ASYA MOHAMED AJITOKEZA KUCHUKUWA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA KIJINI MATEMWE

NDUGU ASYA MOHAMED MUHIDIN  ACHUKUWA FOMU YA UBUNGE  JIMBO LA KIJINI MATEMWE
NA MARYAM NASSOR

ZOEZI la  uchukuaji fomu za kuomba kuteuliwa  kugombea  nafasi za  ubunge, uwakilishi  na viti maalum kupitia chama cha Mapinduzi ‘ CCM’  wilaya ya  kaskazini ‘A’ Unguja  linaendelea vizuri.

Mwandishi wa Habari hizi alifika  katika Ofisi  za Chama   hicho  wilaya ya kaskazini ‘A’  na kushuhudia  wanachama wa  chama hicho wakichukuwa fomu hizo.


Mtia nia  Asya Mohamed Muhidin kutoka Jimbo la Kijini  Matemwe mkoa wa kaskazini Unguja  alifika Ofisi za chama hicho  kuchukua fomu ya kugombea nafasi  ya Ubunge.

Akizungumza na mwandishi wa Habari hizi, nje ya Ofisi ya chama hicho mtia nia  huyo, alisema  ameamua kuchukua fomu hiyo ili kuunga  nguvu za Raisi wa Jamuhuri  ya Muungano wa Tanzania  ya kuwaletea   wananchi maendeleo.

Amesema kuwa, amevutiwa sana na kasi ya  Dk Samia ya kuwaletea  wananchi Maendeleo kwa haraka   na Rais mwanamke  wa kwanza kuiongoza Tanzania.

“ Nimechukuwa fomu hii ya kugombea ubunge katika jimbo hili  la kijini ili kusaidiana na Raisi wetu  kuwaletea  wananchi   maendeleo” amesema mtia nia huyo.

Aidha amesema  kuwa, kila mwananchi ni shahidi wa maendeleo yanayoendelea nchini kwa kipindi kifupi alichoongoza  Rais huyo.

 Akizungumzia   vipaumbele vyake, endapo vikao vya chama hicho vikirejesha jina lake  na kugombea  jimbo hilo la kijini na kushinda  kwenye  uchaguzi  mkuu wa mwaka huu ni Pamoja na kuimarisha  huduma za kijamii katika jimbo hilo, Pamoja na Elimu na Afya.

Akizungumzia kuhusu uzoefu wa kuongoza mtia nia huyo, amesema kuwa ana uzoefu wa kutosha wa kuongoza kwani alishakuwa mbunge wa viti maalumu kwa kipindi cha miaka mitano.

“ Nina uzoefu wa kutosha wa kuongoza na kuwatumikia wananchi kwani  nilisha Jifunza mengi   wakati nikiwa  mbunge wa viti maalum” amesema .

                                    MWISHO

No comments

Powered by Blogger.