RC MJINI MAGHARIBI, AITAKA SUZA KUENDELEA KUIBUA VIPAJI VYA UWANDISHI
NA MARYAM NASSOR
MKUU wa mkoa wa mjini magharibi
Unguja, Idrissa Kitwana Mustafa , amekitaka chuo kikuu cha taifa Zanzibar ( SUZA) kuendelea kuandaa mashindano ya waandishi chipukizi ili kuwapima uwezo wao katika kada hiyo.
Ameyasema hayo, katika hafla ya kuwatunuku vyeti na zawadi washindi wa shindano la waandishi chipukizi huko katika chuo cha suza kampasi ya kiliman.
Alisema ,
fani ya uwandishi wa habari ni kada nyeti sana, hivyo ni vyema wanafunzi
wakasoma na kufanya kazi kwa bidii, kwani siku hizi kumeibuka wimbi kubwa la
watu wanaojiita waandishi bila ya kuwa na sifa ya Uaandishi au bila ya kusomea
fani hiyo.
“ Siku hizi
kumeibuka wimbi la waandishi makanjanja na wao wanajiita waandishi wa habari
wakati hawajasoma hata cheti katika habari na kuichafua kada hii kwa kwenda
kinyume na maadili ya uwandishi”alisema.
Aidha
alisema kuwa, kwa kupitia mashindano kama hayo, watapatikana wandishi wazuri na
wajuzi wa lugha kwani ili uwe mwandishi mzuri basi , uwe na uwelewa wa lugha
nyingi ikiwemo kichina ambacho kinafundishwa katika chuo hicho.
Nae
mwenyekiti wa kamati ya majaji, Saleh
Yussuf Mnemo alisema kuwa, kazi
zilizowasilishwa zilikuwa ni 40 na zote zilikuwa nzuri na zenye sifa hivyo walipata wakati mguu kumtafuta
mshindi.
Alisema kuwa, katika vipengele vilivyoshindania vilikuwa ni vipengele vitatu ambavyo ni uwandaaji wa makala za televisheni na radio, makala za mtandaoni na utangazaji .
Akisoma risala fupi ya chuo hicho, Khamis Juma
Abdallah ambae ni mkuu wa habari na mawasiliano
chuo cha suza, alisema kuwa lengo la kuandaa mashindano hayo ni kujali
mchngo wa vijana hao na ililenga
vijana kuanzia miaka 18 hadi 35. Na
sharti awe amepita katika vyuo vya suza.
Nae, balozi
mdogo wa China , anaeishii Zanzibar zheng min alisema kuwa kuna ofa kubwa ya
masomo kwa wanafunzi wa Zanzibar, hivyo ni vyema wakasoma kwa bidii na
kujifunza lugha ya kichina ili wanufaike na fursa hiyo.
Mashindano hayo, yaliyodhaminiwa na baraza la
habari Tanzania kwa upande wa Zanzibar (MCT ZNZ), chama cha waandishi wa habari
(ZPC) na SUZA Washindi katika mashindano hayo, walidhawadiwa vyeti na fedha
taslimu .
MWISHOO
Post a Comment