KESI YA RAIA WA UGANDA ALIYEINGIZA KETE 38 ZA MADAWA YA KULEVYA ZNZ,IMEENDELEA KUHAIRISHWA MAHAKAMA KUU TUNGUU ZANZIBAR



NA MARYAM NASSOR

KESI ya raia wa Uganda  anayekabiliwa na shitaka la kuingiza madawa ya kulevya nchini  aina ya Cocaine kete 38 zenye uzito wa gramu 454,208  kutoka Entebbe Uganda kuja Zanzibar imeendelea kuairisha  Mahkama kuu Tunguu Unguja baada ya shahidi wa kesi hiyo kushindwa kufika Mahakamani  hapo kwa dharura ya Ugonjwa.

 Kesi hiyo, inayomkabili  Jackie Ninsima (33) Raia huyo wa Uganda mwenye passport namba BOOO65972  alisafiri kwa ndege ya  Ethiopian airline kutoka  Uganda  kuja Zanzibar kupitia  Ethiopian  na kushikwa  na polisi wa  Uwanja wa ndege wa kimataifa wa  Amaan Abeid Karume akiwa na pipi 12 za madawa ya kulevya na  pipi nyengine akiwa kazimeza na kuzitowa kwa  njia ya haja kubwa akiwa katika hospitali ya Mnazi mmoja.

 Mara baada ya kufika Mahakamani hapo akitokea Rumande, mshtakiwa huyo alisomewa shitaka lake hilo na mwendesha mashtaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar, DPP Ali Amour  mbele ya Jaji wa mahkama hiyo, Mohamed Ali Mohamed.

 Amedai kuwa  shahidi wa kesi hiyo hawajafika mahkamani hapo kwa sababu ya ugonywa,na kumuomba jaji wa mahakama hiyo kuihairisha kesi hiyo.

‘’ Muheshimiwa Jaji  leo shahidi ambae tunamtegemea leo hajafika mahakamani hapa , hivyo tunaomba shauri hili ulihairishe na kuipanga siku nyengine ajili ya  kusikilizwa shahidi namba tatu, ambae tulipanga tumsikilize leo’’alidai Dpp huyo.

Jaji wa mahakama hiyo, Mohamed Ali Mohamed alikubali ombi hilo, na kumuliza mshtakiwa  huyo,kuwa yuko  tayari kwa ajili ya kuhairishwa kesi hiyo na kujibu ndio.

 Awali mahakamani hapo, ilidaiwa kuwa mshitakiwa huyo raia wa Uganda  anashtakiwa kwa kosa la kuingiza  dawa za kulevya  Zanzibar aina ya Cocaine  kete  38 zenye uzito wa gramu 454,208 kutoka Entebbe Uganda kuja Zanzibar na kufanya hivyo, ni kosa kinyume na kifungu cha  21 (1) (a)  cha sheria ya mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya, sheria namba 8 ya mwaka 2021 sheria za Zanzibar.

  Jaji wa mahkama hiyo, aliihairisha Kesi hiyo hadi septemba 13 mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa kwa shahidi namba tatu.

                            MWISHO 


No comments

Powered by Blogger.