MAYELE AHUKUMIWA MIAKA 14 JELA KWA KOSA LA KULAWITI MTOTO WA KIUME MIAKA 12



NA MARYAM NASSOR

MAHAKAMA   maalum ya makosa ya  Udhalilishaji mkoa  Mahonda Imemuhukumu Kijana Sharif Juma Hamad  (33) maarufu kwa jina la 'MAYELE' wa Mzambarau mbata Unguja,  kutumikia kifungo cha  miaka 14 jela kwa kukutwa na hatia ya makosa mawili ya Udhalilishaji.

Akisoma hukumu hiyo,Hakimu Luciano makoe nyengo alisema kuwa mshitakiwa huyo amekutwa na hatia hiyo baada ya Mahakama kujiridhisha  na Ushahidi uliyoletwa na Upande wa Mashtaka uliyoongozwa na Mwendesha Mashtaka Hariri Yeshau Ali, na vielelezo vilivyowasilishwa  Mahakamani hapo,

Hakimu Luciano , alisema kuwa Mshitakiwa huyo anatiwa hatiani kwa Makosa mawili  aliyoshitakiwa nayo, kosa la kwanza ni Kulawiti mtoto wa kiume  mwenye miaka 12, kwa kosa hilo atatumikia Kifungo cha maiaka 14 jela.

Kosa la pili, ni kutorosha mtoto wa kiume alie chini wa uwangalizi wa wazazi wake kinyume na kifungu cha 113 (1) (b) cha sheria namba 6 ya mwaka 2018 sheria za Zanzibar. na  kosa hilo atatumikia kifungo cha miaka 10 jela .

Aidha, Hakimu Luciano alisema kuwa adhabu zote hizo ziende sambamba hivyo mshitakiwa huyo atatumikia kifungo cha miaka 14 chuo cha mafunzo.

 kesi hiyo,  yenye namba 18 ilifunguliwa tarehe 11/6/2024 na kusikilizwa mashahidi sita na upande wa utetezi kulikuwa na shahidi mmoja ambae ni mshtakiwa.

Awali mshtakiwa huyo, alishtakiwa kwa makosa mawili kosa la kwanza likiwa ni kulawiti mtoto wa kiume  mwenye umri wa miaka 12 kinyume na kifungu  cha 115(1) vya sheria ya adhabu  namba 6 ya mwaka 2018 sheria za Zanzibar.

 Na kosa la pili ni kumtorosha mtoto wa kiume aliye chini  ya uangalizi wa wazazi wake,  kutoka nyumbani kwao mgambo na kumpeleka nyumbani kwa mshtakiwa  huko huko mgambo bila ya ridhaa ya wazazi wake na kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu  cha 113 (1) (b) cha sheria namba 6 ya mwaka  2018 sheria za Zanzibar .

 

                                         MWISHO

 

                   

No comments

Powered by Blogger.