MWENYEKITI WA ACT WAZALENDO TAIFA AMESEMA, MAMLAKA YA KUENDESHA NCHI NI YA WANANCHI WENYEWE



NA MARYAM NASSOR,

MAKAMO wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, ambae pia ni mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo taifa, Othman Massoud Othman amesema mamlaka ya kuendesha nchi ni ya wananchi ambapo nguvu na uwezo wa Serikali kufuata katiba, unatokana  na wananchi wenyewe.

Amesema hayo huko katika hotel ya Golden Tulip Kiembesamaki Unguja alipokuwa akiwatangaza mawaziri wa kisekta  16(Mawaziri Kivuli)  manaibu waziri pamoja na  wizara zao.

 Alisema kuwa, lengo la kuteuwa mawaziri hao ni kuangalia utendaji wa Serikali , kisera na kisheria juu ya kuwaletea wananchii maendeleo kwa kuishauri Serikali.

Amesema kuwa, hatua hiyo imekuja kutokana  na maagizo ya halmashauri kuu ya chama hicho,kuamua kuanzisha  mabaraza hayo, kutokana na uzoefu waliyoupata  katika baraza kivuli la mawaziri kule Tanzania bara na kuona ipo haja kuamua kuanzisha hapa Zanzibar baada ya kushauriana na wenzake.

Aidha mwenyekiti huyo, amesema kuwa kifungu cha 10 cha katiba ya chama  chao kimeweka bayana  malengo muhimu ya kisiasa na nchi, miongoni mwa malengo hayo ni kuondoa kabisa vitendo vya rushwa na utumiaji mbaya wa cheo kwa viongozi waliyokuwepo madarakani.

Alieleza kuwa, ibara ya 7 ya  katiba ya chama cha Act Wazalendo inaeleza malengo na madhumuni ya chama hicho, ambayo inakiambia chama kupigania takribani malengo yote, yaliyoainishwa katika katiba ya Zanzibar katika kazi zake za kuwa sauti kwa wananchi.

Nao baadhi ya Mawaziri  na manaibu wao,walioteuliwa  ni pamoja na  Profesa Ibrahim Fakih waziri wa Fedha na Halfan Amour Mohamed waziri wa katiba na sheria, wameishuku kamati kuu ya Act Wazalendo kwa kuwapa  fursa hiyo, na kuwahidi  hakika wataitendea haki kwa kuwatumikia wananchi.

 Nao baadhi ya wandishi wa habari waliopata nafasi ya kuuliza maswali walihoji, ni kwanini wamemteuwa waziri mmoja mwanamke au hakuna wanawake  wenye uwezo wa kuongoza katika chama hicho .

Akijibu maswali ya wandishi wa habari, mwenyekiti wa chama hicho Othma Massoud Othaman alisema, wamezingatia uwiano wa jinsia kwa kuteuwa manaibu mawaziri wengi wanawake.

                                 MWISHO

No comments

Powered by Blogger.