Talaka si Suluhisho la migogoro, ipisheni mitihani ipite Safari iendelee.
Imeandikwa na Maryam Nassor - Zanzibar
Muda mrefu imekua ikiaminika
na wanandoa wengi kuwa talaka ndiyo kimbilio la matatizo yote yanayowakumba katika
maisha ya ndoa.
Katika dini ya kiislamu,
talaka ipo kisheria, ingawa maandiko matakatifu na yasio na shaka, ni haramu
ambayo Muumba ameichukia.
Na wapo wanaoamini hata wakati wa kutolewa kwake ama
kuandika, Imani inakubali kuwa, mbingu hutikisika, ni ishara kuwa si uamuzi
sahihi sana.
Ijapo kuwa, maana ya ndoa ni mkataba wa hiari ambao hufungwa kwa makubaliana baina ya mume
na mke, ingawa pale inapofika kuwa ndoa
hiyo haina misingi ya kuendelea tena, basi hupelekea kutoka kwa talaka.
Na huwa hamufikirii hata kwa dakika chache tu, kuwa lile janga la vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia kwa
watoto hao.
Utakuwa na uhakika gani kuwa, ule ulezi wa pande moja
siku hizi unaitwaa ‘single mother’ utakavyooathiri malezi na makuzi ya watoto.
Akizungumza na mwandishi wa Makala haya, alisema Watoto hao mkubwa wao alikuwa ana umri wamiaka
16 na wapili alikuwa na miaka 13 na watatu alikuwa ana miaka 10 basi yule
watatu alikuwa akimlawiti yule ndugu yao wa mwisho aliyekuwa na umri wa miaka sita.
Alisema kuwa, kila ikifika usiku alikuwa akimsikia
akilia kwa uchungu, na yeye kama mzazi alikuwa akijiuliza huyu mtoto ana shida
gani usiku.
“Nilitokwa na machozi, kuwaona Watoto wale
wanavyomtesa ndugu yao, kumbe kaka zake
walikuwa wanamlawiti’’ alisema kwa masikitiko.
Aidha, alisema kuwa chakushangaza Watoto wale walikuwa
wanaishi na bibi na babu yao, lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa anajali.
Ali Issa Kinole, Sheha wa shehia ya Mahonda alisema
kuwa, baada ya kupata habari za manyanyaso ya Watoto hao, walitoa taarifa kwa
watu wa ustawi wa jamii na kuja kuzungumza nao, ili wawashuhulikie Watoto wale
vizuri.
Mrajisi wa
mahkama ya kadhi, Iddi Said Khamis anasema
talaka za kiholela zinaweza kusababisha
vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa
kijinsia.
Alisema, takribani kesi nyingi za watoto unao wasikia
kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji basi,mara nyingi huwa wanaishi na mzazi
mmoja inaweza kuwa wanaishi na mama pekee au baba na mama wa kambo.
Alisema kuwa, kwa sasa hali ni mbaya, talaka za
kiholela zimekuwa ni nyingi, wanandoa hushindwa kustahamiliana na
kuona suluhu pekee ni talaka.
Ingawa kwenye dini ya kiislamu, talaka
imeruhusiwa lakini ni jambo ambalo
linamchukiza sana Muumba.
Aidha alisema kuwa,kitakwimu talaka zinazotolea
kiholela zimekuwa zikiongezeka siku hadi siku.
Alisema, kwa mwaka 2023 jumla yakesi 909 zimeripotiwa
katika mahkama ya kadhi wilaya ya Mwanakwerekwe Unguja pekee.
Na kesi 66 zimeripotiwa katika mahkama ya Mwera Unguja,
huku kwa upande wa mahkama ya kadhi ya wilaya ya Makunduchi zilikuwa 60.
Aidha alisema kuwa, kwa upande wa Pemba kuliripotiwa kesi
119 kwa Mahkama ya kadhi ya wilaya ya Wete na kesi 45 kwa mahkama ya Konde.
Mrajisi huyo alisema kuwa, katika mahkama ya kadhi ya
wilaya ya Chake chake ilionekana kuongoza kwa upande wa Pemba, ikiwa na kesi
126 za talaka.
Alieleza kuwa, kwa upande wa wilaya ya Mkoani , ziliripotiwa
jumla ya kesi 64 na katika mahkama ya
kadhi ya Kengeja zilifikishwa kesi 10.
Aidha, alisema kwa mwaka 2022 kulikuwa na kesi 416
zilizoripotiwa katika mahkama ya kadhi za wilaya Unguja na Pemba.
