TAMWA ZNZ, WAIKUMBUSHA SMZ KUHUSU SHERIA MPYA
NA MARYAM
NASSOR
WADAU wa habari nchini wameiomba
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,
kukamilisha mchakato wa
marekebisho ya sheria zilizotolewa maoni
na wadau ili kutoa mazingira rafiki kwa waandishi
kutekeleza majukumu yao bila vikwazo vyovyote.
Akizungumza katika kongamano la siku ya
habari, Mkurugenzi wa chama cha wandishi
wa habari wanawake Zanzibar (TAMWA ZNZ)
Dk Mzuri Issa Ali huko katika ukumbi wa kariakoo unguja.
Alisema ,
licha ya wadau mbali mbali kutoa na kuwasilisha mapendekezo
yao kuhusu mapungufu yaliyopo kwenye baadhi ya sheria za habari, lakini bado utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua na kupelekea
mazingira magumu ya utendaji kazi
wa vyombo vya habari.
Alisema kuwa
mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari umekuwa kwa miaka mingi lakini bado, sheria hizo ambazo nyengine ni za muda mrefu
zimekwama kurekebishwa.
“ Sisi wengine tangu tuko wandishi chipukizi tunazungumzia kupata sheria hizi , tokea mwaka 2008, ni muda mrefu hivyo, tunahitaji kusimamia jambo hili na hatimae tupate sheria rafiki kwa waandishi wa habari’’ alisema.
Aidha alisema
kuwa, wadau wa habari wamefanya mapitio ya sheria nane , ikiwemo ya usajili wa wakala wa habari ,
magazeti na vitabu namba 5 ya mwaka 1988
iliyofanyiwa marekebisho na sheria no. 8 ya mwaka 1997, sheria ya
tume utangazaji Zanzibr no. 7 ya mwaka 1997 iliyorekebishwa na
sharia no. 1 ya mwaka 2010 na
kuwasilishwa kwa mamlaka husika.
Alisema
kuwa, pia wamewahi kukutana na Rais na kumueleza kuhusu sheria hizi na waziri ,
lakini ipo haja ya kuonana nao tena ili tuone
hili linafikia pazuri.
“
Haitapendeza hata kidogo kuona huu mwaka unamaliza, na hatujajua hatma ya sheria
hizi na kilio chetu cha muda mzuri kikiwa bado hakijapatiwa ufumbuzi” alisema.
Katibu mtendaji wa baraza la habari Tanzania (MCT) Ernest
Sungura, akigusia kuhusu uhuru wa vyombo vya habari na mabadiliko ya tabianchi,
alisema vyombo vya habari vitatekeleza kwa ufanisi wajibu wao, katika
kulinda mazingira iwapo wandishi
watakuwa huru kutekeleza majukumu yao
bila ya hofu kisheria.
‘’ Kauli mbiu ya kimataifa mwaka huu ilikuwa katika uhifadhi wa mazingira , lakini bila ya kuwa na sheria nzuri za habari hatuwezi kutekeleza hayo tunayoyataka,’’ alisema.
Aidha alivitaka vyombo vya habari kubuni mbinu mpya za kukabiliana na changamoto za
kiuchumi na kufikiria njia ya kuendana
na kasi ya mageuzi ya maswala ya kiteknolojia ili kulinda uhuru wao.
Akifafanua
kuhusu mapendekezo ya mchakato wa mabadiliko ya sheria za habari Zanzibar, Katibu Mtendaji Tume ya Utangazaji
, Suleiman Salim alisema, tayari mapendekezo hayo yapo katika ofisi ya
mwanasheria mkuu wa Serikali kwa ajili ya hatua zaidi.
Alisema
mswada wa sheria za habari upo kwa mwanasheria mkuu na karibuni
utakwenda baraza la wawakilishi
kama mswada, hivyo tunawaomba
waliokuweko kule wachangie vizuri ili uweze kupita.
“ Tayari
Serikali imeshakamilisha mchakato wa
kuandaa sera mpya ya habari, na
ninawatoa hofu kuwa itazinduliwa hivi karibuni’’ alisema.
Maadhimisho
ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari2024,
yameandaliwa na baraza la habari Tanzania Zanzibar ,( MCT ZNZ), chama
cha wandishi wa habari wanawake ( TAMWA ZNZ) , jumuiya ya wandishi wa habari za
maendeleo (WAHAMAZA) na klabu ya
waandishi wa habari Zanzibar ( Z P C) kwa kushirikiana na shirika la
Common weath Foundation na kauli
mbiu ilikuwa ni ‘’ UHURU WA VYOMBO VYA HABARI
NA MAGEUZI YA SERA NA SHERIA ZA HABARI ZANZIBAR’’
MWISHO
Post a Comment