WANA MAZINGIRA WALIA NA UKATAJI WA MIKOKO.
NA MARYAM
NASSOR
Mikoko ni
aina ya miti au vichaka vinavyokua katika maji ya chumvi kwenye fukwe za Bahari.
Tafiti
zinaonesha miti ya mikoko ina uwezo
mkubwa wa kufyoza hewa chafu ya kaboni kwa zaidi ya
asilimia 50 , hivyo kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Mikoko ni walinzi wakuu wa kinga ya ardhi na jamii za
pwani dhidi ya Dhuruba, tsunami , na kuongezeka kwa viwango vya usawa wa Bahari na
mmomonyoko wa ardhi .
Waasayansi
wanaamini miti ya mikoko inaweza kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya
tabianchi yanayoikumba dunia kwa sasa,
wakati ambao ulimwengu ukiwa ukishuhudia ongezeko la juu la joto katika
karne hii.
Katika
Shehia ya Unguja Ukuu Mkoa wa Kusini Unguja, wananchi wanatumia mikoko kama
njia ya asili ya kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi.
Abdi
Juma Mgeni kutoka Shehia ya Unguja Ukuu ni Katibu wa kikundi cha Mikoko ni Urithi wetu , amesema wameamua kupanda mikoko kutokana na
kuongezeka kwa kina cha maji katika Kijiji chao.
Amesema kuwa, Miti hiyo ndio urithi pekee
unaoweza kupambana na madhara ya
mabadiliko ya tabianchi Kijiji hapo,
ambapo maji ya Bahari hupanda hadi katika maakaazi yao.
Aidha
amesema kuwa, kikundi chao kimekuwa mstari wa mbele katika kushajihisha jamii
kupanda mikoko kwani wanaamini wakiwa na
mifumo ya ikolojia wanaweza kuboresha Maisha ya watu na kukabiliana na
mabadiliko ya tabianchi.
“ Kikundi
chetu kimeanza kupanda mikoko tokea mwaka 2020 baada ya kupata mafunzo ya
upandaji kutoka taasisi ya Zaveko” amesema Katibu huyo huku akionesha hamu yake
ya kuendelea kutunza Mazingira .
Amesema
kuwa, kitendo kilichofanya na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kukata
mikoko yao zaidi ya miti 200
kimewasikitisha sana bila ya kupewa kivuja jasho.
“ Serikali
kujenga Barabara ni jambo zuri lakini
viongozi wangekuja kutuona sisi watu wa mazingira angalau kututia moyo” anasema
Katibu wao.
Mmoja wa wanachama wa kikundi hicho, Wardat Ramadhan Ali amesema vijana wamevunjika moyo ya kuendelea kupanda na kuhifadhi mikoko baada ya miti hiyo kukatwa bila ya kushirikishwa ili kupisha ujenzi wa Barabara ya Uzi Ng’ambwa
Amesema kuwa
, utafiti wa UNEP unaonesha kwamba mifumo ya ekolojia ya mikoko ina manufaa kwa
Uchumi wa kimataifa na wa ndani ya nchi kwa kusaidia sehemu za uvuvi.
Aidha amesema kuwa, mikoko inasaidia kulinda viumbe vya baharini
ikiwemo Samaki , Kamba na pia inasaidia maji ya Bahari kutokupanda juu katika
makaazi ya watu.
“ Hapa Unguja Ukuu zamani ilikuwa tukienda
baharini asubuhi baada ya maji kutoka
tulikuwa tunaokota samaki wengi lakini kutokana na mabadiliko ya tabia nchi Samaki
wamepote kabisa” anasema Wardat.
Amewataka
vijana wenzake kutokuvunjika moyo na kuendelea na harakati za upandaji wa
mikoko ili kuzuia maji ya chumvi yasipande katika makaazi yao na kutunza
mazingira.
“
Tusivunjike moyo kwa hili la kukatwa kwa mikoko ,japo imetuuma kuruhusiwa watu
kukata mikoko yetu bila ya sisi wana mazingira kupewa taarifa” anasema Wardat.
Salama Hussein
ni mwanachama wa kikundi cha Mikoko ni
Urithi wetu, amesema kuwa ujenzi wa
Daraja la Uzi Ng’ambwa lenye urefu
wa kilomita mbili na nusu, Limechangia
kwa kiasi kikubwa uharibifu wa Mazingira kwa kukatwa miti ya mikoko zaidi ya
miti 200.
Amesema kuwa, ujenzi
huo ulianza mwishoni mwa mwaka jana
ambapo Serikali iliamua kujenga
Daraja hilo , baada ya kilio cha muda mrefu cha wakaazi wa vijiji hivyo.
Amesema
kuwa, hapo awali wanakijiji cha Uzi na Ng’ambwa walikuwa wanapata shida ya kufuata huduma za kijamii
na kiuchumi masafa ya mbali.
Nae Sheha wa
shehia ya Unguja Ukuu Khamis Ibrahim
Shomari alikiri kukatwa kwa miti ya mikoko kwa kupisha ujenzi wa Barabara ya
Uzi Ng’ambwa, na kusema hilo ni jambo la Maendeleo.
Ameitaka
jamii kutokuvunjika moyo na kuendelea kupanda mikoko ili kujikinga na madhara
ya mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri
Kijiji hicho.
“ Ni wasihi
wanakijiji cha Unguja Ukuu kutokuvunjika moyo kwa kukatwa kwa mikoko ili
kupisha ujenzi wa Barabara hilo ni jambo
la maendeleo” anasema Sheha huyo.
Mahafudh
Mohamed Haji ni mwenyekiti wa Taasisi ya kutunza Mazingira na kukabiliana na
mabadiliko ya Tabianchi, amesema ni vyema wananchi waendelee kutunza Mazingira
na kupanda mikoko ili kutunza mazingira yao.
Amesema
kuwa, miti ya mikoko ina uwezo mkubwa wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi
katika vijiji ambavyo maji yanapanda.”Ni ishauri jamii iendelee kupanda
mazingira kwa kupanda mikoko kwani miti
hii ni msaada mkubwa wa kukabiliana na athari
za mabadiliko ya tabianchi” anasema Mahfudh.
Akizungumzia
kuhusu kukatwa kwa miti ya mikoko katika
eneo hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Makamo wa Kwanza wa Rais, Harous Said Suleiman alisema Serikali imelazimika kukata miti ya mikoko katika eneo
hilo ili kupisha ujenzi wa Barabara.
Amesema
kuwa, lakini baada ya kukamilika ujenzi watafanya jitihada za kuirejesha mikoko hiyo” Tutahakikisha tunashirikiana na wananchi katika kupanda tena mikoko ili kufidia miti ya mikoko iliyokatwa
na Serikali imeamua kukata mikoko hiyo, siyo kwa nia mbaya bali ni kuwajengea
Daraja wananchi na kurahisisha usafiri” amesema Waziri Harusi.
Kikundi hicho cha mikoko ni urithi wetu
kimeazishwa mwaka 2020 na mpaka sasa kimepanda miti ya mikoko 2,900,700 huku kikiwa na
wanachama 150 .
Post a Comment