MABADILIKO YA MITAZAMO YA WANAJAMII KATIKA SIASA


NA THUWAIBA HABIB

Ripoti ya  mwaka 2021 iliyopewa jina la wanawake bungeni  iliyochapishwa na wanawake wa wabunge dunia, ilionesha Rwanda ndio nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya wanawake serikalini  ambapo 63.8% ya wabunge na viti 13 vya uwaziri kati ya 32 vya mawaziri viliopo sasa vimekaliwa na wanawake.

Idadi hiyo imemuhamashisha Mosi Haji Ushahidi mkaazi wa kijiji cha Kikungwi  kuona  kuwa upo uwezo wanawake wengi kugombea nafasi za uongozi na kuhamasisha wanawake wenziwe kuingia pia ili kufikia asilimia kubwa ya  kina mama wenye kuleta maendeleo.

Mosi ni mama watoto watano ,56 amesema kwa kweli huu sio tena wakati wa kurejeshwa nyuma wanawake kwa kutumia kasumba ya kuona mwanamke hawezi kuongoza. Ni wakati wa kuendelea na safari ili wanawake  wawe kama wanaume na kuwa na  haki sawa ya kugombea uongozi

"Ni lazima wanawake tuwe wamoja na kushikana mikono linapokuja suala na kugombea  nafasi za Uongozi ."

Jambo muhimu ni wanajamii kutokubaguana kijinsia na badala yake waende sawia katika uongozi wa nchi yetu.Hapa inafaa kukumbushana kwamba mwanamke ni mwalimu, mtu mwenye ujasiri, hekima na busra na sio vyema kudharau sifa hizi panapokuja suala la uongozi

"Kila mwanamke anatakiwa kutodharau mwenziwe na kuwa pamoja kwa anacho kifanya kwani tunaujasiri mkubwa katika masuala mbali mbali"

Mama huyu aliwataka wanawake  wenziwe kujiamini na kuhakikisha wanatekeleza  majukumu yao kwa usahihi na vizuri wanapokwama ukataka ushauri. na kujitoa kuwania  nafasi zilizopo katika siasa  ifikapo 2025 njia hiyo itawafanya watu wote  waelewe uwepo wako.

‘’Ukiwa mtaani unapata maneno mengi yanayovunja moyo ya kuwa hutoweza kuongoza muhimu ni kushikilia malengo yako tu’’, aliongeza.

 Katibu wa wadi ya Bungi  Wilaya ya Kusini Unguja Kassim Makame Kombo, 42  amesema  mimi ni miongoni mwa mwanaume ambaye nahamasisha wanawake kuingia katika  nafasi za uongozi  na hata kuhakikisha nawasaidia katika kipindi chao cha kampeni kwani  nimegundua kuwa wana uwezo mkubwa  na niwapambania "Wanawake wana uwezo mkubwa wa kutuongoza kwa hutumia juhudi kubwa kuhakikisha mafanikio yanapatikana"

Amesema  sisi wanaume tupo katika  matabaka tofauti baadhi yetu wanakuwa ni wagumu kutoa fursa kwa wanawake kuingia katika siasa  kutokana na sababu  mbali mbali kama kufanyiwa udhalilishaji  na mengine yanayoshusha heshima kwani vitu hivyo huweza fanyiwa mtu yoyote muhimu kujielewa nini wanawataka tu.

"Wanaume tutowe fursa kwa wanawake kugombea nafasi za uongozi kwa mtu yoyote awe mwanaume au mwanamke anaweza kufanyiwa udhalilishaji kama haelewi ni anataka"

Katibu  wa Siasa Itikadi na Uenezi katika Wadi ya Kijitoupele, Riziki Abdallah Ali,  amesema kwa mtazamo wake muda  umefika wa kuwawezesha wanawake wengine kuingia katika uongozi na hususa vijana wa kuanzia miaka 15 ili watoe mchango wa kuijenga nchi.

Amesema kila mwanamke awe na uchungu  na mwanamke mwenziwe kuhakikisha anashinda katika uchaguzi ambao umetukabili mwakani kwa ni muhimu kupata watetezi wengi wa kike ‘’Sasa woga wa wanawake kugombea umepungua na tunaahidi kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali katika uchaguzi wa mwaka 2025.alieleza  riziki

Kwa kuwa wanajamii nyingi hufuata miongozo ya dini  na ndio nguzo ambayo wengi hutumia katika kutolea maamuzi.

Mmoja wa wanazuoni maarufu wa elimu ya dini ya Kiislamu, Profesa Issa Haji Zidi,  alipofafanua kwa undani kwamba  dini ya Kiislamu haijakataza mwanamke kuwa kiongozi wala kuwawekea vikwazo.

