MKASA WA MTOTO WA MIEZI MINNE KUKATWA MKONO KWA UZEMBE, WIZARA YA AFYA ZNZ YATOA UFAFANUZI
NA MARYAM
NASSOR
MKASA wa
mtoto wa miezi minne kukatwa mkono kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni uzembe
wa madaktari katika Hospitali ya Mkoa Lumumba, umeilazimu Wizara ya Afya
Zanzibar kutoa ufafanuzi kuhusu tukio hilo.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Mngereza Miraji,
amesema kwamba kufuatia malalamiko yaliyotolewa na mzazi wa mtoto huyo, wizara
imechukua hatua kadhaa za awali.
Amesema kuwa,
kwa kuwa suala hilo linahusisha taratibu za kitabibu, wizara imeelekeza
kufanyika kwa uchunguzi wa kina kwa kuunda tume maalumu ya Baraza la Wauguzi na
Wakunga Zanzibar kwa kushirikiana na Baraza la Madaktari, ili kufanya uchunguzi
ndani ya wiki mbili na kutoa majibu sahihi. Uchunguzi huo unalenga kubaini
kilichotokea na hatua gani za kitaaluma zilizokiukwa.
Dk. Mngereza
ameongeza kuwa Wizara ya Afya imeamua kwenda mbali zaidi kwa kuwasimamisha kazi
wauguzi wawili wa zamu waliokuwepo siku ya tukio, ambao wanadaiwa na wazazi wa
mtoto kuwa walihusika na uzembe uliosababisha mkono wa mtoto kuathirika.
“Wizara ya
Afya imeamua kuwasimamisha kazi wauguzi wawili wa Afya ambao ndiyo
wanalalamikiwa na mzazi wa mtoto huyo, ili kupisha uchunguzi,” amesema Dk.
Mngereza.
Awali, mnamo
tarehe 15 Novemba 2025, kulitolewa malalamiko kuhusu uzembe wa wauguzi katika
Hospitali ya Mkoa wa Mjini Magharibi, baada ya mtoto huyo wa miezi minne
kufikishwa hospitalini hapo akitokea Hospitali ya Jeshi Kibweni, ambako alikuwa
amepewa rufaa kufanyiwa upasuaji wa tumbo.
Awali mzazi wa mtoto huyo, Safia Said
Omar , alisema alipogundua tatizo
hilo aliwaomba madaktari wa hospital hilo kumtoa kenyula mtoto
huyo kabla haijaleta madhara na
wakaendelea kupuuza hilo.
Amesema
kuwa, manesi wa Lumumba hawajali kuhusu wagonywa kwani wamesababisha mtoto mdogo kupata operation
mbili jambo ambalo ni gumu kukubali
Imeelezwa
kuwa kati ya tarehe 15 hadi 19 Novemba, mtoto huyo alipatwa na tatizo la
kuvimba mkono na kubadilika rangi wakati akipatiwa matibabu Hospitalini hapo.
Mzazi wake alidai kuwa aliwaomba wauguzi wamtoe
kanula aliyokuwa amewekewa, lakini wakaendelea kuiacha h adi hali ya mkono
ilipozidi kuwa mbaya na hatimaye kulazimu kukatwa kwa mkono wake wa kulia.
“ Niliwaomba sana wale wauguzi wamtoe kenyula
mwanangu nilipomuona amebadilika rangi
ya mkono wake na walikataa baadae wakasema itabidi akatwe mkono na alipwe fidia
jambo ambalo si muhimu, wakati walikuwa na uwezo wa kumsaidia aisifikie huko “
amesema mzazi huyo.
Kwa sasa,
mtoto huyo anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili
jijini Dar es Salaam.
MWISHO
Post a Comment