WAANDISHI WATAKAO GOMBEA NAFASI ZA UONGOZI WAONDOKE KATIKA VYUMBA VYA HABARI- MCT
NA MARYAM NASSOR
WAANDISHI
wa Habari nchini wanaojihusisha na masuala ya siasa
wametakiwa kuondoka katika vyumba vya Habari ili kuepusha mgongano wa
kimaslahi.
Akizungumza na wandishi wa Habari katika Afisi za Chama Cha Wandishi wa Habari wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ) huko Tunguu, Mjumbe wa Kamati ya Maswala ya Habari Zanzibar (ZAMECO) bi Hawra Shamte.
Akisoma
muongozo, wa Baraza la Habari Tanzania
(MCT) uliyotolewa mwaka huu 2025 na kutiwa Saini na Mkurugenzi wa Baraza
hilo , bi Hawra Shamte amesema kila raia
wa nchi hii ana haki ya kugombea.
Amesema , Katiba
ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka
1977 ibara ya (21) inampa kila
raia haki ya kugombea nafasi za kisiasa , ibara hiyo inasema kila
raia wa
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
anastahili kushiriki katika Serikali ya nchi hii ama moja kwa moja au
kupitia wawakilishi waliyochaguliwa kwa hiari yake kwa kufuata utaratibu
uliyowekwa na sheria hii inajumuisha haki ya kupiga kura na kugombea katika
chaguzi mbali mbali
Amesema
kuwa, kwa hali hiyo wandishi wa Habari wana haki ya kugombea nafasi za kisiasa kama ilivyo kwa raia wengine, hata hivyo kuendelea kuwa mwandishi wa Habari huku ukijihusisha na siasa ni kinyume na maadili ya taaluma ya Habari.
Kwa
mujibu wa muongozo huo wa ( MCT)
mwandishi anayegombea nafasi ya
kisiasa anapaswa kuondoka kwenye chumba
cha Habari ili kuepuka mgongano wa kimaslahi na kupoteza uwaminifu kwa umma.
Anaendelea kusema kuwa, wandishi wa Habari wanaojihusisha na siasa kwa kugombea nafasi za uongozi huku wakiendelea na kazi yao, wanakabiliwa na
athari kubwa kwa taaluma yao , na tasnia ya habari.
“ Kwa mfano mwandishi wa Habari kagombea Chama cha ACT yeye ni mwandishi wa Habari lakini anapokwenda kuchukuwa Habari Chama cha Mapinduzi ( CCM ) atakataliwa kwa sababu hawatamuamini kwa hiyo huo sio uwandishi” amesema.
Amesema mwandishi
wa Habari hapaswi kuwa na upendeleo, sasa unapokuwa na mapenzi makubwa ya chama
kiasi cha kugombea unaonekana na wewe
huwezi kufanya haki wakati ukiandika Habari zako, unaonekana hutendi uwaminifu
katika kazi na unaitia dosari taaluma.
Aidha
amesema kuwa, unapotaka kuwa mwanasiasa
kindaki ndaki bora kazi ya habari uiyache kwa muda ili kuepuka mgongano ya kimaslahi na kupoteza uwaminifu kwa umma
na jamii kwa ujumla.
Awali katika kikao hicho, Mkurugenzi wa TAMWA
ZNZ, Dk Mzuri Isaa amewashukuru wajumbe wa baraza la wawakilishi ambao kwa
namna moja au nyengine wameuliza maswali kuhusu sheria ya Habari.
Amesema
kuwa, ZAMECO itaendelea kushirikiana na wajumbe wa baraza hilo ili kuona sheria
nzuri na rafiki ya Habari inapatikana.
“ Katika
kipindi tunachoelekea wandishi wa Habari mara nyingi wanakumbana na matukio
ya kiusalama hivyo ni vizuri tungepata
sheria mpya na rafiki ili kuwalinda wandishi wanapotimiza majukumu yao” amesema
.
Nae, bi
Shifaa Saidi mjumbe wa ZAMECO amesema kuwa,
kuelekea katika uchaguzi mkuu ni vyema wandishi wa Habari wakafanya kazi
kwa mashirikianao.
Aidha amewataka
, wandishi wa Habari watakaopata matatizo kuelekea kipindi cha uchaguzi ni vyema wakatoa taarifa mapema ili kuweza
kusaidiwa.
Nae,
mwakilishi wa jimbo la Pandani Pemba Profesa Omar Fakih amewataka ZAMECO kuendelea kufanya uchechemuzi
wa sheria rafiki ya habari kwani sheria
inayotumika sasa ni ya zamani tokea miaka ya 1988 na haiendani na wakati.
Amesema
kuwa, sheria hiyo tayari imeshaanza kuzungumzwa katika baraza la wawakilishi na
anaimani muda si mrefu ujayo sheria hiyo itamfikia Spika wa baraza hilo.
Nao, Baadhi
ya Wandishi wa Habari waliopata nafasi ya kuchangia katika kikao hicho wamesisitiza kuwa, wandishi wa Habari kuendelea kufanya
kazi kwa umoja na ushirikiano na kulindana wakati wa matatizo.
Kikao hicho cha
siku moja kimeandaliwa na kamati ya Maswala ya Habari (ZAMECO) kimewashirikisha wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi ( B L W) na wandishi wa Habari .





Post a Comment