“ Mtindo wa maisha unavyoweka rihani maisha ya mama wajawazito”
NA MARYAM NASSOR
Lishe bora ni kitu
muhimu kinachopaswa kuzingatiwa na jamii
ili kuwa na Watoto wenye afya na makuzi bora.
Hii ni
kwasababu lishe husaidia mwili kukua
vyema, kujengeka na kuimarisha kinga ya
mwili kupambana na magonjwa.
Mtindo wa
maisha wenye afya unaozingatia lishe bora, mazoezi na kuepuka
vitu vinavyoweza kuwa na madhara ni miongoni mwa mambo muhimu anayotakiwa kufuata mjamzito ili aendelee vizuri.
Mambo hayo
kama yatafuatwa yatamsaidia mama na
mtoto kuepuka hatari zisizo za lazima.
Imeelezwa
kuwa katika maisha ya sasa, mtindo wa
maisha ni moja ya sababu zinazochangia hatari kubwa kwa wajawazito na vifo vya
mama na mtoto.
Daktari
bingwa wa magonjwa ya kina mama na Watoto kutoka Hospitali kuu ya Mnazi mmoja Unguja, Umulkulthum Omar anaeleza mtindo wa maisha unavyoathiri afya za mama na mtoto.
Anasema,wajawazito
wengi wanaohudhuria hospital wanakuwa na upungufu wa damu kutokana na vyakula
wanavyokula.
“ utamkuta
msichana anakula chipsi na urojo akija kuolewa akipata ujauzito hawezi kula,
mwili wake unakuwa hauna nguvu kwa
kukosa virutubisho, kinachotokezea ni upungufu wa damu” anasema Dk Umu.
Anasema
kuwa, ni vyema jamii ikabadilika na kutumia vyakula vyenye virutubisho kutoka
makundi yote ya vyakula ili kuwajenga Watoto kuwa na afya njema tokea wako
wadogo.
“ Madaktari
kipindi tunachokuwa hatulali na kukoroma ni kile kipindi cha mwezi wa
Ramadhani, wajawazito wengi hupoteza maisha kwasababu ya kukosa damu” anasema
Dk Umulkuruthum huku akishauri jamii ibadilishe mitindo yao ya maisha kwa kuona
usasa ni kula vyakula ambavyo havina faida katika miili yao.
Ingawa
Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vya
wajawazito vinavyotokana na matatizo ya uzazi kutoka wastani wa vifo 556 kwa
kila vizazi hai 100,000 kwa mwaka
2015/16 hadi kufikia wastani wa vifo 104 kwa kila vizazi hai 100, 000 mwaka 2022.
Lakini anashauri kuwa, ipo haja kwa jamii
kubadili mitindo yao ya maisha kwa kula vyakula vyenye afya na ambavyo havina
chumvi nyingi na mafuta ili kuimarisha
afya zao, ambavyo viko karibu na wao kama mboga mboga za majani.
Haitham Abdalla,
ni mama wa Watoto watatu anasema mara
nyingi akihudhuria kliniki ya wajawzito huwa anaambiwa hana damu kwani anakuwa
na kiwango cha damu tisa, hapo mimba ipo katika mwezi wa saba.
Anasema
kuwa, akiwa mjamzito anatapika sana na
kupelekea kushindwa kula, na kila miezi ikienda mbele damu inashuka na kushauriwa kutumia vidonge
vya kuongeza damu mpaka ajifunguwe.
“ Nikiwa
mjamzito kawaida sipendi kula na hata nikila huwa napenda niletewe urojo ndio
unanipa hamu ya kula” anasema Haitham.
Nae, Abdalla
Ali ni Baba wa Watoto wawili mkaazi wa
Mfenesini Unguja anasema, wanawake wengi wakiwa wajawazito hawapendi kula
kutokana na hali zao lakini pia kujiendekeza.
Anasema
kuwa, utamkuta mwanamke mjamzito hana damu lakini ukimpelekea vyakula vya damu
kama mboga mboga , maharage na matunda
Havili, “ Anasema siwezi kula ni kweli lakini anatakiwa ajitahidi kula
kwasababu hayuko pekee yake ana kiumbe tumboni ambacho kinahitaji kula kupitia
mama yake” anasema.
