Millioni 150,000 zatumika katika ununuzi wa vifaa vya Miundombinu ya Maji.

 

 NAMARYAM NASSOR,

Jumla ya shilingi million 150,000 za kitanzania zimetumika kununua vifaa vya mindombinu ya maji, Kwa wanufaika wa kilimo mseto, ili kulima na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

 Akikabidhi vifaa hivyo,  Kwa wanufaika wa mradi ,Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya ugawaji  huko katika kisiwa Cha Uzii  Ng'ambwa, Mkuu wa mkoa wa Kusini Unguja, Ayoub Mohamed Mahmoud, alivitaja vijiji hivyo  , ni Uzii Ng'ambwa, Bungi na Unguja Ukuu.

Mkuu wa Mkoa huyo,amewataka  wanufaika wa mradi wa ZanzAdapt kuvitunza vifaa hivyo, ili vitumike kama ilivyokusudiwa.

 


Aidha , amewashukuru Jumuiya ya Community Forest Pemba(CFP) Kwa kujitoa kuwasaidia wananchi wa Kisiwa hicho na kuwataka Taasisi nyengine kuiga moyo wa kuzalendo walionao.

" Napenda kuishukuru Kwa dhati, Jumuiya ya Community Forest Pemba Kwa kusaidia kutekeleza sera za Wizara ya Kilimo " amesema .

 Amesema kuwa, Serikali ya zanzibar kupitia Wizara ya Kilimo na Umwagiliaji inataka wakulima kulima, kilimo biashara ambacho kitakuza kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa Kwa ujumla.

Nae, Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo, Mbarouk Mussa Omar, amewataka wananchi wa kisiwa Cha Uzii , Ng'ambwa, Bungi na Unguja Ukuu  kuvitumia vifaa hivyo, kama ilivyokusudiwa.

 


Amesema kuwa, lengo la mradi wa ZanzAdapt ni kuwawezesha wanawake  Kwa kuwapa mafunzo na Miche ya miti mbali mbali, ili kulima na kuinua vipato vyao kiuchumi.

 Amesema kuwa, vifaa hivyo walivyotowa Kwa wanavikundi hao,  washiriki wakuu ni wanawake ambao ni asilimia 80 ya washiriki wa mradi huo.


 "Niwaombe  sana muvitunze hivi, vifaa mulivyopewa ili viishii Kwa muda mrefu na vitumike kama ilivyokusudiwa" amesema Mkurugenzi Mbarouk.

 Nao, wanufaika wa mradi wa ZanzAdapt Kutoka Shehia ya Uzii, Khadija Hassan Othman, amewashukuru  Jumuiya ya Community Forest Pemba, Kwa kuwasaidia vifaa hivyo kwani walikuwa wanalima lakini hawana mategemeo ya kuvuna.

 



Amesema kuwa, kutokana na Mabadiliko ya Tabianchi walikuwa , hawapati kitu kwenye kilimo kutokana na kuingiliwa na maji ya chumvi katika mashamba yao. 

Mradi huo,wa Mabadiliko ya Tabianchi (ZanzAdapt) unatekelezwa na Shirika la Misitu Duniani (CFI) chama Cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA ZNZ) na Jumuiya ya Community Forest Pemba (CFP)  na unatekelezwa katika shehia nane Kwa Unguja na Pemba.

 

No comments

Powered by Blogger.