MKE NA MUUME WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA KUPATIKANA NA MIRUNGI

 

 


                               

NA MARYAM NASSOR

MAHAKAMA  Kuu Zanzibar iliyopo Tunguu Unguja imewapandisha kizimbani watuhumiwa wawili  ambao ni mke na mume kwa kesi ya kupatikana na dawa za kulevya aina ya mirungi  vicha 35 vyenye uzito wa  kilo 3.851 .

 Watuhumiwa hao, ambao ni mke na mume  ambao ni Nassor  Aman Ismail(41) na Zeyana  Khamis Mohamed(39)wote  wakaanzi wa meli nne taveta Unguja.

Wakisomewa shitaka lao hilo na mwendesha mashtaka kutoka Afisi ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar Dpp Ali Amour mbele ya Jaji wa Mahkama hiyo Mohamed Ali Mohamed,  alidai kuwa watuhumiwa hao walipatikana  na dawa zinazodaiwa kuwa ni za kulevya aina ya mirungi wakiwa ndani ya nyumba yao wanayoishi.

 Mara baada ya kusomewa shitaka lao watuhumiwa hao, walikana shitaka lao hilo na kuiomba mahkama  wapatiwe dhamana  ombi ambalo lilikataliwa.

Awali mahkamani hapo ilidaiwa na mwendesha mashtaka wa Serikali, kutenda kosa hilo disemba  21 mwaka 2023 majira ya saa11:30 jioni huko maeneo ya meli nneTaveta  wilaya ya magharibi ‘B’ Unguja wote kwa pamoja  wakiwa ndani ya nyumba yenye namba  SH/TV/ZH/08  bila ya halali  walipatikana na vicha 35 vya majani  ambayo yanadaiwa kuwa ni dawa za kulevya aina ya mirungi  yenye uzito wa  kilo 3.851 .

Wakili huyo alidai kuwa, kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha  21 (1) (d) cha sheria  ya mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevy a, sheria namba 8 ya  mwaka 2012 sheria za Zanzibar.

 Jaji wa mahkama hiyo, aliihairisha kesi hiyo hadi august 28 mwaka huu kwa kuanza kusikilizwa kwa mashahidi.

No comments

Powered by Blogger.