VITI MAALUM VINAVYOWALEMAZA WANAWAKE KUGOMBEA MAJIMBONI.
NA MARYAM
NASSOR
VITI Maalumu vya wanawake ni nafasi
zinazotolewa na Serikali kwa lengo la
kuongeza idadi ya wanawake katika bunge na Baraza la Wawakilishi Zanzibar,
ingawa utaratibu huo hutumiwa na nchi
mbali mbali duniani katika siasa, kwa lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake
katika nafasi za uongozi.
Uwakilishi
wa wanawake kupitia viti maalumu, sio wa kudumu ni nafasi za kujiandaa kisiasa,
Pamoja na kuandaa mbinu za kupata ushindi wanapokwenda jimboni ili iwe rahisi kwao kushinda na kuwatumikia wananchi.
Lakini
kinachotokezea kwa baadhi ya wanawake wanaopata nafasi hizo,wanahudumu kwa muda mrefu, tofauti na malengo yake na kuwalemaza kwa hofu ya kuingia
majimboni.
Asya
Mohamed, ni mbunge wa viti maalum Mkoa wa Kaskazini Unguja kupitia chama cha Demokrasia na
Maendeleo -CHADEMA amesema ni kweli viti maalum vinawalemaza baadhi ya wanawake
wanaopata nafasi hizo.
Amesema
kuwa, vyama haviwazuii pia kuendelea kugombea nafasi hizo, kwani hakuna sheria
maalum iliyoweka ukomo wa viti maalum wa muda wa kugombea ni wewe mwenyewe na
uwamuzi wako.” Lakini ni vyema kukaa miaka mitano tu inatosha kujipanda na
kujiandaa kwenda jimboni kwani na wengine wanataka nafasi hizo ili kujifunza”
ameshauri mbunge huyo.
Ameeleza
kuwa, ni vyema ukawekwa ukomo na
sheria maalumu inayowataka wagombea wa
nafasi hizo, kukaa kipindi kimoja tu ili
nafasi hizo, zisiwalemaze
wanawake na badala yake wazitumie kwa kujifunza siasa na kugombea
majimboni.
Kwa mujibu
wa takwimu kutoka baraza la wawakilishi Zanzibar (BLW) idadi
ya wajumbe wote ni 78 kati yao wanawake ni 29 na wanaume 48, huku
wanawake wawakilishi wa majimbo kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ni wanne
tu, wanaume wakiwa 42 na wanawake wa viti maalum ni 18 na wajumbe waliobakia ni
nafasi za kuteuliwa na Rais.
Fatma Abdul
habib Ferej Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, amesema kuwa wanawake wengi wanaochaguliwa katika nafasi
za viti maalumu, wanaenda kinyume na
dhamira ya kuanzishwa kwa nafasi hizo, kwa kudumu kwa muda mrefu.”Wapo wanawake
wanaong’ang’ania nafasi za viti maalumu kwa miaka mingi , japo uwezo wao
unaruhu Kwenda jimboni kugombea na kujilemaza kisiasa” amesema mwenyekiti huyo.
Amesema
kuwa, ni vizuri kuwekwa sheria ya ukomo
wa nafasi za viti maalum, kwani ipo haja kwa wanawake kuingia kwenye majimbo
kugombea ili kuongeza wingi wao.
Ameeleza
kuwa, wapo wanawake ambao ni mfano mzuri
wa kijifunza kutoka kwao, ni Rais Samia ambae alikaa kwa kipindi kimoja tu katika nafasi za viti maalum na kijitupa
jimboni katika jimbo la Makunduchi mkoa wa Kusini Unguja.
Mwakilishi
wa jimbo la Mahonda, Wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja Asha Abdalla Mussa amesema kuwa, hakupita kwenye viti maalum alitoka
kwenye nafasi ya udiwani na kujitupa
jimboni,” Wanawake tukiamua tunaweza ni vizuri kuwa na uthubutu na kujiamini na utafanikiwa” Amesema
Mwakilishi huyo huku akiwasihi wanawake mwaka 2025 kuchangamkia fursa za
majimboni na wakikosa watarudi kwenye viti maalum.
Mkurugenzi wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake
Tanzania Zanzibar -TAMWA ZNZ, amesema ni kweli vyama vya siasa haviwasaidii
wanawake kuondokana na viti maalumu.’’
Kuna mtu utamkuta yupo anagombea kiti maalumu miaka mitano hii na mingine na bado
yupo hapo hapo wakati inatakiwa mtu akae miaka mitano ajifunze kisha atokee
aende jimboni akagombee” ameshauri Dk Mzuri.
Amesema
kuwa, kutokana na hali hiyo ipo haja ya wanawake kuongezeka katika nafasi
za uwakilishi katika majimbo ya uchaguzi ifikapo 2025 kwani idadi ya viongozi wanawake wa kuteuliwa ni ndogo sana.
Ripoti ya sensa ya watu na makaazi ya Tanzania ya mwaka
2022, inaonesha kuwa Zanzibar ina
wakaazi milioni 1.8 kati ya hao wanaume
ni 915,492 na wanawake ni 974,281.hii ina maana kwamba wanawake ni asilimia 51.6 ya wakaazi wote wa
Zanzibar, lakini wingi huo hauonekani katika nafasi za uongozi.
Mchambuzi wa Masuala ya uongozi na
Siasa Visiwani Zanzibar , Almasi Mohamed
amesema kuwa,wanawake wengi wanaohudumu nafasi za viti maalumu wanajisahau na
kubaki kwa kipindi kirefu katika nafasi hizo kinyume na malengo yake.” Uhaba wa
wanawake katika majimbo bado unaendelea
kutokana na wale ambao, wanajifunza siasa kupitia nafasi za viti maalum , ni
vyema mwaka 2025 wakajitupa majimboni
kugombea ili kuongeza wingi wao” ameshauri Mchambuzi huyo.
Amesema kuwa, ipo haja kwa
wanawake waliopitia katika viti maalum
kuonesha uthubutu wao kugombea katika majimbo mwaka 2025 ili kuongeza wingi wao katika nafasi za
uongozi na vyombo vya maamuzi.
Post a Comment