MZEE WA MIAKA 50 APANDISHWA KIZIMBANI KWA KOSA LA KULAWITI MVULANA WA MIAKA 17



NA MARYAM NASSOR

MAHAKAMA ya Mkoa Mahonda imempandisha  kizimbani mzee Alfred Barnabas Mbogo (50) wa Kinduni Unguja kwa kosa  la kulawiti mtoto wa kiume  mwenye  umri wa miaka (17).

 Mara baada ya kufika Mahakamni hapo akitokea rumande mshtakiwa huyo,alisomewa shitaka lake hilo na mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar , Hariri Yeshau Ali mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Luciano Makoe Nyengo.

Mara baada ya kusomewa shitaka lake hilo mtuhumiwa huyo, alikana kosa hilo .

 Mwendesha mashtaka, alidai kuwa kesi hiyo leo ipo kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa kesi hiyo imeshakamilika na kumuomba hakimu wa mahakama hiyo kuihairisha na kuipanga siku nyengine kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa mashahidi.

‘’ Muheshimiwa hakimu leo kesi hii ipo kwa ajili ya kutajwa na Ushahidi wa kesi hii umeshakamilika hivyo, tunaomba uipange siku nyengine kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa mashahidi’’ alidai Dpp huyo.

Awali mahakamani hapo dpp Hariri alidai kuwa, mtuhumiwa huyo anashtakiwa kwa makosa mawili kosa la kwanza ni kumlawiti kijana wa kiume miaka (17) kinyume na kifungu cha 115(1)  vya sheria ya adhabu sheria namba 6 ya mwaka 2018 sheria za Zanzibar.

 Na kosa la pili ni kutorosha  mvulana ambapo ilidaiwa kuwa siku ya august 12 mwaka huu,  majira ya saa moja usiku  huko kinduni , wilaya ya Kaskazini ‘B’ Unguja  bila ya halali alimchukuwa mvulana wa miaka (17)  kutoka nyumbani kwao kinduni na kumpeleka kichakani , na kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu  cha 133(1) (b) vya sheria ya adhabu  namba 6 ya mwaka 2018.

Hakimu wa mahakama hiyo, alihairisha kesi hiyo hadi Septemba 9 mwaka huu kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa mashahidi.

                     MWISHO

No comments

Powered by Blogger.