MTUHUMIWA WA KESI YA KUBAKA NA KUTOROSHA ACHILIWA HURU


 


NA MARYAM NASSOR                      

MAHAKAMA maalum ya kupinga udhalilishaji , mkoa wa Kaskazini Unguja , imemuachia huru kijana Tamimu Ame Juma(28)wa Mahonda Karachi  kwa madai ya kuwa ushahidi  uliyoletwa mahakamani hapo haukumtia hatiani.

Akisoma Uwamuzi mdogo,(Ruling) hakimu wa Mahakama hiyo  Lusiano Makoe Nyengo alisema kuwa katika kesi hiyo mahakama ilisikiliza mashahidi watatu na kielelezo kimoja.

Alisema kuwa, katika mashahidi wote hao , hakuna  ushahidi Mzuri ambao unaweza kumtia hatiani mtuhumiwa huyo moja kwa moja  Hivyo,anamuwachia huru chini ya kifungu cha 215 cha Mwaka 2018.

Alisema kuwa, mshitakiwa huyo ,alishtakiwa kwa makosa Mawili , kosa la kwanza lilikuwa ni kutorosha  na la pili ni kubaka lakini , muhanga alipokuwa anatoa ushahidi wake, Hakusema ni lini na wapi aliingiliwa  na mtuhumiwa huyo.

Aidha alisema kuwa,  ushahidi mzuri ni wa muhanga na mahakama inauzingatia lakini shahidi namba mbili alikuwa ni muhanga, alipokuja mahkamani  alisema ni kweli kabakwa, lakini hakuweza kuieleza mahkama kuwa kabakwa eneo gani  na ilikuwa lini.

  Hakimu Lusiano, alisema kuwa baada ya kuuangalia ushahidi huo, mahakama ilijielekeza katika sehemu kuu mbili, ya kwanza ni umri na kuingiliwa, jee muhanga aliingiliwa kweli na mtuhumiwa, shahidi daktari alipokuja mbele ya Mahakama alisema kuwa , alipompima alimkuta  yuko kwenye siku zake hivyo alishindwa kusema kuwa mtoto kaingiliwa au laa.

 Alisema, na kuhusu  umri muhanga hakusema kuwa yeye ana miaka mingapi , na shahidi namba moja alikuwa ni mama yake na yeye  hakusema pia kuwa mwanawe ana miaka mingapi.

Alisema kuwa, mpelelezi alipokuja mahakamani alisema , Muhanga alibakwa kama alivyoambiwa na muhanga mwenyewe wakati ana muhoji, lakini hakueleza mazingira gani muathirika alibakwa. 

Hakimu huyo, alisema kuwa na kosa la pili lilikuwa ni kubaka, lakini pia ushahidi haujitoshelezi ambao hauoneshi, Mtoto ni kwa namna gani alivyobakwa.

“Kwa mantiki hiyo, ushahidi uliyokuwepo mbele ya mahakama hii, hauoneshi kuwa mtuhumiwa ana kosa la kujibu na badala yake inamuachia huru” alisema.


. Mshtakiwa huyo,  Tamimu Ame Jecha, alishtakiwa kwa makosa mawili,  la kwanza likiwa ni kutorosha  msichana aliye chini ya uwangalizi wa wazazi wake  kinyume na kifungu  113 (1) (a) cha sheria za adhabu  namba 6 ya mwaka 2018 sheria za Zanzibar, na  kosa la pili ni kubaka kinyume na kifungu  cha 108 (1) (2) (e) na 109 (1) ya sheria  ya makosa na adhabu  namba 6 ya mwaka 2018 sheria za Zanzibar.

Awali mshtakiwa huyo, Ilidaiwa Mahkamani hapo kuwa siku ya tarehe 25/01/2024 majira ya saa 11 za jioni huko Mahonda Karachi , Wilaya ya Kaskazini ''B'' Unguja  bila ya halali alimchukua mtoto wa kike Mwenye Umri wa Miaka 16  ambae hajaolewa  na aliye chini ya uangalizi wa wazazi wake, kutoka Posta Mahonda na kumpeleka nyumbani kwake. Bila ya ridhaa ya wazazi wake jambo ambalo ni kosa kisheria.

                       MWISHO


No comments

Powered by Blogger.