nahoda.
Alisema ,
timu nyingi za mpira wa miguu za wanawake hazina ufadhili ukilinganisha na timu
za wanaume.
Alisema kuwa, kuna timu nyingi zimeshindwa kushiriki ligi kuu Zanzibar msimu huu, kutokana na ukosefu wa rasilimali fedha na nyengine kufa kabisa.
“ Kwa sasa ligi ya wanawake imesimama kutokana
na kuwa haina mfadhili, wachezaji wanajitowa vya kutosha hawana hata posho’’
alisema.
Alisema kuwa, wadau mbali mbali wajitokeze kuwasapoti kwasababu hamasa ni kubwa ukilinganisha na hapo awali kulikuwa hakuna timu za wanawake.
Aidha alisema kuwa, soka ni ajira kama ajira nyengine hivyo, lakini tatizo kuwa hakuna wafadhili wakuwashika mkono ili kuendeleza vipaji vya wachezaji hao.
Nao, baadhi ya wachezaji katika timu ya warrious, walisema kuwa wana ndoto za kufika mbali katika soka
ya kuichezea simba guens na nyenginezo .
Walisema
kuwa, lakini wanaiomba Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar kama mdau nambari
moja kuendelea kuwapigania wapate ufadhili
katika ligi za wanawake kutokana na kuwa wanacheza katika mazingira
magumu.
“ Sisi hapa
tunapenda kucheza mpira lakini ligi yetu bado ina changamoto kuwa kwa upande wa
ufadhili” walisema.
MWISHO
Post a Comment