TAMWA ZNZ, YATAKA ADHABU KALI KWA WATU WANAO WADHALILISHA WATOTO
NA MARYAM NASSOR
CHAMA cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar,(TAMWA ZNZ)
kimeonya kuhusu hali ya kukithiri vitendo vya udhalilishaji dhidi ya
watoto na kuomba hatua kali za kisheria
kuchukuliwa dhidi ya wahalifu.
TAMWA ZNZ, Imeeleza kuwa ripoti ya hivi karibuni
kutoka Ofisi ya mtakwimu mkuu wa Serikali Zanzibar inaonesha matukio 165 ya
ukatili wa kijinsia yaliyoripotiwa mwezi julai2024, ambapo watoto walikuwa
wathirika wakubwa.
Katika ripoti hiyo, watoto walihesabiwa kuwa ni 142,
sawa na asilimia 86.1 ya wathirika waote, huku wasichana wakiwa 115( asilimia
81.0) na wavulana 27 ( asilimia 19.0) TAMWA ZNZ, imesema hali hii inahitaji
udhibiti mkali kutoka kwa wadau wote ikiwa ni pamoja na Serikali , taasisi za
kijamii, wazee na watoto wenyewe.
''Tunaona hali hii ni mbaya na ya kusikitisha na inahitaji kudhibitiwa
kwa nguvu zote, wasimamizi wa watoto wanapaswa kuhakikisha haki za watoto
zinazingatiwa na adhabu kali zinachukuliwa dhidi ya wahalifu wa vitendo vya ukatili kwa mujibu wa sheria''
wameeleza TAMWA ZNZ.
TAMWA ZNZ, pia imetolea mfano wa tukio la hivi
karibuni ambapo mtoto wa miaka miwili alikamatwa pamoja na mlezi wake na
watendaji wa Manispa ya Magharibi 'A' kwa kisingizio cha wazazi wake kutolipa
ada ya usafi.
'' Kitendo hiki kilizua taharuki kwa famila ya mtoto
na jamii kwa ujumla, na kimenda kinyume na haki za mtoto pamoja na haki za
binaadamu'' wamesema TAMWA ZNZ.
Sheria ya mtoto ya
Zanzibar Na 6 ya mwaka2011 inapinga udhalilishaji wa watoto wa aina
yoyote ile, ili kukuza ustawi wao, aidha mkataba wa kimataifa wa haki za
watoto(UNCRC) wa mwaka 1989, ambao Tanzania na Zanzibar wameuridhia ,
umesisitiza kulinda haki za watoto.
'' Tunatoa wito kwa jamii kuwalinda watoto wetu na
pia kuhakikisha hawakumbwi na vitendo
vya udhalilishaji, ni jukumu letu sote
kulinda haki za watoto na
kuhakikisha wanakuwa katika
mazingira salama '' walisema TAMWAZNZ.
MWISHO
.jpeg)
Post a Comment