WANANCHI WA ZANZIBAR WAMETAKIWA KUWA NA UTARATIBU WA KUJICHUKUZA SARATANI YA MATITI


Na Maryam Nassor

WANANCHI wa Zanzibar  wametakiwa  kuwa na utaratibu wa  kupima Afya zao mara  kwa mara ,kutokana na kuongezeka  kwa Ugonjwa wa saratani ya matiti nchini Tanzania.

Wakizungumza na waandishi wa Habari , katika kambi ya Matibabu huko katika Ukumbi wa Kariakoo Mjini Unguja  Afisa  kutoka Kitengo Shirikishi  cha Afya ya Uzazi na Mtoto kutoka Wizara ya Afya Zanzibar Mwanafatima Ali Mohamed

 Amesema , Wimbi la wagonjwa wa saratani ya matiti linaendelea kuongezeka  nchini Tanzania, huku wataalamu wa afya wakionya kuwa idadi hiyo inaweza kuongezeka zaidi iwapo jamii haitachukua hatua za mapema za uchunguzi na kinga.

Amesema kuwa, takwimu za ugonjwa huo  Duniani  zinaonesha kukuwa katika wagonjwa 10 wakipimwa afya zao watano wanagundulika na Saratani hiyo.

Amesema kutokana na mwezi huu ni mwezi wa kutoa uwelewa kwa wananchi wameandaa kambi mbali mbali za Matibabu katika Wilaya ya Magharibi ‘A’ Unguja na wamewapima watu zaidi ya mia mbili  ( 200)  na Chumbuni waliwapima watu 170 na bado wanaendelea kutoa huduma hiyo katika shehia nyengine.

 “ Kwa upande wa saratani ya matiti tumewapima watu  wengi lakini pia tuliwakuta wanawake zaidi ya 20 wanadalili za ugonjwa huo na mwanamke mmoja alikuwa  ameathirika na ugonjwa huo “ amesema .

 Aidha amesema kuwa, tokea waanze kazi hiyo  mwaka jana June 2024 mpaka sasa  jumla ya wananchi 740,000 tayari wameshawapima kupitia kambi hizo za Matibabu Unguja na Pemba.

 

Daktari  huyo , amesema idadi ya wagonjwa wa saratani ya matiti imeongezeka kwa kasi katika kipindi cha miaka  ya hivi karibuni  hali inayochangiwa na mabadiliko ya mfumo wa maisha, lishe duni na kuchelewa kufanyiwa uchunguzi

Amesema sababu nyingine ni uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa uchunguzi wa mapema wa saratani ya matiti, na bado kuna hofu miongoni mwa wanawake wengi kwenda hospitalini wakihisi uvimbe au maumivu.

“Wengi wakiona dalili za awali, hufikiri ni mambo madogo kama mabadiliko ya homoni au maumivu ya kawaida ya kifua. Wengine wanaogopa matokeo ya uchunguzi, jambo linalosababisha kuchelewa kupata tiba sahihi,” aliongeza.


Miongoni mwa waliopitia changamoto hiyo ni  Subira Ali Hamza, mkazi wa Matemwe   mkoa wa Kaskazini Unguja, ambaye kwa sasa ni mnusurika wa saratani ya matiti. amesema aligunduliwa kuwa na ugonjwa huo  baada ya kupuuza dalili kwa zaidi ya miezi sita.

Alisema kwa mara ya kwanza, alienda hospital na kumueleza Daktari kuwa kafanya boje akaambia ajichuwe kwa maji ya moto baada ya mwezi akarudi tena hali bado na akaambiwa akafanye kipimo cha Utra sound na kugundulika na ugonjwa huo.

“Nilianza kuhisi uvimbe mdogo kwenye chuchu, lakini nilipuuzia nikidhani utapotea , Baadaye nilianza kuumwa na nilipoenda hospitali madaktari waliniambia nina saratani , nilipoteza  nguvu na matumaini, lakini kwa msaada wa familia na matibabu, nilipona,” alisema kwa hisia.

Amesema kwa  sasa anatumia uzoefu wake, kuelimisha wanawake wengine kuhusu umuhimu wa kufanya uchunguzi wa mara kwa mara ili kugundulika mapema ugonjwa huo.

“Ninawashauri wanawake wenzangu wajipende, wajichunguze na waende hospitalini mapema Saratani inapogunduliwa mapema, ina tiba,” alisisitiza.


Kwa upande wake, DKT Merirose Kaya Giatus  Dokta Bingwa wa Magonjwa ya jamii kutoka  Asasi ya JAPAIGO, amesema  wao kama wadau wanafanyakazi na Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar na wamejikita  katika  kusaidia  katika afua ya Magonjwa yasioambukizwa .

 Amesema, Katika mwezi wa Oktoba   wamewamejikita katika kutoa  elimu ya kinga na kuwajengea uwezo wahudumu wa Afya katika  uchunguzi wa kupapasa lakini pia uchunguzi wa kina kwa kutumia shindano .

Amesema kuwa, watawawezesha pia madaktari kuweza kutoa huduma kwa wagonjwa wa saratani ya Matiti na wao kama mradi wataendelea kutoahuduma hizo kwa kipindi cha miaka mitano.

Aidha amesema kuwa, takwimu zinaonesha ugonjwa wa saratani ya matiti unaongoza kwa kuuwa zaidi ukilinganisha na saratani ya shingo ya mlango wa kizazi.

“ Na Bahati mbaya wagonjwa wa saratani ya Matiti wanaogundulika  zaidi ya asilimia 50 wanapoteza maisha, ukichunguza wanawake 10  basi  watano wanapoteza maisha, kwani wengi wao wanagunduliwa katika stage ya tatu  ambao ni vigumu kutibika “ amesema.

“Wanaume wana nafasi muhimu katika kuwahamasisha wake zao, dada au mama zao kwenda kupima. Saratani ya matiti si ugonjwa wa wanawake pekee, hata wanaume wachache hupata, hivyo elimu ni ya wote,” amesema.

 

Aidha amesema kuwa, kuna vichocheo vingi vinavyosababisha Saratani hiyo, ikiwemo  mtindo wa maisha , vinasaba vya urithi na shida kubwa  ni jamii hawajui visababishi vya ugonjwa huo.

 

Ameongeza kuwa ,serikali inaeendelea kuboresha miundombinu ya matibabu katika hospitali za mikoa, ikiwa ni pamoja na huduma za uchunguzi wa saratani, ili wananchi wengi wapate huduma .

Amewaomba wananchi wa Zanzibar, kuwa na utamaduni wa kujichunguza  matiti yao mapema ili wakigundulika inakuwa rahisi kupata matibabu na kupona kwa haraka.

                                     MWISHO

Top of Form

Bottom of Form

 

No comments

Powered by Blogger.