WANAWAKE WAMETAKIWA KUHAMASISHANA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI.
NA MARYAM
NASSOR
WAANDISHI wa
Habari na jamii kwa ujumla wametakiwa
kuwa na mikakati maalumu ya
kuhamasisha wanawake kugombea nafasi za uongozi kwani bado wako kidogo katika
nafasi hizo.
Ameyasema
hayo, Afisa Programu wa michezo kwa
Maendeleo kutoka Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar- TAMWA
ZNZ Khairat Haji, alipokuwa akizungumza
na wandishi wa Habari na wadau mbali mbali wa michezo katika maadhimisho ya
siku ya wanawake duniani huko katika ukumbi wa TAMWA Tunguu Unguja.
Amesema kuwa, takwimu zinaonesha kuwa bado kuna upungufu wa viongozi wanawake katika nafasi mbali mbali za
uongozi nchini, kwani wanawake mpaka sasa ni asilimia 30 tu ambao wako katika nafasi hizo,
ukilinganisha na wanaume ambao wako asilimia 70.
“ Tuwaunge
mkono wanawake ambao wanatia nia ya kugombea katika nafasi mbali mbali za
uongozi na tusiwavunje moyo, kwani mwanamke akiwa kiongozi basi analeta
maendeleo kwa haraka” anasema Khairat.
Nae, mjumbe
wa bodi kutoka TAMWA ZNZ Bi Asha Abdi
amesema historia inaonesha wanawake
waliachwa nyuma sana katika shughuli
mbali mbali za maendeleo, ikiwemo nafasi za uongozi.
Amesema
kuwa, nafasi ya mwanamke katika uongozi iko nyuma na kwa hapa Zanzibar hali ilikuwa
mbaya zaidi.
“ Ni vyema
tuwe mabalozi wazuri huko uraiani tuwaunge mkono wanawake wenzetu na
ikiwezekana tuwapigie kura ili wawe viongozi” anasema Bi Asha.
Aidha
amewataka wandishi wa Habari kutumia kalamu zao, kuwaonesha wanawake ambao ni
viongozi na wanafanya vizuri katika kuihudumia
jamii na kuleta maendeleo.
Nae, Afisa
Tathimini na Ufuatiliaji kutoka TAMWA ZNZ Mohamed Khatib Mohamed amesema tafiti
iliyofanya na chama hicho inaonesha wanawake ni wachache wanaoshiriki katika
michezo mbali mbali nchini.
Amesema kuwa, utafiti huo umewashirikisha watu 102 wakiwemo makocha, wachezaji na
viongozi wa vyama vya michezo, na wamebaini kuwa Zanzibar ina sera nzuri ya
michezo ya mwaka 2018 lakini shida ni
utekelezaji wake.
“Sera ya
michezo ya mwaka 2018 ni nzuri sana, lakini utekelezaji wake ndio mbaya kwani
haina mikakati ya kuwainua Watoto wa kike washiriki michezo” anasema Mohamed.
Nae,
Kocha wa mpira wa miguu katika timu
za wanawake Khatma Mwalim Khamis ,
anasema udhalilishaji ni mkubwa katika timu za mpira wa miguu kwa wachezaji
wanawake na wanaume.
Aidha
amesema kuwa, changamoto nyengine inayowakumba wachezaji wa kike ni mila na
desturi , ambapo jamii inaona ni kinyume na desturi zao wanawake kushiriki
katika michezo.
Nae,
mwakilishi kutoka Serikali ya Ujerumani
nchini Tanzania( G IZ) Hija Mohamed Ramadhan
amesema wametengeneza mpango mkakati wa kuwalinda wachezaji kwa kushirikiana na wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto
dhidi ya vitendo vya udhalilishaji wakiwa kwenye michezo.
Aidha
amesema kuwa, kutokana na hatua hizo wanategemea siku za mbeleni ushiriki wa
wanawake katika nafasi mbali mbali katika michezo utaongezeka.
Madhimisho
hayo ya siku ya wanawake duniani yameadhimisha na Chama cha Wandishi wa Habari
Wanawake Tanzania Zanzibar, na kuwashirikisha wadau mbali mbali wa michezo, na
kauli mbiu ya mwaka huu ilikuwa ni ‘‘Ushiriki
wa Mwanamke na Msichana ni Kichocheo cha
Maendeleo’’.
mwisho

Post a Comment