MGOMBEA URAIS WA CHAMA CHA ADC AMEAHIDI SHIBE KWANZA KWA KILA MZANZIBAR


NA MARYAM NASSOR,

MGOMBEA Urais kwa tiketi ya chama cha Alliance for Democrats Change ( ADC)  Hamad Rashid Mohammed  ameehidi neema ya shibe kwanza kwa kila Mzanzibar endapo atachaguliwa.

Ameyasema hayo,  huko katika Afisi za Chama hicho Daraja bovu wilaya ya  Magharibi ‘A’  Unguja.

Mgombea huyo amesema , akipewa ridhaa na wananchi wa Zanzibar atahakikisha  shibe kwanza kwa kuweka mazingira mazuri ya upatikanaji  wa Chakula.

Amesema kuwa, kipaumbele chake Cha pili atahakikisha elimu bure kwa kila  mzanzibar kuanzia chekechea mpaka  chuo kikuu.

Aidha amesema kuwa,  kima Cha chini Cha mshahara kwa kila mfanyakazi atalipwa shilingi laki sita za kitanzania

"Nawaombeni sana ndugu zangu , vipaumbele vyetu mumevisikia  na vinauzika  kwa wananchi ,maamuzi mutafanya nyie"amesema mgombea huyo.

Nae, Mwenyekiti wa wanawake wa Chama hicho na mgombea wa ubunge Jimbo la Malindi, Nadhra Ali Haji amelishukuru jeshi la polisi kwa kuimarisha ulinzi muda wote wakati wanamsindikiza mgombea wao, kuchukua fomu ya uteuzi tume ya  uchaguzi Zanzibar.

"Kwa kweli jeshi la polisi limefanya kazi nzuri ya kuimarisha ulinzi kwa kila Chama bila ya upendeleo na hivyo ndivyo inavyotakiwa" amesema.

 

Aidha amewaomba wananchi wa Zanzibar kukipigia kura nyingi Chama hicho tarehe Oktober 29 ili kuhakikisha kinapata ushindi na  kuwaletea maendeleo.

Nae, mgombea ubunge Jimbo la Chumbuni Zanzibar, kwa tiketi ya Chama hicho Mafunda Faisal Ali amewaomba  wanachama wa Chama hicho, kuendelea kutunza amani ya nchi kwani bila ya amani hakuna maendeleo.

" Ndugu zangu tuendelee kutunza amani ya nchi yetu na  naowambeni sana kukipigia kura nyingi za ndiyo Chama chetu ili tushirikiane kuleta maendeleo ya nchi yetu " amesema.

 

                                      MWISHO

                            

 

No comments

Powered by Blogger.