Anasema
kuwa, ni vyema wanawake wakiwa wasichana wapewe elimu ya lishe bora, waaache kula vyakula ambavyo havina
faida katika miili yao, kwani wao ni mama watarajiwa.
Nae, Fatma
Haji mama wa Watoto watano , mkaazi wa Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja
anasema mara nyingi akiwa mjamzito huwa anakosa damu, kutokana na kukosa lishe
bora.
Anasema
kuwa, baadhi ya wanaume hawazihudumii
familia zao ipasavyo kwa kupeleka
vyakula vizuri majumbani .
“ Mimi mume
wangu ni mchuuzi lakini Samaki wazuri hawaleti nyumbani, labda labda awe tayari
kaanza kuharibika wateja wawe hawamtaki ndio amlete nyumbani kwa hali hiyo ndio
maana tunakosa damu” anasema Maryam.
Anasema
kuwa, ni vyema wanaume wapewe elimu ya
afya bora ili isaidie kuleta vyakula
vyenye afya majumbani .
Kwa mujibu
wa ripoti ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO)linasema kila siku wanawake 830 hufariki dunia
kutokana na matatizo wakati wa
kujifungua na asilimia 99 ya vifo hutokea katika nchi zinazoendele.
Maryam Ali Hassan ni Mratibu wa
Afya ya Uzazi ya mama na mtoto wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja, anashauri wajawazito
kuepuka kula vyakula ambavyo havina faida katika afya zao kama udongo na makaa
na kula vyakula vyenye virutubisho kutoka katika makundi yote ya chakula.
“
Tunaendelea kutoa elimu kwa jamii waone
umuhimu wa kula vyakula vyenye Afya na virutubisho ili kulea mimba vyema na
kujifungua salama” anasema.
Aidha
amewasihi kina baba wawe karibu sana na wake zao kipindi cha ujauzito na kuwahudumia kwa kuwapa vyakula vyenye afya
ili kuepusha kuzaa Watoto wadumavu na kupunguza vifa vya mama na mtoto.
MWISHO NA MARYAM NASSOR
Lishe bora ni kitu
muhimu kinachopaswa kuzingatiwa na jamii
ili kuwa na Watoto wenye afya na makuzi bora.
Hii ni
kwasababu lishe husaidia mwili kukua
vyema, kujengeka na kuimarisha kinga ya
mwili kupambana na magonjwa.
Mtindo wa
maisha wenye afya unaozingatia lishe bora, mazoezi na kuepuka
vitu vinavyoweza kuwa na madhara ni miongoni mwa mambo muhimu anayotakiwa kufuata mjamzito ili aendelee vizuri.
Mambo hayo
kama yatafuatwa yatamsaidia mama na
mtoto kuepuka hatari zisizo za lazima.
Imeelezwa
kuwa katika maisha ya sasa, mtindo wa
maisha ni moja ya sababu zinazochangia hatari kubwa kwa wajawazito na vifo vya
mama na mtoto.
Daktari
bingwa wa magonjwa ya kina mama na Watoto kutoka Hospitali kuu ya Mnazi mmoja Unguja, Umulkulthum Omar anaeleza mtindo wa maisha unavyoathiri afya za mama na mtoto.
Anasema,wajawazito
wengi wanaohudhuria hospital wanakuwa na upungufu wa damu kutokana na vyakula
wanavyokula.
“ utamkuta
msichana anakula chipsi na urojo akija kuolewa akipata ujauzito hawezi kula,
mwili wake unakuwa hauna nguvu kwa
kukosa virutubisho, kinachotokezea ni upungufu wa damu” anasema Dk Umu.
Anasema
kuwa, ni vyema jamii ikabadilika na kutumia vyakula vyenye virutubisho kutoka
makundi yote ya vyakula ili kuwajenga Watoto kuwa na afya njema tokea wako
wadogo.
“ Madaktari
kipindi tunachokuwa hatulali na kukoroma ni kile kipindi cha mwezi wa
Ramadhani, wajawazito wengi hupoteza maisha kwasababu ya kukosa damu” anasema
Dk Umulkuruthum huku akishauri jamii ibadilishe mitindo yao ya maisha kwa kuona
usasa ni kula vyakula ambavyo havina faida katika miili yao.