Alisema kuwa, ‘’utaona jinsi gani talaka zinavyotolewa
kiholela, na kusahau kuwa zimeruhusiwa lakini kwa utaratibu maalum uliyowekwa’’,alisema.
Mratibu wa chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania,
TAMWA Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali alisema, talaka siku zote sio nzuri kwa
wanandoa, wanapaswa kukaa pamoja na kutafuta suluhu ya matatizo yao, mbali ya
talaka.
Alisema kuwa, wazazi wanapotengana kwa sababu zozote
zile, basi wanao umia zaidi ni watoto, kwani huwa ni wadogo na wanahitaji
malezi na mapenzi ya wazazi wawili.
Aidha alisema kuwa, watoto hupitia kipindi kigumu
katika maisha yao, pale ambapo wazazi hupeaana talaka.
Alisema kuwa, watoto waliyopitia vipindi vigumu vya kutengana
kwa baba na mama, haawezi kusahau katika
maisha yao yote, shida na mateso waliyapata.
“Hivyo, tunashauri wazazi wakae pamoja kuzungumza
tofauti zao, lakini si kuona suluhu pekee ni kupeana talaka,”alishauri.
Alifafanua kuwa, wao TAMWA- Zanzibar wataendelea kutoa
elimu juu ya madhara yatokanayo na talaka, kupitia vyombo vya habari, ili kuwe
na jamii bora ,ambayo inajikinga na vitendo vya udhalilishaji.
Fatma Ali Bakar, Mwanasheria kutoka chama cha wanasheria wanawake Zanzibar ‘ZAFELA’ alisema kuwa
wanawake wanatakiwa kusoma ili kutimiza ndoto zao za kielimu.
Alisema kuwa, sababu moja wapo ya talaka ni kuwa wanawake
wengi hukatishwa masomo na kupewa mume, hivyo bado wanakuwa hawajaandaliwa kisaikolojia kuingia kwenye ndoa.
Nae, Mratibu wa maswala ya udhalilishaji shehia ya
Mahonda Semeni Bundala, alisema kuwa kwa upande wa shehia hiyo, huwa wana toa
ushauri kwa wana ndoa kuwa, wakae na kuzungumza tofauti zao.
Alisema kuwa, wanapo achana baba na mama basi watoto
ndiyo, wanaoteseka na kupelekea kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji.
Sheikh Nahoda
Haji wa msikiti wa Mahonda, alisema kuwa talaka ni jambo baya linalomchukiza
mungu, hivyo ni bora wazazi kuacha jazba
kwa kutaka kuoneshana nani bora kuliko mwenzake.
Aidha alisema kuwa,
talaka huchangia vitendo vya udhalilishaji kwa watoto kwani, wazazi
wakiwa mbali mbali kila mmoja huwa hana muda na watoto wao.
Nae, Askofu Stephen Aron wa kanisa la Mahonda, alisema
kuwa katika dini yao talaka hairuhusiwi kutokana na kuwa wanaamini atakae
muunganisha mungu, basi hakuna atakae mtenganisha.
Hivyo, jambo la talaka limekemewa vikali na dini yao,
na hivyo wao hawaruhusu litokee, mpaka mmoja wao atakapo fariki.
Nao, baadhi ya wazazi waliyo wahi kuachwa na kuwaachia
ulezi wa pekee yao, Bifarida Sudi wa Chuini mkoa wa mjini wa Magharibi alisema,
kuwa talaka ni jambo baya sana, kwani watoto hukosa malezi ya pamoja ya baba na
mama.
Alisema kuwa, yeye alipoachwa alikuwa anashinda ndani
na kulia, alikuwa hajui la kufanya na watoto wadogo akiangalia hana kazi wala
ndugu wa kumsaidia.
“Wazazi tunatakiwa kuzungumzia tofauti zao ili tupate
suluhu, kwani watoto huteseka sana wakiishii na mzazi mmoja kwani hatuwezi
kuwamalizia shida zao, hata kama mzazi atakuwa na kipato kizuri,’’ alisema.
Nae, Mzee Ali Faki Sungura alisema yeye alimuacha
mkewe tu, kwasababu alikuwa haoni njia nyengine ya kupita zaidi ya talaka.
Alisema, baada ya kumuacha talaka zote tatu ndipo alipokuja kutoka kwenye
usingizi mzito aliyokuwa nao,na kukumbuuka ule msemo usemao” amekumbuka shuka
kumesha kucha.




Post a Comment