“Wanawake
katika Uongozi ni chachu ya kufikia
dunia yenye usawa”
NA MARYAM NASSOR
Pili Said
Mohamed diwani wa wadi ya Mahonda wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja simulinzi yake katika harakati za
uongozi inaonesha historia ya kipekee katika safari
za wanawake wengi wenye ndoto za uongozi visiwani Unguja.
Pili ambae
alianza harakati za siasa mwaka 2020
akiwa mwanachama hai wa chama cha Mapinduzi-CCM ambaye aligombea nafasi ya
udiwani mara mbili mwaka 2020 na mwaka 2015 ndipo aliposhinda na kuwa diwani.”
Sikukata tamaa, niligombea mara mbili
nafasi ya udiwani, na mwaka ule (2015)
bahati ilikuwa upande wangu nilifanikiwa
kuupata udiwani” amesema Pili.
Pili ambae ni
mkulima na mama wa nyumbani, amesema ushiriki mdogo wa wanawake katika nafasi za uongozi zinawanyima
wanawake fursa za kushika nafasi
za juu za uongozi na vyombo vya maamuzi. “Niliingia katika siasa kuongoza kama
kielelezo. Kuhakikisha hakuna mwanamke anayeachwa nyuma. Kwa miaka yote katika
baraza letu la Madiwani, nimehakikisha masuala ya wanawake na watoto yanapewa
uzito na umuhimu sawa”
Amesema
kuwa, licha ya uhaba wao katika nafasi za uongozi lakini wakipata nafasi ya
uongozi, wanafanya vizuri ikiwemo
kutetea haki za wanawake na Watoto na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo
katika wadi zao.”Nilijiunga na siasa kwa
sababu nilitaka kufanya mambo mengi zaidi kwa ajili ya wasichana na wanawake ambao
huku kwetu vijijini tuko nyuma kimaendeleo, katika kuwawezesha wanawake
kiuchumi wachukuwe mikopo wajiendeleze kimaendeleo”
Amesema
kuwa, masuala mengi yanayohusu wanawake hayaingizwi katika sera, mipango na bajeti za Halmashauri kwani wengi wanaoshikilia nafasi za juu
za upatikanaji wa maji, uwezeshaji kiuchumi kwa
wanawake zinashikiliwa na wanaume, hivyo
ni vyema kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 wanawake wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi za uongozi ili kuongeza
ushiriki wao.
Maryam Ali
Mussa diwani wa viti maalum katika Baraza la Manispa wilaya ya Mjini Unguja , amesema ushiriki
wa wanawake katika nafasi za uongozi bado ni mdogo, na kuwataka wanawake
kuongeza ushiriki wao katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2025.
Amesema
kuwa, ni vyema wanawake wanaotaka kugombea nafasi za uongozi kujitathimini
kabla ya kugombea nafasi wanayoitaka
kugombea ili iwe rahisi kuipata” Nawashauri wanawake wenzangu wanaotaka
kugombea ni vyema kuangalia kwa makini na kujitathimini nafasi wanazotaka
kugombea ili iwe rahisi kwako
kuwahudumia wananchi watakapo chaguliwa” ameshauri diwani
huyo wa viti maalum.
Amesema kuwa, huu ndio wakati wa wanawake
kushirikiana kuelekea katika uchaguzi
mkuu ili kupeana uzoefu wa kugombea ,na kushika majimbo mengi ya uchaguzi.
Kwa mujibu
wa takwimu kutoka tume ya uchaguzi –
ZEC ya mwaka 2020 idadi ya madiwani ni 110 wanaume wakiwa 85 sawa na asilimia 77% na
wanawake 25 sawa na asilimia 23, huku
wawakilishi wanawake wa kuchaguliwa ni
wanane kati ya 50 sawa na asilimia 16.
Kwa upande wa wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wanaoiwakilisha
Zanzibar kwenye majimbo 50 ya uchaguzi ni wanne tu, sawa na asilimia nane.
Hali hiyo inaonesha, haja ya wanawake kuongezeka katika nafasi za uwakilishi katika majimbo ya uchaguzi ifikapo 2025, kwani idadi ya wawakilishi wanawake ni kidogo.
Dk Mzuri Issa ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha
Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar -TAMWA -ZNZ ambao kwa
kushirikiana na Taasisi ya Kidemokrasia
-NDI, walifanya utafiti juu ya
kujua hali ya wanawake viongozi kwenye vyama vya siasa,” Ushiriki hai wa
wanawake katika siasa mara nyingi husababisha
kuimarika kwa hali ya kijamii na
kiuchumi, kwani wanawake wana uwezo wa
kukabiliana na kupunguza umasikini ukilinganisha na wenzao wanaume”Amemaliza Dk Mzuri akiwa Ofisini kwake Tunguu Zanzibar.
Amesema
kuwa,Ipo haja kwa Serikali, asasi za kiraia na vyama vya siasa kushirikiana na
kufanya kazi kwa Pamoja ili kuondoa
vikwazo kwa wanawake ili iwe rahisi kwao
kugombeea nafasi za uongozi, huku akiona
utekelezaji wa mikataba na matamko mbali mbali ya kikanda na kimataifa ya
kuhamasisha usawa wa kijinsia bado utekelezaji wake haujafikiwa.
Kwa mujibu
wa ripoti ya sensa ya watu na makazi ya
Tanzania ya mwaka 2022, inaonesha kuwa
Zanzibar ina wakazi wapao milioni 1.8 kati ya hao wanaume ni 915,492 na wanawake ni
974, 281.
Hii ina
maana kwamba, wanawake ni asilimia 51.6 ya wakaazi wote wa Zanzibar, lakini wingi wao huo hauonekani
katika nafasi za uongozi.
Abdulrazak
Said Ali mwanasheria kutoka Ofisi ya msajii wa vyama vya Siasa Zanzibar
,amesema kuongezwa kwa kifungu cha 10 C
katika sheria ya vyama vya siasa nchini
itasaidia kuongeza kwa ushiriki wa wanawake kwani sheria hiyo inavitaka vyama
vya siasa kuwa na sheria ya jinsia kwa muda wote” Lengo la kuongeza kwa kifungu
hichi katika sheria ya vyama vya siasa
nchini ni kuongeza ushiriki wa wanawake
kwa kuwa na sera ya jinsia kwa
muda wote” amesema mwanasheria huyo.
MWISHO
Post a Comment