Ingawa
Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vya
wajawazito vinavyotokana na matatizo ya uzazi kutoka wastani wa vifo 556 kwa
kila vizazi hai 100,000 kwa mwaka
2015/16 hadi kufikia wastani wa vifo 104 kwa kila vizazi hai 100, 000 mwaka 2022.
Lakini anashauri kuwa, ipo haja kwa jamii
kubadili mitindo yao ya maisha kwa kula vyakula vyenye afya na ambavyo havina
chumvi nyingi na mafuta ili kuimarisha
afya zao, ambavyo viko karibu na wao kama mboga mboga za majani.
Haitham Abdalla,
ni mama wa Watoto watatu anasema mara
nyingi akihudhuria kliniki ya wajawzito huwa anaambiwa hana damu kwani anakuwa
na kiwango cha damu tisa, hapo mimba ipo katika mwezi wa saba.
Anasema
kuwa, akiwa mjamzito anatapika sana na
kupelekea kushindwa kula, na kila miezi ikienda mbele damu inashuka na kushauriwa kutumia vidonge
vya kuongeza damu mpaka ajifunguwe.
“ Nikiwa
mjamzito kawaida sipendi kula na hata nikila huwa napenda niletewe urojo ndio
unanipa hamu ya kula” anasema Haitham.
Nae, Abdalla
Ali ni Baba wa Watoto wawili mkaazi wa
Mfenesini Unguja anasema, wanawake wengi wakiwa wajawazito hawapendi kula
kutokana na hali zao lakini pia kujiendekeza.
Anasema
kuwa, utamkuta mwanamke mjamzito hana damu lakini ukimpelekea vyakula vya damu
kama mboga mboga , maharage na matunda
Havili, “ Anasema siwezi kula ni kweli lakini anatakiwa ajitahidi kula
kwasababu hayuko pekee yake ana kiumbe tumboni ambacho kinahitaji kula kupitia
mama yake” anasema.
Anasema
kuwa, ni vyema wanawake wakiwa wasichana wapewe elimu ya lishe bora, waaache kula vyakula ambavyo havina
faida katika miili yao, kwani wao ni mama watarajiwa.
Nae, Fatma
Haji mama wa Watoto watano , mkaazi wa Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja
anasema mara nyingi akiwa mjamzito huwa anakosa damu, kutokana na kukosa lishe
bora.
Anasema
kuwa, baadhi ya wanaume hawazihudumii
familia zao ipasavyo kwa kupeleka
vyakula vizuri majumbani .
“ Mimi mume
wangu ni mchuuzi lakini Samaki wazuri hawaleti nyumbani, labda labda awe tayari
kaanza kuharibika wateja wawe hawamtaki ndio amlete nyumbani kwa hali hiyo ndio
maana tunakosa damu” anasema Maryam.
Anasema
kuwa, ni vyema wanaume wapewe elimu ya
afya bora ili isaidie kuleta vyakula
vyenye afya majumbani .
Kwa mujibu
wa ripoti ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO)linasema kila siku wanawake 830 hufariki dunia
kutokana na matatizo wakati wa
kujifungua na asilimia 99 ya vifo hutokea katika nchi zinazoendele.
Maryam Ali Hassan ni Mratibu wa
Afya ya Uzazi ya mama na mtoto wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja, anashauri wajawazito
kuepuka kula vyakula ambavyo havina faida katika afya zao kama udongo na makaa
na kula vyakula vyenye virutubisho kutoka katika makundi yote ya chakula.
“
Tunaendelea kutoa elimu kwa jamii waone
umuhimu wa kula vyakula vyenye Afya na virutubisho ili kulea mimba vyema na
kujifungua salama” anasema.
Aidha
amewasihi kina baba wawe karibu sana na wake zao kipindi cha ujauzito na kuwahudumia kwa kuwapa vyakula vyenye afya
ili kuepusha kuzaa Watoto wadumavu na kupunguza vifa vya mama na mtoto.
MWISHO

Post a Comment