“ SARATANI YA SHINGO YA MLANGO WA KIZAZI NI HATARI KWA WATU WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI’’


Maryam Nassor

SARATANI ya shingo ya  mlango wa kizazi ni aina ya saratani inayotokea kwenye mlango wa kizazi (sehemu inayounganisha uke na mji wa mimba).

Saratani hii husababishwa kwa kiwango kikubwa na maambukizi ya muda mrefu ya virusi vya Human Papillomavirus (HPV), hasa aina za HPV 16 na 18.

 Watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi wako katika hatari kubwa zaidi ya kupata saratani hii kutokana na mfumo wao wa kinga ya  mwilini kuwa dhaifu.

Kwa mujibu wa ripoti ya  Shirika la Afya Duniani ( WHO) ya  mwaka 2020 inasema   saratani ya shingo ya mlango wa kizazi ni ya nne kwa kuathiri wanawake, ikiwa na wagonjwa zaidi ya 604,000 .

Takribani  asilimia 90 ya vifo  hutokea kila mwaka , hasa  katika nchi zenye kipato cha chini na kati kama Tanzania.

Takwimu za WHO zinaonesha  kuwa, kila mwaka Tanzania inapata wagonjwa wapya 42,000 wa saratani  ya shingo ya mlango wa kizazi ambao wanafika katika vituo vya Afya.

Akizungumza na mwandishi wa Makala hii,  Daktari dhamana kutoka Hospitali ya Wilaya  ya Kaskazini ‘A’ Unguja  Kivunge Haji Machano  anasema  ugonjwa  wa saratani ya shingo ya mlango wa kizazi huwapata sana watu wanaoishi na ugonjwa wa ukimwi ukilinganisha na watu wengine.

Ameeleza kuwa, ugonjwa huo huwapata sana wanawake  wanao ishi na maradhi ya ukimwi   kutokana na kudhofika kwa kinga zao na kwa Bahati mbaya hufika Hospitali wakiwa katika hatua ya pili na tatu  hivyo ni taabu kutibika.

Anasema kuwa, watu wenye ugonjwa wa  ukimwi hupunguza uwezo

Wa mwili kupambana na HPV kwa kuwa ndio kirusi kinachosababisha saratani ya shingo  ya mlango wa  kizazi.

”Watu wanaoishi na VVU wanapata maambukizi sugu ya HPV ambayo huwaengeza hatari ya kuendelea hadi hatua ya saratani” anasema dk Haji.

Aidha anasema kuwa, katika wilaya ya kaskazin ‘A’ Unguja ugonjwa huo huwa athiri wanawake  hasa wanaoishi na maradhi ya Ukimwi. 

Anasema kuwa, saratani hutokea mapema zaidi kwa watu waishio na VVU kuliko watu wasio uguwa ugonjwa huo, na matibabu yake huwa na changamoto zaidi kutokana na kinga ya mwiili kupungua.

Halima Ali shuhuda wa ugonjwa huo, anasema  alikuwa anatokwa na damu kila akishiriki tendo la ndoa na mume wake.

“ Nilikuwa natokwa na damu usiku na mchana kila niliposhiriki tendo la ndoa , nilijua nimerogwa na mke mwenzangu  nilimaliza waganga mpaka siku moja nikamuhadithia rafiki yangu na kunishauri nije Hospitali ndipo nikafanya vipimo na kugundulika ni saratani” anasema

Anasema kuwa, ni vyema jamii ikawa na utaratibu wa kuchunguza afya zao mara kwa mara ili kubainika mapema  na kupata matibabu katika hatua za awali.

Naye, mgonjwa mwengine Asha Ame ( si jina lake halisi)  alikuwa ameketi  kwenye kiti,huku kichwa chake  akikiinamisha chini   yeye ni mkaazi wa Nungwi mkoa wa Kaskazini Unguja  anasema  baada ya kuanza matibabu harufu  mbaya imekata  na sasa anaendelea vizuri.

Amesema ,” Mimi nilikuwa natoka na uchafu wenye harufu katika sehemu zangu za siri ndipo nikaja kufanya vipimo na nikagundulika ni saratani ya shingo ya  mlango wa kizazi”  ameendelea kusema kuwa ni vyema watu wakawa na utaratibu wa kufanya uchunguzi mara kwa mara.

Anasema kuwa,  wanawake wanaoishi na virusi vya Ukimwi  wako hatarini zaidi hivyo aliwata wanawake kuchunguza afya zao mapema ili kupata matibabu .

 Daktari Umukulthumu Omar kutoka Hospitali ya Mnazi mmoja anasema saratani ya shingo ya mlango wa kizazi inaweza kutibika iwapo itagundulika mapema, na kufanya vipimo vya Pap Test ( Papanicolaous Test)  Pap – smear ni kipimo ambacho hutumika kuchunguza mabadiliko ya chembe chembe zilizoko katika mlango wa kizazi  ili kugundua mabadiliko  na kuwahi kuyakabili.

“ Kinga kuna chanjo. Lakini kinga pekee kabla hujaanza kujamiiana upewe chanjo ambayo inatolewa kwa wasichana wadogo maskulini kote, tuhamasishe watu waelewe chanjo, kwa hiyo tuwapeleke mabinti wakapate chanjo” anasema Dk Umu.

Wataalamu wa Afya katika mataifa mbali mbali  ikiwemo Tanzania wamekuwa wakito elimu ya ugonjwa huo katika jamii na kuhamasisha  wanawake kujitokeza kuchunguza afya zao. Ili kujulikana mapema kama wana mabadiliko ya awali au  viashiria vya  saratani ya shingo ya  mlango wa kizazi.

Mkakati wa WHO ni kupunguza idadi  ya wagonjwa wapya kila mwaka hadi kufikia wanne au pungufu zaidi kwa kila wanawake elfu moja na kuweka  malengo matatu yatakayofikiwa ifikapo  mwaka 2030.

 

                                  mwisho

 

 

No comments

Powered by Blogger.