WANDISHI WA HABARI WAPIKWA KUWA MABALOZI WAZURI KUELIMISHA JAMII USAWA WA KIJINSIA WANAWAKE NA UONGOZI
NA MARYAM
NASSOR CHAMA
cha wandishi wa habari wanawake Zanzibar, (TAMWA ZNZ) kimewataka wandishi wa
habari vijana kuwa mabalozi wazuri katika kushajihisha usawa wa kijinsia katika uongozi kwa maendeleo
ya nchi kwa ujumla.
Akifungua
mafunzo ya siku tano , mkurugenzi wa chama hicho Dk Mzuri Issa Ali alisema kuwa vijana wa kiume wana nafasi kubwa ya kufanya
uchechemuzi kusaidia wanawake kuingia katika maswali ya uongozi.
Alisema kuwa
awamu hii vijana wa kiume wamepewa nafasi kubwa, ukilinganisha na awamu iliyopita, lengo la mradi huo ni kuona
ongezeko kubwa la washiriki wanawake katika nafasi za uongozi.
“ Vijana wa
kiume haikuwa bahati mbaya kuchaguliwa
katika mafunzo haya, bali tumefanya hivyo kwa kuwajenga kuwa mashujaa, mabalozi
na wanaume wa mabadiliko katika kuhamasisha usawa wa kijinsia’’ alisema.
Aidha DK Mzuri
alisema kuwa wamechaguwa vijana
wenye taaluma mbali mbali ikiwemo wandishi wa habari, wandaaji na
waongozaji wa filamu ambao wanaamini watasaidia kuelimisha jamii kuhusu maswala
ya usawa wa kijinsia na wanawake kushiriki katika vyombo vya maamuzi.
Nao baadhi ya wandishi wa habari walioshiriki katika mafunzo hayo, wameishukuru TAMWA ZNZ, kwa kuwapa mafunzo hayo kwani yatawasaidia kuzidi kutoa elimu na kuelimisha jamii na wanawake kuingia kwenye uongozi.
Nae mkufunzi
Najjat Omar aliwataka washiriki wa mafunzo hayo, kutumia takwimu katika kuandika Makala zao
ili kuonesha hali halisi ya wanawake wangapi ambao wako katika uongozi .
Nae mshiriki Zurima Ramadhani kutoka radio asalam fm aliahidi kufanya kazi kwa bidii na kuzidi kuelimisha wanawake kuingia katika uongozi.
Chama cha
wandishi wa habari wanawake Zanzibar TAMWA ZNZ imeandaa mafunzo kwa wandishi wa habari vijana 25 Unguja na Pemba , ambapo wanawake jumla ni 15 na wanaume 10 kwa
kushirikiana na shirika na ( NED) la nchini marekani.
MWISHO
Post a Comment