Mbunge wa Viti Maalum Zanzibar aunga Mkono Juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan

 NA MARYAM NASSOR    


MBUNGE wa viti maalum Zanzibar  Bi Asya Mwadini Mohammed, amewataka wananchi wa Jimbo la Kijini Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja, kuokoa maisha yao kwa kutumia nishati safi ya kupikia ambayo, itawaepusha na Athari katika mfumo wa upumuaji na kutunza mazingira.

Ameyasema hayo, huko Kijini Matemwe alipokuwa akigawa Majiko  ya gesi ya kupikia kwa wananchi wa jimbo hilo, yenye lengo la kumuunga mkono jitihada za Raisi Samia Suluhu Hassan,katika kampen yake ya  kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema Kuwa, matumizi ya nishati  safi ya kupikia, itawasaidia wanawake kutumia muda mwingi katika kufanya shughuli za kiuchumi na maendeleo, kutokana na Kuwa matumizi  ya gesi ni rahisi na yaana ukoamuda.




Amewataka wananchi hao, kuanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa ujumla,  kwani yataondoa uharibifu  wa mazingira ambapo, Jamii itaachana na ukataji wa miti ovyo,  na kumuondolea mwanamke adhaa ya   kutumia  muda mwingi katika kutafuta Kuni.

"Matumizi  ya nishati safi ya kupikia,  yatawasaidia kutumi muda mwingi  katika kufanya shughuli za kiuchumi, kwani matumizi  ya majiko ya haya ni rahisi na yanaokoa muda"alisema.

Aidha mbunge huyo,  aliwataka wananchi hao kuwa mabalozi wazuri  katika kumuunga mkono Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan ,katika kampeni yake ya matumizi  ya nishati  safi ya kupikia.

Nae, mwananchi  wa shehia iyo, Patima Mwepo Juma amemshukuru mbunge huyo kwa kuwajali  afya zao,na kuwapa majiko hayo  ya gesi ya kupikia na kuahidi  kuanzia sasa  watakuwa balozi wazuri wa kuhamasisha  matumizi ya nishati  safi.







"Kwa kweli mimi sijawahi kutumia  nishati safi ya gesi kwa kupikia, lakin kuanzia  Leo nitaanza kupikia" amesema.

Mwananchi Khadija Simai Makame, amemshukuru mbunge huyo kwa kuwapa majiko hayo ya gesi, na kuwapa elimu ya matumizi  ya majiko hayo.

Awali mbunge huyo, mara baada ya kuwapa majiko hayo  wananchi hao,aliwapa elimu ya matumizi  sahihi  ya majiko hayo ya gesi.

Zaidi ya majiko hamsini yametolewa na mbunge  huyo, ikiwa ni muendelezo wake katika mkakatiti wa matumizi  ya nishati  safi ya kupikia, iliyozinduliwa na Raisi Samia Suluhu Hassan  Mei 8, 2024 ikilenga  kuepuka athari  za kuni na mkaa,  unaoambatana na utunzaji wa mazingira. 





No comments

Powered by Blogger.