"Dini ya kiislamu hajakataza mwanamke kuwa kiongozi wa kumuwekea vikwazo bali inamtaka afuate msingi ya dini katika uongozi wake"

Profesa Zidi ameeleza  kwa undani kwamba katika enzi ya Mtume Muhammad (SAW) walikuwepo wanawake waliokuwa viongozi katika vita na mambo mengine na kote huko yalipatikana mafanikio chini ya uongozi wao.

"Wapo wanawake walioweza kushiriki jatika vita jwa ajili ya kutetea dini ya kiislamu"

Alitoa mfano wa  Bi Nasiba  binti Kaabu  kuwa ni   mmoja wa walinzi majasiri wa Mtume (SAW)  katika vita vya Uhud na kuhakikisha mtume anakuwa salama na alijeruhiwa  takribani mara 11.

Kwa mijibu wa ripoti ya sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 imeeleza kuwa Zanzibar ina watu 1,889,773 kati ya hao wanaumme ni 915 ,492 na wanawake ni 974 ,281 hii ina manisha kwamba wanawake  ni asilimia 51.6ya wakaazi wote Zanzibar.

 Asilimia hiyo iliyokuwepo inatakiwa kushika  hatamu ya uongozi ifika 2025 kwani uwezekano huo upo endapo wanawake watashirikiana na kuungana mikono katika kuhakikisha wanakuwa katika ngazi za maamuzi.

Mkurugenzi wa wa chama cha waandishi wa habari  wanawake Zanzibar _Tanzania  Tamwa Dkt Mzuri Issa Ali amesema wanachukua hatua za kuwasaidia wanawake kushiriki katika uongozi

Hii ni pamoja na kutoa elimu ya kujitambua, kujielewa na kuthubutu kuwa wagombea huku wakizijuwa haki zao za kidemokrasia.

Na tunatoa elimu ya na namna ya kujilinda na rushwa na kujuwa sheria za uchaguzi zinavyowalinda wanapokuwa katika harakati za kugombea uongozi

 Vijana huunganishwa na wanasiasa wakongwe ili kupata uzoefu na kuhamasika kuchukua nafasi za uongozi.

wanazopambana nazo ni pamoja na kuitaka jamii ikubali mwanamke anao uwezo wa kuongoza  na kuachana na mila na desturi zinazomkwamisha mwanamke kupata nafasi ya kuongoza wenzake

Kwa sasa tumepunguza matatizo yanayomkatisha tamaa mwanamke asijitokeze mbele kugombea uongozi.Jambo muhimu ni kuondoa hofu na kujichanganya na watu wote ili uwezo wao uonekane

"Tumeweza kupunguza matatizo yanayokwamisha wanawake wasijitokeze kugombea jambo lilibaki ni wao kuondoa hofu tu ili kushikilia nafasi hizo".

Aidha Dira ya Zanzibar ya 2050 imeelezea jinsi gani masuala ya usawa wa jinsia juu ya kuondoa unyanyasaji na kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake, ikiwa pamoja na kuinua na kutoa nafasi za uongozi kwa wanawake.

Vile vile imelenga kuongeza fursa na kuwawezesha katika vyombo vya kutoa maamuzi na kwenye shughuli za uchumi, kijamii, siasa, ngazi za utawala na huduma za sheria.

 

Naibu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Zanzibar,  Anna Atanas Paul amesema wizara hiyo itaendelea kuhamasisha wanawake kugombania nafasi mbali mbali za uongozi wa kuchaguliwa ili ifikapo 2025 wafikie asilimia  sawa 50 kwa 50.

Aidha amesema nafasi za viti maalumu kwa wanawake ziondolewe badala yake nafasi hizo wapewe watu wenye mahitaji maalumu kwani katika zama hizi wanawake wa Tanzania wameshathibitisha kwa vitendo kwamba wanaweza kugombea majimboni na kushinda na kuongoza kwa ubora wa kiwango cha juu.

 "Chama Cha Mapinduzi na vyama vya upinzani vimethibitisha kupitia chaguzi zilizopita kwamba wakiteuwa wanawake kugombea wengi wao wanachaguliwa na kushinda", alieleza.

 Katibu Uenezi Chama cha ACT Wazalendo Halima Ibrahim Mohammed  ameeleza kuwa wanawake wamejitahidi kuchukua jitihada kubwa ya kushikana mikono, kwa kuthibitisha hilo uchaguzi ujao wameandaa kampeni ya kumnyanyua mwanamke, awemo katika ngazi za maamuzi, kamati kuu na halmashauri juu.

Uchaguzi wa mwaka 2020, mchakato wa kuwania nafasi za uongozi majimboni kwa wanawake ulihamasika na kufikia takriban wanawake 400 waliojitokeza kwenye vyama mbalimbali vya siasa vyenye ushindani mkubwa,

 

No comments

Powered by Blogger.